Thursday 19 April 2018

TASAF Katavi kulipa kaya masikini Benk

Na Walter Mguluchuma
Katavi
Mfuko wa  hifadhi ya  Jamii  TASAF  katika   Halmashauri ya  Manispaa ya  Mpanda Mkoani  Katavi umefanikiwa kuzilipa kaya masikini zaidi ya shilingi milioni 67  imeanzisha  utaratibu  mpya kwa  njia ya  mtandao  sambamba  na kuwafungulia  akaunti   Benki  bure.
Afisa  ufuatiliaji  wa  TASAF  katika  Manispaa ya   Mpanda   Twambulile   Solomon alisema  hayo hivi karibuni ambapo  alisema kuwa utaratibu huo   mpya kwa walengwa wa  mfuko huo ulianza  mwezi julai  mwaka  jana   katika   Manispaa hiyo.
Alisema kuwa mpaka sasa utaratibu  huo hapa  nchini  umefanyika   katika   halmashauri 16 kwa  ajiri ya  majaribio  na   kwa  mkoa  wa   Katavi unafanyika  katika Manispaa ya  Mpanda   huku  lengo  likiwa  ni    kutaka  malipo  kwa  njia ya  mtandao  yafanyike  katika  halmashauri zote za  Mkoa wa  Katavi kwa njia hiyo .
Twambulile  alisema   kuwa  katika kipindi cha  kuanzia  Julai  mwaka  jana  hadi  sasa  wamelipa  walengwa malipo yao  kwa  njia ya  mtandao  kiasi cha  shilingi milioni 67,459,500.
 Alifafanua  kuwa    hadi  kufikia  mwezi wa  pili  mwaka  huu   dirisha  lilikuwa  linawalipa  walengwa 344  kwa  njia ya  mtandao  ambapo  kwa  kipindi cha  mwezi  Machi  na April  walengwa  wengine 300  wamejiunga  na  utaratibu huo wa kulipwa  kwa  njia ya  mtandao.
Afisa   ufuatiliaji   huyo wa  Tasaf   alisema kwa  kipindi cha  mwezi  Aprili  wameweza  kuwafungulia  walengwa  71   akaunti  katika Benki ya  CRDB  Tawi  la   Mpanda   bila   malipo  yoyote  na   akaunti zao   hazitakuwa  na   makato yoyote.
 Aliitaja  mitaa  ambayo   walengwa  wamefunguliwa    akauti   Benki  kuwa ni    Kawajense   walengwa  30   Kamakuka  walengwa  14,  Mbugani  Kakese walengwa  walengwa  24 na  Kijiji  cha  Mwamkulu  walengwa  4.
 Mmoja  wa  walengwa  hao  Salome   John   alisema  kuwa    utaratibu huo utawazidi  kuwahakikishia  usalama wa  fedha  zao kuliko ilivyokuwa  awali na  utawapunguzia  usumbufu wa kupanga  foleni   kwenye  malipo.
Mwenyekiti wa  Mtaa wa   Kawajense   Simon  Jumapili   alisema  utaratibu  huo wa malipo kwa  njia ya  mtandao   utawasaidia walengwa  kwenda  kuchukua   fedha  zao  kwa  muda  wanaotaka  wao  tofauti na  hapo  awali  walipokuwa wakipangiwa muda wa  kwenda kuchukua  fedha.
Pia alisema utawafanya  walengwa wa mfuko  kwenda  kuchukua  fedha zao  pindi   wanapokuwa  wamemaliza   shughuli  zao  za  nyumbani  na hivyo kuto athiri muda wa uzalishaji mali.

Mwisho


No comments:

Post a Comment