Na Walter Mguluchuma
Katavi
JESHI
la polisi mkoani Katavi linamsaka mtu asijejulikana kwa tuhuma za
kumbaka,kumchoma kisu,kumuua na kisha kukata sehemu za siri za
mwanafunzi(14) wa
darasa la sita shule ya msingi
Vikonge wilaya ya Tanganyika na kukimbilia kusiko julikana.
Akitoa taarifa ya tukio hilo kamanda wa polisi Damas Nyanda alisema
kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 1;30 za asubuhi wakati
marehemu akiwa anakwenda shule akiwa ameongozana na mdogo wake ambaye
wanasoma shule moja.
Kamanda Nyanda alisema wakiwa njiani alitokea mwendesha pikipiki maarufu kwa jina bodaboda ambae walikuwa hawamfahamu na kusimamisha pikipiki yake na kuwaambia anataka awape lifti ili wafike haraka shuleni kwao.
Alisema
baada ya kuambiwa hivyo
wanafunzi hao walikubali hata
hivyo alimtaka apande kwenye bodaboda hiyo mtoto huyo wa kike peke yake na aliondoka na kumwacha mdogo wake wa kiume.
Baada ya kunyimwa lifti hiyo mdogo wake aliamua kutembea kufuata nyuma hata hivyo akiwa njiani
aliona pikipiki kama
ile iliyokuwa imembeba dada yake ikiwa kwenye kichaka pembeni ya
barabara lakini hakwenda kuangalia badala yake aliendelea na
safari yake ya kwenda shule.
Mdogo wake huyo na marehemu kutokana
na umri kuwa mdogo alipofika shuleni hakumtafuta dada yake na
badala yake aliingia darasani na
kuendelea na masomo kama
kawaida na baada ya muda wa masomo ulipofikia
majira ya saa 8;30 alianza
safari ya kurejea nyumbani pasipo kumtafuta dada yake.
Kamanda Nyanda alieleza kuwa
baada ya kufika nyumbani kwao wazazi wake walishituka kumwona
akiwa peke yake
ndipo walipomuuliza aliko dada yake
na aliwaeleza mazingira yote ya jinsi
alivyo achana na
dada yake wakati walipokuwa njiani
na jinsi alivyoiona pikipiki
iliyombeba dada yake ilivyokuwa kichakani.
Wazazi wa marehemu
baada ya kupata maelezo
hayo walipatwa na mashaka ambapo
walimtaka mdogo wa marehemu awapeleke
kwenye eneo aliloona
pikipiki ile.
Alisema wazazi wa
marehemu waliokuwa wameongozana na majirani zao baada ya kufika kwenye
eneo hilo walishitushwa kuona
majani yakiwa yamelala
na ndipo walipokwenda mbele kidogo wali ukuta mwili wa marehemu ukiwa
amechomwa kifu sehemu ya
ubabu wake wa kulia na sehemu za
siri zikiwa zimenyofolewa.
Kwaupande wake kaimu mwalimu mkuu wa shule ya msingi Vikonge
Gadinendi Kaseka alisema
mpaka walipomaliza
masomo ya siku hiyo hawakuwa na
taarifa juu ya kifo cha mwanafunzi huyo ila walipata taarifa hiyo
siku hiyo hiyo
majira ya saa kumi na mbili jioni baada ya mwili wa marehemu kuwa umepatikana.
Kamanda huyo wa polisi alisema
kuwa wazazi na majirani walikwenda polisi kutoa taarifa ambapo polisi
walifika na kuuchukua mwili wa marehemu na msako wa mtu aliyefanya tukio
hilo unaendelea.