Friday 30 June 2017
Thursday 29 June 2017
Marufuku kuchungia mifugo ndani ya hifadhi
Na Gurian Adolf
Katavi
Wizara ya Maliasili na Utalii imewaonya wafugaji hapa nchini kuacha tabia yakwenda kuchungia mifugo yao katika hifadhi za taifa na mapori ya akiba kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria na watambue kuwa hawataepuka mkono wa sheria iwapo watabainika wakiingiza mifugo yao humo.
Amewataka Wahifadhi wote kushirikiana na Mamlaka za Mikoa na Wilaya ili kuweza kukabiliana na tatizo la uvamizi wa maeneo ya hifadhi yanayofanywa kwa ajili ya shughuli za kibinadamu hususani uvamizi wa mifugo kwenye maeneo ya hifadhi .
Onyo hilo limetolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Generali Gaudence Milanzi alipokua akifunga mafunzo ya uongozi kwa maafisa Wanyama pori yenye lengo la kuwafanya wafanye kazi kutoka mfumo wa kiraia na kuwa mfumo wa kijeshi yaani Jeshi usu, yaliofanyika katika kituo cha mafunzo Mlele Mkoani Katavi .
Alisema kuwa hivi sasa uhifadhi unakabiliwa na tatizo la uvamizi unaonywa kwa shughuli za kibinadamu hususani uchungaji wa mifugo kwenye maeneo ya hifadhi baadhi ya maeneo hata binadamu kujenga na kuishi ndani ya maeneo ya uhifadhi kitendo ambacho ni kosa kisheria na kamwe hakita vumiliwa.
Meja Jenerali huyo alisema kuwa Wizara inatoa wito kwa Wahifadhi wote na kwa kushirikiana na Mamlaka za Mikoa na Wilaya husika kulimaliza kabisa tatizo hilo.
Aliwaagiza wahitimu wa mafunzo hayo washirikiane na wakuu wao kupanga mipango itakayo washirikisha wananchi katika kumaliza tatizo la uvamizi wa mifugo kwenye maeneo ya hifadhi na migogoro ya mipaka kati ya maeneo ya hifadhi na Vijiji kwani nalo zimekuwa ni changamoto kubwa.
Milanzi aliwaomba wananchi wote kuendelea kuheshimu sheria za nchi na kuacha kufanya shughuli za kibinadamu kwenye maeneo ya hifadhi kwani watambue kuwa kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Alisema kwa kipindi cha miaka ya hivi karibuni wizara ya Maliasili na Utalii imeshuhudia baadhi ya matukio ya mmomonyoko mkubwa wa maadili hasa kwa watumishi wa kada ya Askari wao wenyewe kujihusisha na vitendo vya ujangili na mengine mambo yasiyo faa katika utumishi wa umma.
Alieleza kuwa mafunzo waliopatiwa wahitimu hao anaamini kuwa kwa kuwa wao ndio viongozi wakuu wa askari watakwenda kusaidia kurudisha nidhamu kwa askari na watumishi wa chini yao kwa kuwaelekeza mambo mazuri ya kujenga wanayotakiwa kuyafanya ili kuhakikisha kunakuwepo na uhifadhi endelevu wa maliasili za nchi.
Kaimu kwaupande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Wanyama pori Tanzania Martin Loibooki alisema ulinzi wa rasilimali za Wanyama pori umeendelea kuimarika ndani na nje ya mapori ya akiba na tengefu sambamba na kuimarisha ukaguzi wa nyara katika maeneo ya mipakani kwa kushirikiana na wadau wengine.
Chini ya uongozi wa Wizara TAWA imeshirikiana na idara ya Wanyama pori ,TANAPA na mamlaka ya hifadhi Ngorongoro NCCA katika kutekeleza kazi mbalimbali.
Mafunzo hayo ya wiki sita yaliwashirikisha wahitimu 97 wakiwemo Maafisa wandamizi 20 na maafisa wa kati 77 wa kutoka Mamlaka ya Wanyama pori Tanzania TAWA.
Mwisho
Amuua rafiki yake akimdai mbao mbili
Na Gurian Adolf
Sumbawanga
MTU mmoja anayefahamika kwa jina la Fokas Pera(48) mkazi wa kitongoji cha Ilemba B, kata ya Nankanga tarafa ya Laela wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa ameuawa na rafiki yake kwa kumkata na kitu chenye ncha kali kinachodhaniwa kuwa ni panga kichwani kwa madai kuwa alimdhurumu mbao mbili.
Tukio la mauaji hayo kilitokea Juni 28 majira ya saa 3:00 asubuhi katika kitongoji hicho baada ya kumhadaa marehemu na kwenda naye porini ambako yalifanyika mauaji hayo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Rukwa George Kyando alisema kuwa marehemu alikuwa akidaiwa mbao mbili na rafiki yake aitwaye Paul Kayuni (50) mkazi wa kitongoji hicho ambazo anadaiwa alimpa rafiki yake huyo.
Baada ya kumdai kwa muda mrefu Pera alikuwa akisumbua kulipa hali iliyomkasilisha mtuhumiwa na kupanga kumpiga kutokana na usumbufu aliokuwa akiufanya.
Siku hiyo mtuhumiwa alimtumia rafiki zake marehemu kuwa waende porini wakamuuzie mbao naye alikubali na alipofika kule polini alimkuta mtu anayemdai ambapo alianza kumshushia kipigo.
Akiwa anampiga marehemu naye aliamua aanze kupigana hali ambayo ilimfanya mtuhumiwa kuchukua panga aliyokuwa ameficha porini na kumkata nayo kichwani ambapo alimsababishia jeraha kubwa lililoanza kuvuja damu nyingi.
Baada ya kuvuja damu nyingi katika jeraha hilo alianguka chini na kupoteza fahamu ambapo walimchukua na kumkimbiza katika zahanati ya kijiji kwaajili ya matibabu.
Alipofikishwa katika zahanati ya kijiji hicho mganga wa zamu alipompokea na kumfanyia uchunguzi aliwaambia amekwisha fariki kutokana na kuvuja damu nyingi kutokana na jeraha alilopata.
Polisi inamshikilia mtuhumiwa wa mauaji hayo na atafikishwa mahakamani pindi upelelezi wa awali utakapokuwa umekamilika.
Mwisho
Wanawake washauriwa kupata tiba za kitaalamu
Na Gurian Adolf
Sumbawanga.
Wanaume mkoani Rukwa wametakiwa kuweka kando mifumo kandamizi ya dhidi ya wanawake hivyo waruhusu kwa wake zao wenye kusumbuliwa na maradhi mbalimbali kujitokeza na kupata tiba hospitalini pindi madaktari bingwa watakapowasili mkoani hapa.
Mkazi wa kitongoji cha Jangwani, Pendoeva Kapola alisema hayo jana wakati akizungumza na mwandishi wa gazeti hili, kuhusu ujio wa madaktari bingwa wa magonjwa mbalimbali wanaoletwa na mfuko wa bima ya afya (NHIF).
Mkazi wa kitongoji cha Jangwani, Pendoeva Kapola alisema hayo jana wakati akizungumza na mwandishi wa gazeti hili, kuhusu ujio wa madaktari bingwa wa magonjwa mbalimbali wanaoletwa na mfuko wa bima ya afya (NHIF).
Madaktari hao wanaotibu maradhi mbalimbali wanatarajiwa kuwasili na kuanza kutoa tiba mapema juma lijalo katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Rukwa iliyopo mjini Sumbawanga.
Kapola alisema kuwa wapo baadhi ya wanaume wamekuwa wakiendekeza mifumo kandamizi dhidi ya wanawake, kiasi cha kushindwa kuwapata hata ruhusu ya kutoka nyumbani kwao ili waende hospitali kupata tiba hivyo kutibiwa kienyeji hali ambayo imesababisha baadhi ya wanawake kutopata ufumbuzi wa kudumu wa maradhi yao na wakati mwingine kupoteza maisha.
Kapola alisema kuwa wapo baadhi ya wanaume wamekuwa wakiendekeza mifumo kandamizi dhidi ya wanawake, kiasi cha kushindwa kuwapata hata ruhusu ya kutoka nyumbani kwao ili waende hospitali kupata tiba hivyo kutibiwa kienyeji hali ambayo imesababisha baadhi ya wanawake kutopata ufumbuzi wa kudumu wa maradhi yao na wakati mwingine kupoteza maisha.
Alisema mifumo dume na mingine iliyotawala katika jamii inapaswa kuachwa mara moja ili wanawake waweze kujitokeza hospitali na kutumia fursa ya uwepo wa madaktari bingwa kupata tiba ya uhakika ya magonjwa sugu na mengineyo yanayowasumbua.
Aidha, Meneja wa NHIF, Simon Mbaga alisema ujio wa madaktari bingwa ni sehemu ya utekelezaji mpango wa mfuko huo kuyafikia maeneo ya pembezoni ili wagonjwa waweze kupata tiba kutoka kwa wataalamu hao wa afya pasipo kutembea umbali mrefu na kutumia gharama kubwa kuwafuata.
Mbaga alisema kwamba madaktari bingwa watakaokuwepo ni wale wa magonjwa sugu ya ndani pamoja na magonjwa ya moyo, watoto, mfumo wa mkojo, pua, koo, na masikio sambamba na madaktari bingwa wa afya ya uzazi na magonjwa ya wakina mama.
Alisema kwamba wanachama wa Mfuko wa bima ya afya watatibiwa kwa kutumia kadi zao, lakini wale wasio na kadi watalazimika kulipia gharama za kawaida za hospitali.
Mwisho.
Wednesday 28 June 2017
Amuua mdogo wake kwa kumpiga mpini wa jembe
Na Gurian Adolf
Sumbawanga
Jeshi la Polisi mkoa wa Rukwa, linamshikilia mkazi wa kijiji cha Kilida kona wilayani Sumbawanga, Japhet Kigula kwa tuhuma ya kumuua mdogo wake kwa kumpiga mpini wa jembe kichwani wakati
akimuadhibu.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa, George Kyando amethibitisha kutokea kwa tukio hilo juni 26 nyakati za saa 12 jioni katika kijiji hicho, ambapo aliyeuawa ni Makumbi Kigula.
Taarifa zinaeleza kuwa siku mbili kabla tukio mtuhumiwa ambaye alikuwa amesafiri kutoka mkoani Mwanza alimwita mdogo wake nyumbani kwake ili waweze kufanya mazungumzo ambayo hayakuwekwa bayana lakini kijana huyo hakuweza kwenda hali ambayo ilimkera Japhet.
Inasemekana kwamba juzi nyakati za jioni saa 11 kijana huyo alikwenda nyumbani kwa kaka yake na kuanza kuongea nae ambapo mtuhumiwa
alionekana kutofurahisha na kitendo cha mdogo wake kuchelewa kuitika wito wake.
Kutokana na hali hiyo, Japhet akisaidia na mmoja wa watumishi wake wa ndani walimkamata kijana huyo na kumfunga kamba mikono na miguu kisha
kaka mtu kuanza kumuadhibu kwa kutumia mpini wa jembe ambao alimpiga nao sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo kichwani huku damu
zikimtoka puani ndipo majirani walipoingilia kati.
Baada ya majirani kuingilia kati walimkimbiza katika zahanati ya kijiji iliyopo kijijini hapo lakini ilipofika jana mchana alifariki dunia.
Polisi walifika kijijini hapo na kumkamata mtuhumiwa wa mauaji hayo ambaye bado anashikiliwa kwa mahojiano kabla ya kufikishwa mahakamani ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.
Katika hatua nyingine, Polisi inamshikilia dereva Josephat Salya mkazi wa Sumbawanga mjini kwa tuhuma za kumgonga kwa gari mtoto Eliud
Steven(5) mkazi wa kijiji cha Kipundu Kala tarafa ya Namanyere wilayani Nkasi.
Tukio la kumgonga mtoto huyo lilitokea juni 27 saa 10:05 katika kijiji hicho wakati mtoto huyo akiwa anatembea barabarani.
Kamanda wa polisi mkoani Rukwa George Kyando alisema kuwa dereva huyo alikuwa akiendesha gari lenye namba za usajili T 790 DEM T aina ya Tata Truck mali ya Assif Ashraf ambapo lilimgonga mtoto huyo na kufa papo hapo.
Alisema kuwa chanzo cha ajalia ni uzembe wa dereva kushindwa kujali watumiaji wengine wa barabara na hivyo kukosa umakini awapo
barabarani.
Mwisho.
akimuadhibu.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa, George Kyando amethibitisha kutokea kwa tukio hilo juni 26 nyakati za saa 12 jioni katika kijiji hicho, ambapo aliyeuawa ni Makumbi Kigula.
Taarifa zinaeleza kuwa siku mbili kabla tukio mtuhumiwa ambaye alikuwa amesafiri kutoka mkoani Mwanza alimwita mdogo wake nyumbani kwake ili waweze kufanya mazungumzo ambayo hayakuwekwa bayana lakini kijana huyo hakuweza kwenda hali ambayo ilimkera Japhet.
Inasemekana kwamba juzi nyakati za jioni saa 11 kijana huyo alikwenda nyumbani kwa kaka yake na kuanza kuongea nae ambapo mtuhumiwa
alionekana kutofurahisha na kitendo cha mdogo wake kuchelewa kuitika wito wake.
Kutokana na hali hiyo, Japhet akisaidia na mmoja wa watumishi wake wa ndani walimkamata kijana huyo na kumfunga kamba mikono na miguu kisha
kaka mtu kuanza kumuadhibu kwa kutumia mpini wa jembe ambao alimpiga nao sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo kichwani huku damu
zikimtoka puani ndipo majirani walipoingilia kati.
Baada ya majirani kuingilia kati walimkimbiza katika zahanati ya kijiji iliyopo kijijini hapo lakini ilipofika jana mchana alifariki dunia.
Polisi walifika kijijini hapo na kumkamata mtuhumiwa wa mauaji hayo ambaye bado anashikiliwa kwa mahojiano kabla ya kufikishwa mahakamani ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.
Katika hatua nyingine, Polisi inamshikilia dereva Josephat Salya mkazi wa Sumbawanga mjini kwa tuhuma za kumgonga kwa gari mtoto Eliud
Steven(5) mkazi wa kijiji cha Kipundu Kala tarafa ya Namanyere wilayani Nkasi.
Tukio la kumgonga mtoto huyo lilitokea juni 27 saa 10:05 katika kijiji hicho wakati mtoto huyo akiwa anatembea barabarani.
Kamanda wa polisi mkoani Rukwa George Kyando alisema kuwa dereva huyo alikuwa akiendesha gari lenye namba za usajili T 790 DEM T aina ya Tata Truck mali ya Assif Ashraf ambapo lilimgonga mtoto huyo na kufa papo hapo.
Alisema kuwa chanzo cha ajalia ni uzembe wa dereva kushindwa kujali watumiaji wengine wa barabara na hivyo kukosa umakini awapo
barabarani.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)