Tuesday 31 July 2018

Elimu ya hitajika kwa wanafunzi waachane na dada poa

Na Gurian Adolf
Katavi
BARAZA la madiwani la  Manispaa  ya Mpanda mkoani Katavi  limeshauri  itolewe elimu  kwa wanafunzi wa  shule  za   Sekondari  na  Msingi katika manispaa hiyo ili  wajiepushe na tabia ya kunua wakina dada wanaouza miili ya maarufu kama dada poa ili kuwakinga na magonjwa mbalimbali ya ngono.
Ushauri huo ulitolewa jana kwenye  kikao  cha baraza la madiwani la  manispaa  hiyo  kilichofanyika  katika   ukumbi wa  mikutano wa  manispaa  ya Mpanda  kilichoongozwa  na  Meya  wa Manispaa hiyo Willy   Mbogo.
 Awali  katika  kikao  hicho   Mwenyekiti wa  kamati ya  kudhibiti  ukimwi  Lucas  Kanoni wakati akiwasilisha  taarifa  ya  kamati  hiyo  alisema  kuwa  biashara ya akina  dada ya kuuza  miili yao  imekuwa ni tishio kubwa hivi sasa katika Manispaa hiyo .
Alisema  kuwa  madada  poa  hao   kwasasa  wameanza    kufanya   biashara ya  kuuza  mili yao  kwa  kujishusha  na  kuanza  kufanya  ngono  na  wanafunzi wa  shule hadi za  msingi  jambo   ambalo ni  hatari kwa   watoto hao kutokana na kuwepo kwa magonjwa ya ngono kama ukimwi.
Kanoni  alisema kuwa  yapo maeneo  mbalimbali  katika Manispaa  hiyo   ambayo yamekuwa ni  maarufu  kwa  biashara  hiyo ambayo    aliyataja  kuwa ni  mtaa wa   Fisi  ulioko     katika  Kata  ya   Majengo  B  ,M taa  wa   Simba  ulioko  Kata  ya   Majengo  B, Kakese  na  Mwamkulu .
Naye diwani wa  Kata  ya   Kashaulili  John  Matongo aliliambia   baraza  hilo la  madiwani kuwa  hivi sasa  elimu  ni  muhimu ikatolewa  kuanzia  shule za msingi  ili kuwaelimisha  wanafunzi  waweze kuacha kuwa wateja wao na pia kujikinga magonjwa ya ngono.
 Alisema   endapo    hatua  za  haraka   hazitachukuliwa   kutokana  na  kushamilikwa  biashara hiyo upo   uwezekano   mkubwa  wa kuongezeka  kwa mitaa  mingine  ambayo haina  sifa ya   biashara  hiyo  ya  dada  poa  kama  ilivyo kwa mitaa ya   simba  na  fisi .
 Kwaupande wake meya  wa  Manispaa  ya   Mpanda   Wily Mbogo    alisema  kuwa ni  vema watoto  waanze kufundishwa  toka  wakati wakiwa wadogo wakiwa mashuleni  kutojihusisha  na  kufanya  mambo   ambayo hayalingani na  umri wao kama  vile kufanya  ngono.
 Alifafanua kuwa  endapo kama  hawatapewa elimu  mapema ya  kujiepusha  na  kufanya  ngano wakiwa  na   umri  mdogo  upo   uwezekano wa kupata  maambukizi ya  vvu.
Katika kikao hicho mkuu wa   Wilaya  ya   Mpanda  Lilian  Matinga  alisema kuwa kwa sasa   Mkoa  wa  Katavi    ni  miongoni  mwa   mikoa  yenye  maambukizo ya   vvu  kwa kiwango cha  juu ya  wastani  wa Kitaifa .
 Alisema  maambukizi  ya   vvu  kwa  mkoa  wa   Katavi   ni  asilimia 5.9   wakati wastani wa  kitaifa  ni  asilimia  5.9  hivyo  mkoa huo  uko   juu ya  wastani  wa maambukizi ya Kitaifa.
Aliongeza kuwa  kwa  kipindi cha  miaka  mitatu  sasa  wastani  huo  wa   maambukizi  umekuwa   upo  pale  pale  bila kushuka jambo  ambalo   ni  hatari kwa wananchi  endapo  hawata   badili   tabia.
Ndiyo  maana  serikali   imepanga  kufanya  utafiti  kwenye  mikoa mitano yenye  maambukizi  makubwa  ya   maambukizi ya   vvu  ambayo ni  Songwe,  Katavi   Njombe ,Mbeya  na  Kigoma.
Mwisho

Onyo kwa makampuni ya ujenzi barabara

Na Gurian Adolf
Katavi

WAZIRI wa  ujenzi  uchukuzi na   Mawasiliano mhandisi  Isack  Kamwelwe ameyaagiza  Makampuni  ya  ujenzi   kuhakikisha kuwa  wanamwagia  maji  kwenye   sehemu za   makazi ya  watu  pindi wanapokuwa wakitengeneza  barabara ili kuwaondolea  vumbi na kuwaepusha  na  magonjwa .
Alitoa   agizo  hilo jana kwa  nyakati   tofauti katika  maeneo ya   Majalila   Wilayani   Tanganyika  na   katika   Kijiji  cha   Inyonga  Wilayani   Mlele mkoani Katavi wakati akikagua   ujenzi wa  barabara  kwa  kiwango cha   lami  kutoka   Mpanda mkoani katavi   hadi   sikonge   Mkoani Tabora.

Alisema kuwa  kumekuwa  na  tabia ya  wakandarasi wa  makampuni ya  kichina wanaotengeneza  barabara  kwenye   maeneo  mbalimbali hapa   nchini  kutomwagilia  maji  kwenye  maeneo ya  makazi   wanayoishi   watu hivyo kuwasababishia kero kubwa ya vumbi.
  Alisema kuwa ni wajibu  wa  kila  kampuni  inayotengeneza  barabara  kumwagia  maji  kwenye maeneo  wanayoishi  watu  kwani  kwenye  mikataba  yao wanatakiwa  kufanya  hivyo  na    wanalipwa  fedha na  Serikali    hivyo  swala  la  uwagiliaji wa   maji ni  la lazima.
Waziri  huyo alisema  kuwa  matokeo ya  kutomwagia  maji  kwenye  maeneo   ya  makazi  kwanasababisha  wananchi  kupata  maradhi ya   ugonjwa  wa   vifua na mafua.
  Alisema kuwa licha ya  ujenzi  wa  barabara  ya   Mpanda    Tabora  kwa  kiwango cha  lami  pia  serikali imepanga  kutengeneza  barabara  yenye   urefu wa  kilometa   128 kwa  kiwango cha  lami kutoka   Mpanda   hadi   Karema  mwambao mwa  ziwa   Tanganyika   Mkoani  Katavi .
  Aliongeza kuwa barabara  hiyo ni  muhimu  sana   kwaajiri ya  kusafirisha  mizigo  kwenda  nchi ya Demokrasia ya  Kongo kupitia   bandari  inayojengwa  karema  kwani  lengo la   Serikali ni  kutaka  kusafirishia   mizigo    kupitia    bandari ya  karema  kwenda  kwenye  miji ya  Momba  na  Karemii  nchini  Kongo .
Pia  alisema serikali imepanga  kuanzisha   safari za  ndege  katika  uwanja wa  ndege wa   Mpanda  ifikapo  mwezi  desemba  mwaka  huu  baada ya   Wizara ya  ujenzi na  uchuzi na  mawasiliano  kuagiza  magari  sita   ya     zima    moto   ambapo moja  litapelekwa uwanja  wa  ndege wa  Mpanda na    safari  za  ndege kutoka  Dares  salaam   hadi    Mpanda   kwani  tatizo  lilikuwa  likisababisha kutokuwepo  safari za  ndege ilikuwa  ni   uwanja  wa  Mpanda  kutokuwa na  gari ya  zima  moto .
Alisema  kuanza  kwa  safari za  ndege  kutasaidia watalii  kuongezeka  katika  hifadhi ya  Katavi kwani walikuwa wanashindwa kwenda  kwa  wingi  kutokana na kutokuwepo kwa  usafiri wa  ndege.
Naye Meneja    wa  TANROADS   mkoa  wa   Katavi   muhandisi  Martin  Mwakabenda   alisema  kuwa  kumekuwepo na   changamoto  mbalimbali  kwenye  ujenzi wa  barabara ya  kutoka    Mpanda  kwenda  mkoani Tabora  yenye    urefu wa  Zaidi ya  kilometa   340  inayotarajiwa  kukamilika  baada  ya  miezi  36.
Alitaja  baadhi ya  changamoto kuwa  ni  wizi wa  mafuta  unaofanywa  na       watumishi  wasio  waaminifu wa  vibarua  wanaoshirikiana  na    wananchi  wanaoishi  jirani  na  Kambi  za   ujenzi wa  barabara .

Mmoja wa wakazi wa    Kijiji  cha   Inyonga John  Samoja alimweleza   Waziri   Kamlwelwe kuwa  wamekuwa  wakipata tabu sana kutokana na vumbi  kwenye  maeneo  wanayoishi  hivyo  wanaomba  wakandarasi  wawe  watii agizo la waziri siku zote na si  tu  kumwagia  maji  pindi  wanapo  sikia   waziri anafanya ziara ya kukagua barabara wanazo jenga.
 MWISHO

Washushwa vyeo kwa kutochukua hatua

Na Gurian Adolf
Nkasi

MKUU wa wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa Said Mtanda  ameagiza kushushwa cheo afisa elimu wa kata ya Kala pamoja na mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi ya Kilambo cha Mkolechi  huku afisa mtendaji wa kijiji na afisa mtendaji wa kata wakitakiwa kukamatwa kufuatia tukio la Mwalimu mkuu wa shule hiyo Erad Kapyela kumpa mimba mwanafunzi na wao kutochukua hatua za haraka kumkamata kitendo kilicho sababisha mwalimu huyo kutoroka.

 Agizo hilo alilitoa jana katika baraza la madiwani  la halmashauri ya wilaya ya Nkasi baada ya kumebaini kuwa viongozi hao walikua wanalifahamu tukio hilo na wakakaa kimya bila kuchukua hatua yoyote  kutokana na uzembe huo wanatakiwa kuchukuliwa hatua.

Alisema kuwa wao wamefanya uchunguzi na kubaini kuwa mwalimu mkuu huyo amekuwa na tabia hiyo ya kuwapa mimba Wanafunzi ambapo mpaka sasa wanafunzi watatu wamezalishwa na  mwalimu huyo  huku wao wakikaa kimya pasipo  kuchukua hatua zozote na kuwa na wao wanaingia moja kwa moja katika adhabu.

 Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa inashangaza kuona jambo kama hilo linafanywa na mwalimu mkuu wakati wao wanafahamu vita vilivyopo sasa katika wilaya Nkasi ya kupambana na mimba kwa Wanafunzi  na viongozi  wa maeneo hayo wanakaa kimya  na kuwa sasa ni lazima Watendaji hao wawe mfano ili na waweze kujifunza namna ya kuchukua hatua za haraka pale wanapoona mambo hayaendi sawa

“kama viongozi hao wa vijiji na kata wangechukua hatua za haraka mwalimu mkuu huyo angekamatwa na asingepata nafasi ya kutoroka na watendaji wa namna hiyo hawatakiwi katika serikali ya awamu hii ya tano.

Sambamba na hilo aliwataka madiwani kuendelea kuisimamia halmashauri yao vizuri na kuwa mpaka sasa wilaya ipo vizuri hasa kwa kufanya vizuri katika makusanyo na kuongoza katika halmshauri zote nne za mkoa wa Rukwa ambapo  makusanyoi ya ndani yamefikia asilimia 89.97 kiwango ambacho ni kikubwa.

Aliwataka madiwani kuyasimamia mapato hayo vizuri  ili kuona kuwa zinarudi kwa wananchi  kwa kusaidia nguvu za Wananchi katika miradi mbalimbali ya maendeleo waliyoianzisha ili waone kuwa makusanyo yao yanawasaidia ili waweze kutoa mchango zaidi wa kuhakikisha kuwa halmashauri inakusanya zaidi na kuwa walinzi kwa wale wanaotorosha mapato.

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri hiyo Zeno Mwanakulya aliahidi kuendelea kuisimamia halmashashauri vizuri na kuwa maagizo yote ya serikali watayatekeleza.

Naye mkurugenzi wa wilaya  hiyo Missana Kwangula alisema  kuwa  wao kama halmashasuri wataendelea kusimamia misingi ya kiutumishi na kusimamiana ili kila mmoja aweze kutimiza wajibu wake kwa kutoa huduma bora kwa Wananchi

Mwisho

Wednesday 6 June 2018

Basi laua lajeruhi

Na Israel  Mwaisaka
Nkasi

MTOTO mwenye umri wa miaka minne amefariki dunia papo hapo baada ya basi lenye Namba za usajili  T178 DHD lililokuwa likisafiri kutoka Kabwe wilayani Nkasi kuelekea mjini Sumbawanga mkoani Rukwa kuacha njia na kupindukaa huku abiria 25 wakijeruhi na tisa kati yao wakiwa ni majeruhi.

Akizungumzia tukio hilo afisa mtendaji wa kata ya Kabwe  Jofrey Kuzumbi alisema kuwa ajali hiyo ilitokea mei 5 majira ya saa 12 asubuhi katika eneo la Malimba katika kata hiyo ya Kabwe.

Alisema kuwa  gari hilo lilikua limebeba  abiria 43 na waliojeruhiwa ni 25 na kati yao tisa ni mahututi na wamekimbizwa katika hospitali teule ya wilaya Nkasi huku wengine wakipelekwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa kwa matibabu zaidi kutokana na majeraha waliyoyapata.

Alisema kuwa baada ya ajali hiyo kutokea mtoto wa kike aliyefahamika kwa jina la Beatrice Nyansio (4) alifariki papo hapo huku mzazi wake akipata majeraha.

Afisa mtendaji huyo alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa basi hilo na baada ya ajali hiyo dereva wa gari hilo aliyefahamika kwa jina moja tu la Moses alikimbia na mpaka sasa haijulikani alipo.

Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa George Kyando alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuongeza kuwa bado uchunguzi wa ajali hiyo  ikiwa ni pamoja na kuendelea kumsaka dereva wa gari hilo ambaye amekimbia ili aweze kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazo mkabili.

mwisho

Kipindu pindu chaua 397

Na Gurian Adolf
Sumbawanga
HALI ya ugonjwa wa kipindu pindu bado ni tete wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa ambapo idadi ya wagonjwa imeendelea kuongezeka ambapo hivi sasa imefikia vifo 15 na wagonjwa 397 waliougua ugonjwa huo tangu ulipolipuka tena  Mei 6 mwaka huu.
Mganga mkuu wa wilaya ya Sumbawanga Fani Mussa akizungumza na mwandishi wa habari hizi amesema kuwa ugonjwa huo bado haujaisha na watu wamekuwa wakiendelea kuugua.
Alisema kuwa mpaka kufikia jana jumla ya watu 397 wameugua kufa na wengine kupona ambapo mpaka hivi sasa kuna wagonjwa  saba ambao bado wapo wodini wakitibiwa ugonjwa huo.
Mganga mkuu huyo alisema kuwa changamoto kubwa iliyopo ni wananchi kutofuata kanuni bora za afya hasa kunywa maji yasiyosalama sambamba na kutojisaidia kwenye vyoo.
Alisema kuwa hivi sasa wakulima wanavuna mpunga na maji wanayotumia kwa kunywa ni ya kwenye majaruba ambayo si salama kiafya kwakuwa hayajachemshwa na baadhi yao wakijisaidia porini.
Dkt Mussa alisema kuwa idara ya afya inajitahidi kutoa elimu lakini bado wananchi hawafuati taratibu za kujikinga na ugonjwa huo licha ya kwamba sheria kali pia zinatumika lakini bado ugonjwa huo unaendelea.
Alisema katika kipindi cha November mwaka jana ugonjwa huo ulilipuka na ulidhibitiwa ilipofika mwezi March mwaka huu lakini bila matarajio ugonjwa huo ulilipuka tena mwezi mei mwaka huu na katika siku si nyingi umeua watu 15 tofauti na mwaka jana ambapo watu 7 ndiyo waliopoteza maisha.
Mwisho

Rukwa kujikita kwenye Alizeti

Na Gurian Adolf
Sumbawanga

MKOA wa Rukwa umejipanga kwaajili ya kuzalisha zao la alizeti ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa mafuta ya kula unaotokea mara kwa mara hapa nchini.

Mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo alisema hayo hivi karibuni wakati anazungumza na balozi wa Jamhuri ya Ireland Paul Sherlock ofisini kwake  wakati akiwasilisha ombi la ushirikiano baina ya mkoa wa Rukwa na nchi yake hali itakayo ongeza uzalishaji wa zao la alizeti mkoani humo na kupelekea kuinua kipato cha wakazi wa mkoa wa huo.

alisema kuwa Kwa mwaka 2016/2017 zililimwa hekta 47,862 za alizeti na kupatikana tani 53,470 ambayo ni chini ya kiwango kilichotakiwa kuzalishwa kutokana na tafiti mbalimbali zilizofanywa kwa hekta 47,862 zikilimwa vizuri zinaweza kupatikana tani 119,655 ambayo ni ongezeko la asilimia 55.

Wangabo alisema kuwa nia ya kujikita katika kuzalisha alizeti kwa wingi ni kuzalisha mafuta ya alizeti kwa wingi, kutengeneza ajira na kuongeza viwanda ili kufikia nia ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa viwanda.

Alisema kwa mujibu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na uwekezaji Tanzania inatumia Shilingi bilioni 189.6 kila mwaka kununua mafuta ya kula nje ya nchi huku ikizalisha tani 91,000 ambayo ni sawa na asilimia 40 za mafuta hayo tofauti na makadirio ya tani 200,000 hadi 300,000 ya uhitaji wa bidhaa hiyo kwa mwaka kitu ambacho mkoa wa Rukwa umeiona fursa hiyo na hivyo umejipanga kujikita katika kilimo cha alizeti vizuri.

Mkuu huyo wa mkoa wa Rukwa alisema kuwa mkoa unatarajia kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Faida mali ambalo limefanikiwa kwa kiwango kikubwa kukuza zao la alizeti katika Mkoa wa Singida ili kuhamishia ujuzi huo katika Mkoa wa Rukwa.

Kwa upande wake balozi wa Jamhuri ya Ireland Paul Sherlock alisema kuwa amefurahishwa sana na mikakati hiyo ya mkoa wa Rukwa kwa kuona umuhimu wa kutafuta zao mbadala la biashara katika Mkoa wa Rukwa ikiwa ni pamoja na kuinua kilimo cha mkoa na kuinua kipato cha wakulima wadogo na hatimae kuwatafutia namna ya kuongeza viwanda vidogo na kuongeza ajira.

Alisema kuwa serikali ya nchi yake ipo tayari kutoa msaada wa hali na mali ili mkoa huo uweze kufikia malengo hayo kitu cha muhimu ni kuendelea na ushirikiano ili mikakati hiyo iweze kufanikiwa na kuleta tija kwa wakulima pamoja na serikali kwa ujumla.
 
Mwisho

Saturday 2 June 2018

Wanafunzi Nkasi sasa wapeana mimba

Na Gurian Adolf
Nkasi

IMEELEZWA vitendo vya kupeana mimba baina ya wanafunzi kwa wanafunzi vimeshika kasi katika wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa hali inayochangia kukwamisha jitihada za kukabiliana na mimba za utotoni wilayani humo.

Hayo yalielezwa jana na hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya hiyo Ramadhan Rugemalila wakati akitoa mada katika mkutano wa siku moja wa kupitia utekelezaji wa mpango kazi wa kuanzia mradi wa kuzuia mimba za utotoni unaofadhiriwa na shirika la kimataifa la Plan International  wa mwezi Januari hadi Juni na kuandaa mpango kazi wa mwezi Julai hadi mwezi Desemba mwaka huu.

Alisema kuwa kutokana na elimu inayotolewa kwa wananchi pamoja na adhabu kali za kisheria zinazotolewa hivi sasa vitendo vya watu wazima kuwapa mimba watoto wa kike vimepungua badala yake vimeibuka vitendo vya kupeana mimba wanafunzi kwa wananfunzi.

Rugemalila alisema kuwa hivi sasa mahakani zimejaa kesi za mimba kwa wanafunzi ambazo idadi kubwa ni wanafunzi wamekuwa wakipeana mimba hali ambayo inalazimu sasa mashirika ya kutoa elimu yaelekeze nguvu mashuleni huenda mashirika yaliyopo yalijikita kutoa elimu kwa watu wazima na wakawasahau wanafunzi.

Hakimu huyo mfawidhi alisema kuwa pia changamoto nyingine iliyopo ni sheria inayotoa adhabu kwa mwanafunzi anayempa mwanafunzi wa kike ujauzito kwani haitoi adhabu kali  isipokuwa inaelekeza kupelekwa katika magereza maalumu ya watoto ambako anakwenda kuendelea na masomo hivyo kitendo hicho kinasababisha baadhi yao kuto ogopa wakati mwanafunzi wa kike anapoteza fursa ya masomo.

Alisema kuwa pia ipo chanagamoto kwa baadhi ya kesi kukosa ushahidi wa kutosha kuwatia hatiani watuhumiwa ama baadhi ya mashahidi wakiwemo waadhirika wa mimba za utotoni kutofika mahakamani hali inayosababisha baadhi ya kesi kufutwa na watuhumiwa kuachiwa huru kitendo kinachosababisha wananchi kuvitupia lawama vyombo vya sharia kuwa havitendi haki.

Kwaupande wake mratibu wa mradi wa kuzuia mimba za utotoni wilayani Nkasi Frank Nestory alisema kuwa tangu mradi huo ulipoanza kutekeleza wilayani humo kumekuwa na madiliko chanya kitendo kinachoonesha jamii hiyo ilikosa elimu.

Alisema kuwa wapo baadhi ya wazazi walikuwa hawatambui kuwa kumuozesha mtoto  wake  mdogo wa kike ni kosa kisheria kwani mlolo huyo ni wakwake kwahiyo hakuna mtu anayeweza kumzuia kufanya hivyo mradi aamue yeye mwenye mtoto.

Nestory alisema kuwa ni mtumaini yake mpaka mradi huo utakapokuwa umefikia mwisho suala la mimba kwa watoto wilayani Nkasi litabaki historia kutokana na elimu wanayoitoa sambamba na nmwitikio wa wananchi katika kuunga mkono jitihada za kutokomeza ndoa za utotoni pamoja na mimba.

Mwisho