Sunday 7 January 2018

Mkaguzi wa ndani apewa jukumu

Na Gurian Adolf
Nkasi
SERIKALI wilayani Nkasi mkoani Rukwa imemuagiza mkaguzi wa hesabu za ndani afanye ukaguzi katika michango ya maendeleo  ya wananchi ili kujiridhisha Kama michango yote inatumika Kama ilivyokusudiwa. 

Mkuu wa wilaya ya Nkasi Said Mtanda aliyasema  hayo jana wakati akiongoza Songambele ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika sekondari ya Kirando iliyomo wilayani humo.

Alisema kuwa hivi sasa serikali haina mzaha katika suala la fedha za wananchi na nilazima ijue kila shilingi iliyotolewa kwaajili ya maendeleo inatumika Kama ilivyo kusudiwa.


"nimemuaziza mkaguzi wa hesabu za ndani akague fedha zilizokusanywa kutoka kwa wananchi kwaajili ya shughuli za maendeleo Kama tulivyokubaliana ili tujiridhishe kama ni sahihi, na iwapo kuna yoyote atakuwa amekwenda tofauti lazima sheria ichukue mkondo wake, tunataka kila mwananchi fedha yake ionekane imefanya shughuli gani ya maendeleo" alisema

Alisema kuwa kwa watendaji wenye tamaa na michango ya wananchi waondoke wilayani mimesema hayo leo mkuu wa wilayani Nkasi kwani hakuwafai wakatafute sehemu nyingine watakapovumiliwa.

Mkuu huyo wa wilaya aliwasihi wananchi wawilaya hiyo kujitoa Kwa hali na mali na wanapaswa kutambua kuwa maendeleo ya wilaya hiyo yatatokana na juhudi zao wasisubiri mgeni kutoka nje ndio awafanyie maendeleo kwani wilaya hiyo imejaliwa kila kitu. 

Alisema ili iweze kupiga hatua nilazima wawekeze kwenye elimu kwani duniani pote maendeleo yanaletwa nawatu wenye elimu hivyo sualala la elimu lazima liwe kipaumbele chao namba moja ndipo watafanikiwa.

Aidha mkuu huyo wa wilaya aliwasihi wananchi kutunza mazingira kwakua maendeleo na mazingira ni vitu pacha wajitahidi kufuga kwa Kuzingatia eneo la malisho sambamba na kufanya Kilimo endelevu ili ardhi itumike muda mrefu kwani wasipo zingatia hayo watajuta siku zijazo.

Naye mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo aliyeshiriki songambele hiyo aliwasihi wananchi kufanya kazi wasitegemee wahisani kutoka nje ya wilaya hiyo kwani zama hizo zimepitwa na wakati. 

Nao wananchi wa wilaya hiyo waliwaomba viongozi wa serikali kuwa nao bega kwa bega kwani wanachohitaji ni maendeleo kutokanana na wilaya yao kuwa nafursa nyingi hivyo nijukumu lao kuwaongoza vizuri. 

Mwisho

No comments:

Post a Comment