Na Gurian Adolf
Nkasi
SERIKALI
mkuu mkoani Rukwa imepiga marufuku kuutumia mwalo uliopo katika
Kijiji cha Kirando ziwa Tanganyika kwaajili ya kupakia na kushia mizigo
kwani mwalo huo umetengwa kwaajili ya shughuli za kuuzia samaki.
Mkuu
wa mkoa huo Joachim Wangabo alisema hayo jana wakati akiwa katika ziara
ya kikai wilayani Nkasi na kukuta katika mwalo wa Kirando unatumika
kama bandari ambapo malori yalikuwa yakipakua na kupakia mizigo kwa
lengo la kusafisirisha kuipeleka kwenye visiwa vilivyopo ziwa
Tanganyika.
Alisema
kuwa wananchi wasipotoshe lengo la kutebnwa kwa mwalo huo ambayo ni
kwaajili ya kuuza na kununua samaki wavuliwao kwenye ziwa Tanganyika na
si kwaajili ya magari kupakilia mizigo.
,“Lengo
la Mwalo huu ni kuuzia samaki na dagaa lakini naona mizigo hii,
imegeuzwa kuwa bandari, narudia nimarufuku kupakilia mizigo katika mwalo
huu kwani hapa ni sehemu ya kuuzia mazao yatokanayo na ziwa na si
vinginevyo" alisema
Mkuu huyo wa mkoa alisema
kuwa sehemu iliyotengwa ikitumika kama bandari haiko vizuri basi waone
namna ya kuboresha ili sehemu hiyo ilirudi kama ilivyokuwa na sio
kuikimbia na kuiacha kama ilivyo jwani kukimbia tatizo sio suluhisho
bali kupambana na changamoto zilizopo na kuboresha.
Awali
kabla ya Kukaribishwa Mkuu wa Mkoa, Mbunge wa Nkasi Kaskazini Ali Kessy
alikemea vitendo vya wananchi wa Kirando kutumia mwalo huo kama bandari
jambo ambalo ni kinyume na sheria na kuwataka kuacha tabia hiyo mara
moja.
“Nawaomba
ndugu zangu kuanzia sasa hii sio bandari na haipo chini ya TPA,
bandari ni ile ya zamani na iendelee kutumika ile ile na hapa tuwaachie
wavuvi"alisema
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Said Mtanda aliwaasa wananchi
wanaotumia vyombo usafiri ziwani kuzingatia kuvaa maboya na kuonya
kutozidisha mizigo na abiria na kuwasisitiza wasafiri wa majini kuwa
watumiaji wawe wantoa taarifa endapo wataona taratibu zinakiukwa kwakuwa
wasafirishaji hao huangalia faida kuliko usalama wa maisha ya abiria
wao.
Mwisho
No comments:
Post a Comment