Monday 4 August 2014

walimu Rukwawapewa siku 14 waanze kutoa chakula shuleni

Na Gurian Adolf
Sumbawanga.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa ametoa siku 14 kwa watendaji wa vijiji kuhakikisha shule zilizopo katika vijiji yao zinatoa chakula kwa wanafunzi atakaye shindwa awekwe ndani kwa siku saba.

Agizo hilo lilitolewa jana na kaimu mkurugenzi Chrispin Mlwanda katika mkutano wa hadhara wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Kaengesa wilayani humo kwa lengo la kukaugua utekelezaji wa sera ya matokeo makubwa sasa (BRN).

Alisema kuwa baadhi ya watendaji wa vijiji wamekuwa ni kikwazo cha utekelezaji mambo mbalimbali ya maendeleo ikiwemo elimu.

Alisema kutokana na hali hiyo sasa ni wakati wa kuanza kuwawajibisha watendaji wa vijiji kwani kulegalega kwao kumekuwa ni kikwazo cha maendeleo.

"natoa siku 14 kwa watendaji wa vijiji wote kuhakikisha wanafunzi wa shule za msingi wanapata chakula, kwa mtendaji atakayeshindwa akamatwe na kuwekwa ndani kwa siku saba ili iwe fundisho"...alisema

kaimu huyo mkurugenzi alisema kuwa changamoto nyingi katika shule za msingi katika halmashauri hiyo zinaweza kutatuliwa lakini tatizo ni viongozi wa serikali wamekuwa hawawajibiki kutekeleza majukumu yao.

Kwaupande wake Afisa elimu shule za sekondari wilayani humo Emiliana Fungo alisema kuwa wazazi wanawajibu wa kuhakikisha wanatatua changamoto kaika shule ambazo wanasoma watoto wao ili waweze kupata matokeo bora.

Mwisho.