Tuesday 9 January 2018

Rc apiga marufuku kupakia mizigo katika mwalo wa Kirando

Na Gurian Adolf
Nkasi
SERIKALI mkuu mkoani  Rukwa imepiga marufuku  kuutumia mwalo uliopo katika  Kijiji cha Kirando ziwa Tanganyika kwaajili ya kupakia na kushia mizigo kwani mwalo huo umetengwa kwaajili ya shughuli za kuuzia samaki.

Mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo alisema hayo jana wakati akiwa katika ziara ya kikai wilayani Nkasi na kukuta katika mwalo wa Kirando unatumika kama bandari ambapo malori yalikuwa yakipakua na kupakia mizigo kwa lengo la kusafisirisha  kuipeleka kwenye visiwa vilivyopo ziwa Tanganyika.

Alisema kuwa wananchi wasipotoshe lengo la kutebnwa kwa  mwalo huo ambayo ni kwaajili ya kuuza na kununua samaki wavuliwao kwenye ziwa Tanganyika na si  kwaajili ya magari kupakilia mizigo.

,“Lengo la Mwalo huu ni kuuzia samaki na dagaa lakini naona mizigo hii, imegeuzwa kuwa bandari, narudia nimarufuku kupakilia mizigo katika mwalo huu kwani hapa ni  sehemu ya kuuzia mazao yatokanayo na ziwa na si vinginevyo" alisema

Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa sehemu iliyotengwa ikitumika kama bandari haiko vizuri basi waone namna ya kuboresha ili sehemu hiyo ilirudi kama ilivyokuwa na sio kuikimbia na kuiacha kama ilivyo jwani kukimbia tatizo sio suluhisho bali kupambana na changamoto zilizopo na kuboresha.

Awali kabla ya Kukaribishwa Mkuu wa Mkoa, Mbunge wa Nkasi Kaskazini Ali Kessy alikemea vitendo vya wananchi wa Kirando kutumia mwalo huo kama bandari jambo ambalo ni kinyume na sheria na kuwataka kuacha tabia hiyo mara moja.

“Nawaomba ndugu zangu kuanzia sasa hii  sio bandari na haipo chini ya TPA, bandari ni ile ya zamani na iendelee kutumika ile ile na hapa tuwaachie wavuvi"alisema

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Said Mtanda aliwaasa wananchi wanaotumia vyombo usafiri ziwani kuzingatia kuvaa maboya na kuonya kutozidisha mizigo na abiria na kuwasisitiza wasafiri wa majini kuwa watumiaji wawe wantoa taarifa endapo wataona taratibu zinakiukwa kwakuwa wasafirishaji hao huangalia faida kuliko usalama wa maisha ya abiria wao. 

Mwisho

No comments:

Post a Comment