Wednesday 24 January 2018

Mwanafunzi auawa kikatili

Na Walter Mguluchuma
Katavi

JESHI la polisi mkoani Katavi linamsaka mtu asijejulikana kwa tuhuma za kumbaka,kumchoma kisu,kumuua na kisha kukata sehemu za siri za mwanafunzi(14) wa  darasa la sita shule ya msingi  Vikonge wilaya ya  Tanganyika na kukimbilia kusiko julikana.

Akitoa taarifa ya tukio hilo kamanda wa polisi Damas Nyanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 1;30 za asubuhi wakati marehemu akiwa anakwenda shule akiwa ameongozana na mdogo wake ambaye wanasoma shule moja.

Alisema kuwa siku ya  tukio hilo marehemu  alitoka  nyumbani akiwa na mdogo wake wa kiume  mwenye  umri wa miaka 11  mwanafunzi wa   darasa  la  nne  ambaye waliongozana wakielekea  shule ya  msingi  vikonge ambayo wanasoma.
Kamanda Nyanda alisema wakiwa  njiani  alitokea  mwendesha  pikipiki maarufu kwa jina bodaboda  ambae walikuwa  hawamfahamu  na  kusimamisha  pikipiki yake  na  kuwaambia anataka  awape  lifti ili wafike haraka shuleni  kwao.

Alisema  baada ya  kuambiwa  hivyo  wanafunzi hao walikubali  hata  hivyo alimtaka apande kwenye bodaboda hiyo mtoto huyo wa kike peke yake na aliondoka na kumwacha mdogo wake wa kiume.

Baada ya kunyimwa lifti hiyo mdogo wake aliamua kutembea kufuata nyuma hata hivyo akiwa  njiani  aliona  pikipiki  kama  ile  iliyokuwa imembeba  dada yake ikiwa kwenye kichaka  pembeni ya  barabara  lakini hakwenda kuangalia badala yake aliendelea  na  safari yake ya  kwenda  shule.

Mdogo wake huyo na marehemu  kutokana  na umri  kuwa mdogo alipofika shuleni hakumtafuta  dada yake na   badala yake  aliingia  darasani na  kuendelea  na  masomo  kama    kawaida   na   baada ya muda wa  masomo  ulipofikia  majira ya  saa 8;30  alianza  safari ya  kurejea  nyumbani pasipo kumtafuta  dada yake.

Kamanda  Nyanda   alieleza kuwa  baada ya kufika  nyumbani kwao wazazi wake walishituka  kumwona  akiwa  peke  yake  ndipo  walipomuuliza  aliko  dada  yake  na   aliwaeleza  mazingira yote  ya jinsi  alivyo  achana  na  dada  yake wakati walipokuwa  njiani  na  jinsi alivyoiona   pikipiki  iliyombeba dada yake ilivyokuwa  kichakani.

Wazazi wa  marehemu  baada ya  kupata  maelezo  hayo walipatwa na mashaka   ambapo  walimtaka  mdogo wa marehemu  awapeleke  kwenye  eneo   aliloona  pikipiki ile.

Alisema  wazazi wa marehemu waliokuwa wameongozana  na majirani zao  baada ya kufika  kwenye  eneo  hilo walishitushwa  kuona  majani yakiwa  yamelala  na  ndipo walipokwenda  mbele kidogo wali ukuta  mwili wa marehemu  ukiwa  amechomwa  kifu  sehemu ya  ubabu wake wa kulia  na  sehemu za  siri  zikiwa  zimenyofolewa.

 Kwaupande wake kaimu   mwalimu   mkuu wa  shule ya msingi Vikonge   Gadinendi   Kaseka  alisema    mpaka   walipomaliza  masomo ya siku  hiyo  hawakuwa na  taarifa juu ya kifo cha mwanafunzi huyo ila walipata taarifa hiyo siku  hiyo  hiyo  majira ya saa kumi na  mbili jioni  baada ya mwili wa marehemu kuwa umepatikana.

Kamanda huyo wa  polisi alisema kuwa wazazi na majirani walikwenda polisi kutoa taarifa ambapo polisi walifika na kuuchukua mwili wa marehemu na msako wa mtu aliyefanya tukio hilo unaendelea.

Mwisho

No comments:

Post a Comment