Sunday 7 January 2018

Cwt yampongeza rais Magufuli

Na Gurian Adolf
Kalambo

CHAMA cha Walimu CWT wilayani Kalambo mkoani Rukwa kimepongeza hatau ya rais John Magufuli kutangaza kutoa fedha kiasi cha bilioni 200 kwaajili ya kulipa madeni mbalimbali ya ndani yakiwemo ya walimu.

Pongezi hizo zilitolewa jana na katibu wa chama hicho Peter Simwanza alipokuwa akizungumza na gazeti hili lililotaka kujua wanachama wa chama hicho wamepokeaje ahadi hiyo ya rais.

Alisema kuwa hatua ya serikali kuamua kulipa madeni yaliyokwisha hakikiwa ikiwemo ya walimu italeta moyo wakuongeza juhudi katika utendaji kazi kwani kilikuwa ni kilio cha muda mrefu cha Walimu wa wilaya hiyo. 

Simwanza alisema kuwa tangu walimu walipomsikia raisi akitangaza ahadi hiyo kupitia vyombo vya habari wamekuwa na morali wa kufanya kazi kwakua wanaamini serikali itawalipa fedha hizo ambazo walikuwa wakizisubiri kwamuda mrefu.

Aidha katibu huyo wa CWT wilaya ya Kalambo aliwataka walimu kuendelea kufanya kazi kwa weledi ili kuongeza ufaulu na kuleta tija katika wilaya ya Kalambo na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla. 

 Mwaka jana  walimu nchini walitishia kuitisha kugoma kwa kile walichodai kuwa ni njia ya kuishinikiza serikali ili ilipe madeni yao kwani yamekuwa ni ya muda mrefu na yanasababisha walimu kuvunjika moyo katika kufanya kazi.

Hata hivyo walimu wilayani humo walitumia fursa hiyo kumuomba raisi John Magufuli afanye uamuzi wa kuwapandisha madaraja watumishi wa umma sambamba na kuwaongeza mishahara. 

Mwisho
 

No comments:

Post a Comment