Monday 28 May 2018

CCM yawaonya wanachama wake

Na Gurian Adolf
Katavi

CHAMA cha mapinduzi CCM mkoani Katavi kimewaonya baadhi ya wanachama wake waache mara moja tabia ya kuwa andaa wanachama wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 kabla ya muda kwani kitendo hicho kinasababisha uhasama baina ya wanachama na mipasuko ndani ya chama hicho.

Onyo  hilo lilitolewa hivi karibuni na katibu wa chama hicho mkoa wa Katavi Kajoro  Vyahoroka wakati  alipokuwa akiwatubia  wananchi wa   Kata  ya  Majalila katika mkutano uliondaliwa na  Mbunge wa  Jimbo la  Mpanda   Vijijini  Moshi  Kakoso uliofanyika  kwenye   uwanja wa  shule ya  Msingi  Majalila wakati  Mbunge  huyo  alipokuwa  akikabidhi  kompiyuta 25   zenye  thamani ya  milioni 50 kwa  ajiri ya  shule  sita za  Sekondari  za  jimbo hilo.

Alisema kuwa wapo baadhi ya  viongozi wa  chama   hicho wa  ngazi mbalimbali  wameanza kuwapigia kampeni viongozi  wanao wataka wao  wakati ni kinyume  na taratibu na  watakao  bainika  hawata  sita  kuwachulia  hatua  kali za  kinidhamu. 

 Alisisitiza kuwa  ni  vema  viongozi  walipo  madarakani  kwa  sasa  waachwe  watimize  wajibu wao  ili  wakati ukifika  waje waulizwe  waliokuwa  wameyahidi kwa  wananchi  wao ndipo wanachama waone kama wanastahili kuchaguliwa tena ama laa.
 Alieleza  kuwa  kitendo  cha viongozi kuanza kuwaandaa  viongozi  wanao wataka wao kinawafanya viongozi walipo  madarakani  waanze kuvunjika  moyo  katika  utekelezaji wa majukumu  yao na kujenga chuki kwa wananchama wanaoandaliwa hali inayosababisha makundi ndani ya chama hicho.
 Kwenye  mkutano huo  Katibu wa  CCM  wa  Mkoa wa  Katavi  alipokea  kadi    150 kutoka   kwa  wanachama wa  vyama  mbalimbali vya upinzani na  kuwakabidhi kadi za   CCM  ambapo  baadhi yao walimwakikishia  Katibu  huyo kuwa  wao na  wake  zao  kuanzia  siku  hiyo  wamehamia rasmi  CCM .
Mmoja  wa  wanachama  hao wapya    Juma    Ramadhan alisema  wameamua  kurudi    Ccm kutokana  na  kasi ya  maendeleo  ilipo  sasa   inayofanywa na  Serikali ya  awamu ya  pili inayoongozwa na  Rais Dkt John Magufuli.
Naye   Mbunge wa  Jimbo la   Mpanda   Vjijini   Moshi   Kakoso   alisema  kuwa  Jimbo lake  na   Wilaya    ya  Tanganyika  wamepata  maendeleo kwa haraka  kutokana  na  jinsi  viongozi  wanavyofanya  kazi kwa  ushirikiano  bila  kuwepo na  migogoro yoyote.
 Alisema  anamwombea heri    Mkuu wa  Wilaya  hiyo  Salehe  Mhando  asihamishwe  kwenye    Wilaya  hiyo kutokana  na  utendaji kazi wake  kwani   amekuwa akifanya kazi   mpaka  anasahau  kujenga  mwili  wake   kwa  kushindwa  hata  kula  kwa  ajiri ya majukumu  ya  kuwatumika wananchi .
Kwa upande wake mkurugenza wa  Halmashauri  hiyo  Romuli   Rojas  alisema  kuwa  Wilaya  hiyo imepiga  hatua  kubwa ya  maendeleo  kwenye  sekta  mbalimbali    kama  vile   afya ,barabara  ,mawasiliano elimu   maj, na  kilimo.


Mwisho

Nkasi kinara kwa ujauzito

Na Gurian Adolf
Nkasi
HALMASHAURI ya wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa imetajwa kuwa ndiyo inayo ongoza kwa wanafunzi wanafunzi kupata ujauzito mkoani Rukwa na katika kipindi cha miezi tisa jumla ya wanafunzi 74 wamekatiza masomo kutokana na kupata ujauzito.
Akizungumza jana  kwenye kikao cha baraza la madiwani afisa serikali za mitaa mkoani humo Albinus Mgonya alisema kuwa kwa kipindi cha kuanzia mwezi Julai mwaka jana hadi april 30 mwaka huu  wanafunzi 36 wanafunzi wa shule za msingi na wanafunzi38 wa sekondari walipata ujauzito.
Alisema kuwa kulingana na takwimu hizo inamaana kuwa wanafunzi wanaopata ujauzito ni sawa na kuwa kila mwezi wanafunzi  wanne wa shule za msingi  wanapata mimba sambamba na wanne wa sekondari wanapata ujauzito.
Mgonya alisema kuwa kutokana na hali hiyo ameiagiza halmashauri ya wilaya Nkasi kuandaa taarifa itakayoainisha idadi ya Watoto wenye mimba  mahali walipo,wazazi  wao ikiwa ni pamoja na viongozi wa maeneo yao hasa Watendaji wao wa vijiji na kata ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Katika hatua nyingine afisa huyo wa serikali za mitaa ameipongeza halmashauri ya wilaya Nkasi kwa kufanya vizuri katika makusanyo ya ndani ambapo hadi sasa makusanyo ni asilimia 76 na kuwa wilaya hiyo inaongoza kimkoa katika suala zima la makusanyo ikiwa ni pamoja na wilaya kuendelea kupata hati safi.
Kwa upande wake Katibu tawala wa wilaya hiyo Festo Chonya ameitaka halmashauri hiyo kutowahamisha watendaji wabovu bali washughulikiwe pale pale walipo ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi kwani serikali ya sasa haiwezi kuwahamisha watendaji wabovu kutoka eneo moja kwenda jingine.
Alisema kuwa katika mjadala ulioendelea katika kikao hicho madiwani walisema  kuwa yupo afisa mtendaji mmoja wa kijiji ambaye ameonyesha uwezo mdogo wa kiutendaji  na kuiomba halmashauri  imuhamishe kutoka katika kijiji alipo na  kwenda eneo jingine.
Chonya alisema kuwa  serikali ya awamu ya tano haimuhamishi mtumishi ambaye ameshindwa katika eneo moja  na kwenda eneo jingine na kuwa mawazo hayo ya madiwani si sahihi bali kama mtendaji huyo ameshindwa kuwajibika waanze mchakato mwa kumfukuza kazi na aajiriwe mwingine mwenye uwezo wa kazi.
Naye mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Zeno Mwanakulya aliwataka watendaji wa halmashauri kuyasimamia yale yote yaliyoagizwa katika kikao hicho ,huku akisisitiza suala la uwajibikaji ili kuweza kufikia malengo waliyojiwekea.
Kaimu mkurugenzi  wa halmahsauri ya wilaya hiyo  Missana Kwangula alisema kuwa halmashauri ya wilaya inafanya kazi vizuri na ndiyo maana kila mwaka imekua ikipata hati safi hasa katika eneo la makusanyo.
Mwisho

Friday 25 May 2018

kipindu pindu chaibuka upya

Na Gurian Adolf
Sumbawanga

UGONJWA wa kipindu pindu umeibuka tena katika wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa na katika kipindi kifupi cha siku kumi umesababisha vifo vya watu saba huku jumla ya watu 166 wakiwa wamekwisha ugua ugonjwa huo katika kipindi hicho.
Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga Dkt Halfan Haule alitoa taarifa hiyo jana katika kikao cha kamati ya afya ya mkoa huo ambayo ilikutana kwa lengo la kuweka mikakati ya kukabiliana na magonjwa ya Ebola pamoja na kipindu pindu mkoani humo.

Alisema kuwa awali ugonjwa huo ulikuwepo katika wilaya hiyo kuanzia mwezi Novemba mwaka jana na jitihata za kuumaliza zilifanyia na ilipofika mwezi Machi mwaka huu ukawa umekwisha na katika kipindi hicho cha miezi mitano uliua watu saba.

Alisema kuwa hivi sasa ugonjwa huo umeibuka upya katika vijiji vya Maenje,Milepa,Kpaenta, Mkusi,Tunko na Laela ambapo uliripotiwa Mei 12 na tayari watu saba walikwisha fariki dunia katika kipindi kifupi cha siku kumina mpaka hivi sasa bado kuna wagonjwa 44 wakiwa wanatibiwa kipindu pindu.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa sababu kubwa ya kuibuka upya kwa ugonjwa huo ni kutokana na kuwa hivi sasa wakulima wa mpunga wanavuna mbugani na hawana utamaduni wa kutumia maji yaliyochemshwa hali ambayo imesababisha kuibuka upya ugonjwa huo na kusababisha vifo hivyo.

Dkt Haule alisema kuwa hivi sasa wilaya hiyo inakabiliwa na ukosefu wa dawa za kutibu maji(water guard) ambapo alitumia fursa hiyo kuwaomba wadau mbalimbali kusaidia upatikanaji wa dawa hizo ili zigawiwe kwa wananchi ambapo zitasaidia kupunguza kasi ya ugonjwa huo.

Katika kikao hicho mganga mkuu wa mkoa wa Rukwa Bonifas Kasululu alisema kuwa katika suala la ugonjwa wa Ebola tayari taratibu zote zimekwisha fuatwa ikiwa ni pamoja na kutenga maeneo ya kuwapatia matibabu wagonjwa watakao onesha dalili za ugonjwa huo na vifaa kwaajili ya wahudumu wa afya vipo licha ya kuwa bado hakujaripotiwa mgonjwa wa Ebola katika mkuoa huo.

Kwaupande wake mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo ambaye alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho aliagiza madaftari ya wakazi yaanze kutumika katika serikali za vijiji ilikuwatambua watu wanaoingia mkoani humo kwa lengo la kukabiliana na Ebola.

Pia Wangabo alisema kuwa ifike pahala ugonjwa wa kipindu pindu ukomeshwe kabisa katika mkoa huo kwani kunadalili kuwa ugonjwa huo umeanza kuzoeleka kwa wakazi wa mkoa huo kitu ambacho ni hatari.

Alisema kuwa changamoto kubwa kwa wananchi ni ukosefu wa elimu wa namna ya kujikinga na kipindu pindu ni lazima nguvu kubwa iwekezwe upande huo yeye hayupo tayari kuvumilia kuona watu wanakufa kwa ugonjwa huo.



Mwisho

viongozi wa dini waaswa

Na Gurian Adolf
Sumbawanga



VIONGOZI wa madhehebu ya Kikristu mkoani Rukwa wameshauriwa kuwaelekeza waumini wao namna bora ya kushiriki ibada ili kuepuka hofu ya kuambukizana magonjwa mbalimbali hususani nyakati hizi ambapo mkoa huo unakabiliwa na hofu ya magonjwa ya kipindupindu na Ebola.

Mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo alisema kuwa katika madhehebu ya Kikristo kunakipengele cha waumini kutakiana amani wakati wa ibada ambapo baadhi ya waumini hushikana mikono na wengine kukumbatiana hali ambayo ni hatari kwani kunawengine miili yao inakuwa inatoka jasho.

''mimi pia ni Mkristo huwa nikiwa katika ibada kunakipengele cha kutakiana amani ambapo huwa tunapeana mikono waumini,baadhi ya waumini mikono yao inakuwa na majimaji yaani jasho, na ugonjwa wa Ebola unaenezwa kwa maji maji ya mwili ikiwemo jasho hii inaweza kuwa hatari pia.

Alisema kuwa inafaa sasa viongozi wa dini waone namna bora ya kuwaelekeza waumini wao namna ya kushiriki ibada bila kuwa na hofu ya kuambukizana magonjwa mbalimbali hasa kipindu pindu kilichopo hivi sasa mkoani mkoani humo.

Akitoa taarifa katika hiivi karibuni katika kikao cha kamati ya afya ya mkoa huo ambayo ilikutana kwa lengo la kuweka mikakati ya kukabiliana na magonjwa ya Ebola pamoja na kipindu pindu mganga mkuu wa mkoa huo Bonifas Kasululu alisema kuwa pamoja na nchi jirani ya Kidemokrasia ya Kongo kukabiliwa na ugonjwa wa Ebola lakini katika mkoa wa Rukwa hakuna hofu yoyote.

Alisema kuwa mpaka hivi sasa kusiwepo hofu yoyote kwa wananchi na maisha yanapaswa kuendelea kama kawaida iwapo kutakuwa na tishio hilo idara ya afya iko makini na inafuatilia kwa umakini kila hatua na itatoa taarifa iwapo kuna mtu amebainika kuwa na dalili za ugonjwa huo.

Mwisho.

Tuesday 15 May 2018

waomba kupimwa tezi dume

Na Gurian Adolf
Sumbawa

WAKATI baadhi ya  wanaume jijini Dar es salaam wakipinga hoja ya mkuu wa mkoa huo Paul Makonda ya kupima saratani ya tezi dume nyumba kwa nyumba ,hali ni tofauti katika kijiji cha Zimba  halmashauri ya wilaya ya
Sumbawanga mkoani Rukwa ambapo baadhi ya wanaume wameiomba idara ya afya wilayani humo kuwapima
saratani ya tezi dume kutokana na hofu kuwa saratani hiyo imekuwa
ikisababisha vifo vya wanaume wengi.

Ombi hilo walilitoa jana kwa nyakati tofauti wakati wakizungumza na
waandishiwa habari katika siku ya afya kijijini hapo ambapo wilaya ya
Sumbawanga kwa kushirikiana na mradi wa mama na mwana iliandaa siku
maalumu kwaajili ya kupima afya kwa wakazi wa kijiji hicho.

Mmoja wa wanaume walio hudhuria siku hiyo Peter Katyega alisema kuwa
pamoja na vipimo mbalimbali vinavyotolewa lakini angependa pia kupima
saratani ya tezi dume kwani ni miongoni mwa magonjwa yanayosababisha
vifo vya wanaume wengi na hakuna mkakati wa kuwahimiza wanaume wa
wilaya hiyo kwaajili ya kupima ili kubaini kama wanaugua saratani ya
tezi dume.

Alisema kuwa mara kwa mara wanawake wamekuwa wakihimizwa kupimwa
saratani ya matiti na hivi sasa wilaya hiyo imezindua chanjo kwaajili
ya saratani ya mlango wa kizazi kwaajili ya watoto wa kike wenye umri
wa miaka 14 lakini hakuna jitihada za makusudi za kuhamasasha sambamba
na upimaji wa saratani ya tezi dume kwa wanaume.

Naye Majaliwa Ntobo mkazi wa kijiji hicho alisema kuwa inawezekana
baadhi ya vifo vya wanaume vinavyotokea katika kijiji hicho vingine
vinasababishwa na saratani ya tezi dume lakini kwakuwa hakuna
wataalamu wa kupima saratani hiyo na hawahamasishwi kufanyiwa
uchunguzi inaonekana kuwa wanakufa na magonjwa mengine,ambapo
wangeweza kutibiwa na wakaendelea kuishi.

Alisema kuwa imefika wakati sasa kwa watendaji wa idara ya afya
kubadili fikra kuacha kufikiria saratani ya matiti tu na badala yake
waanze kupima na saratani ya tezi dume ili kuokoa maisha ya wanaume
waliopo hatarini ambao wanasumbuliwa na ugonjwa huo.

Kwa upande wake Maria Kela mkazi wa kijiji cha Zimba alisema kuwa
pamoja na changamoto ndogo ndogo kama ukosefu wa mataktari bingwa
kwaajili ya kutibu  baadhi ya magonjwa lakini anaishukuru serikali
wilaya hiyo kwa kutenga walau siku mbili kwa mwaka kupima afya kwa
wakazi wa kijiji hicho kwani imesaidia watu wengi kujua matatizo ya
kiafya yanayo wasumbua.

Akizungumzia siku ya upimaji wa afya katika kijiji hicho mganga mkuu
wa halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga Fani Musa alisema kuwa
halmashauri hiyo imetenga siku mbili katika mwaka kwa kila kijiji cha
wilaya hiyo ambapo wakazi wa kijiji husika wanapata fursa ya kupima
magonjwa mbalimbali pamoja na uchangiaji damu.

Alisema kuwa lengo ni kusaidia wanachi kutambua mapema magonjwa
yanayowasumbua na kuanza taratibu za matibabu mapema kabla hali
haijafikia katika hatua kubwa ambapo alisema kuwa itakuwa ni rahisi
kutibiwa na kuishi maisha marefu kwakuwa mgonjwa anakuwa anafahamu
tatizo lake mapema.

Musa alisema kuwa yeye binafsi anatoa wito kwa wakazi wa vijiji vya
halmashauri hiyo kujitokeza kwa wingi ili kutumia nafasi hiyo kupima
afya zao bila kujali kuwa hakuna madaktari bingwa ama baadhi ya
magonjwa hayafanyiwi vipimo lakini ni afadhali wakapima hata yatakayo
wezekana kuliko kukata tamaa na kuendelea kuishi na magonjwa mengi
zaidi.

Mwisho

kutohudhuria clinick chanzo cha vifo

Na Gurian Adolf
Sumbawanga

TABIA ya wanawake wajawazito mkoani Rukwa kuto hudhuria huduma za kliniki ni miongoni mwa sababu zinazo changia kurudisha nyuma jitihata za kukabiliana vifo vya wajawazito na watoto wachanga mkoani humo.
Mganga mkuu wa mkoa huo Bonifas Kasululu aliyasema hayo jana wakati akiwasilisha mada katika uzinduzi wa mradi wa mama na mwana mkoani Rukwa ambao utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2018 hadi mwaka 2020 na utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 25.
Alisema kuwa pamoja na elimu inayotolewa kwa wanawake mkoani humo kuhudhuria kliniki bado kumekuwa na mwitikio mdogo hali inayosababisha wanawake wengi kupoteza maisha wakati ama baada ya kujifungua kwakuwa hawapatiwi tiba ya matatizo yanayowakabili.
Kasululu alisema kuwa mwanamke mjamzito anapohudhuria klinick inakuwa ni rahisi kutibiwa magonjwa mbalimbali aliyonayo sambamba na kuangalia maendeleo ya ujauzito wake lakini inashindikana kwakuwa hawahudhurii klinick.
Alisema kuwa sababu nyingine ni tabia ya wananwake kujifungulia majumbani nayo ni changamoto kubwa kwani wapo baadhi ya wanawake wajawazito hawataki kujifungulia hospitali hali inayosababisha kupata huduma sahihi wakati wa kujifungua.
Mganga mkuu huyo wa mkoa wa Rukwa alisema kuwa tatizo linakuja pale ambapo mama mjamzito amepata changamoto ya kuvuja damu nyingi ama mtoto mchanga amepata matatizo na anahitaji huduma za kitaalamu wengiwao wamekuwa wakipoteza maisha kwa kukosa huduma hizo.

Katika uzinduzi huo mwakilishi wa wizara ya kutoka  TAMISEMI,Winan Koheleth alisema kuwa serikali bado inawatambua wakunga wa jadi na mpaka sasa hawawezi kuondolewa kutokana na uhaba wa watumishi katika wizara ya afya lakini kilichopo ni kuendelea kuwajengea uwezo.
Alisema kuwa wakunga wanapaswa kuelimishwa kuwa iwapo mama mjamzito amepata changamoto wasimng'ang'anie kumpa huduma badala yake wampeleke hospitali iliaweze kupatiwa huduma stahiki zitakazo okoa maisha ya mama na mtoto.
Akizindua mradi huo wa mama na mwana unaotekelezwa na mashirika ya Jpiego,Africare na Plan International kwa ufadhili wa serikali ya Canada mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo alisisitiza pia suala la lishe kwa watoto mkoani humo kwani unakabiliwa na kiwango kikubwa cha udumavu na utapia mlo.
Alisema kuwa takwimu zinaoshe kuwa udumavu kitaifa upo nchini kwa asilimia 32 wakati mkoa wa Rukwa upo kwa kiwango cha asilimia 56 kitu ambacho kinahitaji mikakati ya kukabiliana nao kwani ukiachwa kuendelea unasababisha madhara katika akili sambamba na kuwa kichocheo katika jitihada za kukabiliana na vifo vya akina mama wajawazito pamoja na watoto wachanga.
Mwisho