Sunday 25 February 2018

Serikali haina mpango wa kuwakopesha wachimbaji wadogo

Na Walter Mguluchuma
Katavi

SERIKALI
imesema kuwa   haina  mpango  wa  kuwakopesha fedha wachimbaji wadogo  bali imeahidi kutatoa mikopo wa vifaa baada ya kubaini kuwa fedha  zilizokuwa  zikitolewa awali wachimbaji hao zilikuwa  hazitumiki kama  ilivyokusudiwa.

Naibi  Waziri wa madini   Doto  Biteko aliyasema hayo jana wakati alipokuwa  akiwahutubia  wachimbaji wadogo wa  madini wa  mkoa wa  Katavi  katika  mkutano wa   hadhara uliofanyika katika   machimbo ya  dhahabu ya   Ibindi  Wilayani   Mpanda.


Alisema  kuwa  Wizara ya  madini imeamua kuondoa  utaratibu  wa  hapo  awali  wa kuwakopesha  fedha wachimbaji wadogo kwa  ajiri ya kununulia  vifaa  vya  kufanyia   shughuli za uchimbaji  na   badala  yake watakuwa  wanawakopesha vifaa.
Waziri huyo alisema kuwa   fedha  zilizokuwa  zikitolewa  na  Serikali  kwa   ajiri ya kuwakopesha  wachimbaji   wadogo  zimekuwa    hazitumiki  kama  ilivyokusudiwa  na   badala  yake wamekuwa  wakizitumia kwa  matumizi       mengine.
 Alieleza  wachimbaji  wadogo  wamekuwa  wakikopeshwa   fedha  kati ya  shilingi Milioni 100 na  milioni 200   lakini  badala ya  kununua  vifaa  vya  kuchimbia    madini wao wamekuwa wakizitumia kwa  ajiri ya  kununua  magari na  kujengea   nyumba .
  Alisema  kuwa     wachimbaji  wadogo  wote  walikopeshwa   fedha  na   wakashindwa  kuzirudisha  wanatakiwa  wazirudishe   mara  moja  kwani kwa  wale watakao shindwa  kurejesha watakamatwa  na  kufikishwa   mahakamani .
  Aliwataka  wachimbaji  wote wa  madini   hapa   nchini    wawe  waaminifu  kwenye  kulipa   kodi  za   Serikali na  wachimbaji  wadogo waache  tabia yao ya  vichochoro   vya  kusafirisha   madini kwa  njia ya  magendo kwani  mchango wa  sekta ya  madini   bado ni  mdogo  kwenye   mapato ya  Taifa  kutoka  na  madini  mengi kuzushwa  nje ya  nchi .
Alisema   Serikali  haiko   tayari  kuona  kazi  zinazoweza  kufanywa  na   Wanzania  kwenye  migodi ya   madini  zinafanywa  na  watu wa kutoka  nchi za   nje  kwani lengo la  Serikali ni kutaka kuona   Watanzania  wananufaika   na  rasilimali za  madini .
Mwenyekiti wa   Chama  cha  Wachimbaji wadogo wa  Mkoa wa  Katavi  Willy  Mbogo   aliiomba  Wizara ya     madini  kutunga   sheria    ambazo   zitakuwa   zinawapa  nafuu   kwani   sheria  za  sasa  haziangalia   aina ya  wachimbaji  wadogo  na wakubwa .
  Alisema   yapo  maeneo  ambayo  ambayo   baadhi ya  wachimbaji  wanayamiliki kwa  kuwa  na  leseni  lakini  yamekuwa  hayaendelezwi  hivyo   ni   vema   serikali   ikawafutia   leseni  wachimbaji  hao .
Katibu  wa  chama  wa   wachimbaji  wadogo wa  Mkoa  huu   Filberti   Sanga   aliomba  wizara  ya  madini  iwafutie  leseni  wachimbaji   ambao     wachindwa  kuyaendeleza  na  bbadala yake  wapewe wachimbaji  wadogo .
 Alisema  wapo  wamiliki wa  leseni  za  madini    ambao  maeneo yao  hawayaendelezi wamekuwa  wakibadili  majina  kila  muda  wao  wa  leseni  kumalizika  kwa kuhofia  kufutiwa  leseni zao .
Mwisho

Saturday 24 February 2018

Padre ashauri watoto wajawazito wafungwe

Na Walter Mguluchuma
Katavi

PADRE
wa Kanisa  Katoliki Jimbo la Mpanda mkoani Katavi, Leonald  Kasimila ameishauri serikali ya mkoa huo kuanza kuwachukulia hatua za kisheria  wasichana  wanaopata  mimba wakiwa  na  umri mdogo pamoja  na  wanaume  waliowapa ujauzito ili iwe ni njia ya kupunguza  tatizo  la  ongezeko la mimba za   utotoni katika mkoa huo.

Ushauri huo  aliotoa jana  kwenye  kikao cha kamati  ya ushauri cha mkoa wa  Katavi RCC  Kilichofanyika jana mkoani humo.

Padre Kasimila alikiambia  kikao  hicho  kuwa  mimba  za utotoni  kwa  asilimia 80  zimekuwa   zikichangiwa na wanaume  na   vijana  wa kiume  huku asilimia 20 zikisababishwa na  wasichana  wenyewe.
 Alisema  ilikukabiliana  na  tatizo  hilo  ni vizuri  sasa   ukaanzishwa  utararibu na   sheria ya kuwakamata na  kuwafungulia   mashitaka wasichana  wanaopata  mimba  badala ya  utaratibu wa  sasa wa kuwakamata wanaume  peke yao.
Aliwaeleza  wajumbe wa  kikao  hicho kuwa kitendo cha kutowachukulia  hatua wasichana  wanaopata   ujauzito  wakiwa  na  umri  mdogo  kunazidi kuwafanya  waone  jambo hilo ni kitu cha  kawaida.

Naye mbunge wa  jimbo  la   Mpanda  Vjijini  Moshi  Kakoso  alisema   kuwa   idadi ya  wanafunzi  wanaoanza kusoma  darasa   la  kwanza  na  wanaofanikiwa  kumaliza shule huwa hailingani  kwa   wanafunzi wa mkoa huo  kutokana  na   baadhi yao kupata  ujauzito wakiwa wanasoma.
 Alisema  zipo  sababu zinazosabisha  wasichana   wengi  kupata ujauzito  na  kuwafanya   wakatishe   masomo  yao kwa   wanafunzi wa   Shule  za   Msingi na   Sekondari ambapo alitaja  miongoni mwa  sababu za  kuwepo kwa  mimba  za utotoni  kuwa ni utoro uliokithiri.
Wanafunzi  kutembea  umbali   mrefu  kwenda  shule hali  ambayo  imekuwa   ikiwafanya  wasichana   kupata    vishawishi  wakati wakiwa  njiani.
Aliomba   Serikali ya   Mkoa  wa  Katavi  ihakikishe  maeneo  ambayo   hayana   vijiji   rasmi  watu wasiruhusiwe   kuishi  kwani   ndio  wamekuwa wakisababisha  watoto wao  kuwa  mbali  na  shule  wanazo  soma.
Afisa  Elimu wa   Mkoa  wa    Katavi   Ernesti   Hinju  alisema   tatizo  la   mimba  za  utotoni kwa   Mkoa wa   Katavi  lipo  na  kwa  takwimu  zilizotolewa  hivi  karibuni   Mkoa  huo   unaasilimia  45 za   mimba  za utotoni   hali  ambayo inaufanya   Mkoa  huo  kuongoza  kwa  kuwa  na  idadi kubwa za  mimba za utotoni hapa   nchini.
Alisema  mimba  hizo  zimekuwa  pia   zikitokea  kwa  wanafunzi wa  sekondari  wakati   ambao  wanapokuwa   wapo    likizo   hivyo jukumu  la  kumlinda   mtoto wa  kike  sio la   walimu  na   mzazi wa  mtoto peke yao  bali  ni  la jamii nzima.
Mkuu wa  Wilaya ya  Mlele  Rachae  Kasanda   aliwaeleza  wajumbe wa kikao  hicho  kuwa  katika   Wilaya  yake ya   Mlele    ameisha anza kuwachukulia  hatua  wazazi wa  wasichana  wanaopata ujauzito wakiwa  na  umri  mdogo .
Pia  katika   Wilaya  hiyo    wameweka    utaratibu wa  kufanya   msako  kwenye   kumbi  za    starehe  na    endapo   watamkuta  mtoto  mwenye  umri  mdogo  huwa  wanamkamata  yeye  na  wazazi  wake.
Mwisho

Serikali ya mkoa yataka mkandarasi alipwe haraka ili amalize ujenzi wa barabra

Na Gurian Adolf
Kalambo

SERIKALI mkoani Rukwa imeshauri mwanamuziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul  (Diamond) atumike kuyatangaza maporomoko ya Kalambo Falls yaliyopo mpakani mwa nchi ya Zambia na Tanzania katika kijiji cha Kapozwa wilaya ya Kalambo mkoani humo.
Mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo alitoa ushauri huo juzi wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi na aliyatembelea maporomoko hayo ambayo ni yapili kwa urefu barani Afrika yenye urefu wa kina zaidi ya mita 230 kwenda chini.
Alisema kuwa maporomoko hayo bado hayajatangazwa vya kutosha kwani watu wengi ikiwemo watanzania wenyewe hawayajui hivyo ili yaweze kufahamika nilazima yakatangazwa na mtu ambaye anafanya vizuri katika sanaa ambaye yeye binafsi anao Diamond anafaa kufanya kazi hiyo.
Wangabo alisema kuwa maporomoko hayo ni miongoni mwa fursa za kitalii mkoani humo ambapo zikitangazwa vizuri zitasababisha kuongeza kipato katika wilaya ya Kalambo,mkoa wa Rukwa na nchini kwa ujumla.
Alisema kuwa mikakati ifanyike ili kujua hatua gani zifikiwe ili Diamond apewe kazi hiyo kwani ni wajibu wa watanzania waliofanikiwa kutangaza rasilimali zao kwani mapato yanayopatikana yanainufaisha nchi kwakuwa watakao tembelea ni watalii wa ndani pamoja na nje ya nchi.

Akizungumzia kauli hiyo ya mkuu wa mkoa mmoja wa wakazi wa kijiji cha Kapozwa wilayani Kalambo ambapo yapo maporomoko yako John Simtowe alisema kuwa anamshukuru mkuu huyo wa mkoa wa Rukwa Wangabo kwa uamuzi wa kuyatangaza maporomoko hayo kwani alisema kuwa iwapo yatafahamika na watalii kuanza kuyatembelea watanufaika kiuchumi.
Alisema kuwa maporomoko ya Kalambo kuwepo katika kijiji hicho ni fursa kwao kwakuwa watafanya biashara kwa watalii watakao kuwa wanayatembelea na kupata fedha tofauti na hivi sasa ambapo hawapati fedha licha ya kuwepo kwa utajiri huo mkubwa ambao bado hauja tangazwa ipasavyo.
Mwisho

Wednesday 21 February 2018

Wafugaji lawamani kukabili mimba za utotoni

Na Gurian Adolf
Nkasi

BAADHI ya wafugaji wilayani Nkasi mkoani Rukwa wamelaumiwa kwakuwa ni kikwazo cha sheria kuchukua mkondo wake katika jitihada za kupambana na mimba za utotoni.
Akizungumza hivi karibuni  mwenyekiti wa kijiji cha Mtenga Soatenes Kalikwenda katika kikao cha siku moja kilichofanyika katika hicho na kufadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la Plan International chenye lengo la kupitia utekelezaji wa mradi wa kupambana nandoa pamoja na mimba za utotoni mwaka 2017 na kuandaa mpango mkakati wa mwaka 2018.
Alisema kuwa baadhi ya wahusika katika kesi hizo wanakuwa ni watoto wa wafugaji ambao wanaishi maisha ya kuhama hama kwaajili ya kutafuta malisho ya mifugo hivyo hujikuta wakihama wakati mashauri hayo yapo mahakamani.
''unakuta aliyepewa ujauzito ni mtoto wa mfugaji,bila kujali kuwa shauri linaendelea mahakani yeye anahama na mtoto wake kwaajili ya kutafuta malisho ya mifugo matokeo yake hawafiki mahakamani na hakuna kinacho endelea'' alisema
Alisema kuwa jambo hilo limekuwa ni changamoto kubwa kiasi kwamba linafifisha jitihada za kukabiriana na ndoa za utotoni pamoja na mimba za utotoni kwakuwa wahusika wanafikiria zaidi mifugo  kuliko hata maisha ya baadae ya watoto wao kuwekeza kwenye elimu.
Naye diwani wa kata ya Mtenga Pankras Maliyatabu alisema kuwa changamoto nyingine iliyopo ni jeshi la polisi kutochukua hatua kwa wakati kitendo kinacho sababisha baadhi ya watuhumiwa kuhama ama kukimbia kabisa.

Diwani huyo alisema kuwa changamoto nyingine ni mtoto mjamzito kufundishwa akataje mahakamani mtuhumiwa zaidi ya mmoja na baada ya kufanya hivyo watuhumiwa huachiwa huru kwakuwa hakuna ujauzito ambao unawahusika wa kiume wawili.

Awali akizungumza wakati wa kupitia mpango kazi huo mratibu wa mradi wa  kuzuia mimba za utotoni wilayani humo,kutoka shirika lisilo la kiserikali la Plan International Nestory Frank alisema kuwa shirika hilo limekwisha baini michezo hiyo lakini isiwe sababu ya kuwakatisha tamaa.
Alisema kuwa kila kazi inachangamoto zake lakini pamoja na mapungufu yaliyopo mafanikio ni makubwa kuliko hapo awali hivyo wanapaswa kuandaa mikakati mipya ya kukabiliana na suala hilo kwani wanaopata madhara ni watoto hao wakike ambao baadhi yao hawajui kuwa wanachokifanya kinaharibu maisha yao ya baadaye.
Mratibu huyo aliisihi jamii wilayani humo kujiandaa kuendeleza mapambano ya tatizo hilo kwakuwa mradi huo upo katika awamu ya tatu na yamwisho na unatarajia kufikia mwisho mwakani.
 
Mwisho

Milioni 700 kujenga kituo cha afya

Na Gurian Adolf
Kalambo
WAKAZI wa kata ya Legezamwedo wilayani Kalambo mkoani Rukwa wanatarajia kuondokana na adha  ya kufuata huduma za afya umbali wa zaidi ya kilomita 50 baada ya serikali kutoa shilingi milioni 700 kwaajili ya kujenga kituo cha afya  katika kata hiyo.
Mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura aliwaambia jana wakazi hao wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika kata hiyo kuwa halmashauri ya wilaya ya Kalambo tayari imekwisha pokea fedha hizo na ujenzi wa kituo hicho cha afya utaanza ndani ya muda mfupi baada ya kukamilika taratibu zote.
Alisema kuwa fedha hizo zipo kinacho subiriwa ni kukamilisha taratibu ndogo ndogo na ujenzi utaanza baada ya muda si mrefu nay eye amekwisha agiza ukamilike ndani ya siku 90 ili wananchi waanze kupata huduma za afya katika kituo hicho cha afya.
Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa kinachotakiwa ni wananchi wa kata hiyo kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano kwa kujitolea nguvu kazi pindi zinapo hitajika kwani zipo kazi kama za kuchima mitaro,kubeba zege na kusogeza tofali zinaweza kufanya na wananchi hao kwa kadiri ya maelekezo ya mafundi ujenzi.
‘’ndugu wanachi serikali imekwisha toa shilingi milioni 700,kinachotakiwa ni nyinyi kuunga mkono katika mchakato mzima wa ujenzi,sitaku kusikia kuna watu wanahujumu jitihada za serikali kwa kuiba vitendea kazi ili ujenzi huo ukamilike kwa wakati’’ alisema
Alisema kuwa serikali imetambua shida wanayopata wananchi hao ndiyo maana imetoa fedha hizo ambazo zinapaswa kutumika kama zilivyo kusudiwa ambapo kata hiyo itapata kituo cha afya na wananchi watatibiwa katika kata hiyo bila usumbufu.
Awali kabla ya kumbalibisha mkuu huyo wa wilaya diwani wa kata hiyo Mwakyusa Larmeck aliishukuru serikali kwa kutoa fedha hizo ambapo alisema wananchi wa kata hiyo walikuwa wakipata matibabu katika kituo cha afya cha Mwimbi kilicho umbali wa kilomita 50.
Alisema kuwa kituo hicho cha afya kitasaidia kupunguza idadi ya vifo vya wakina mama wajawazito na watoto ambao wangekufa kutokana na kuchelewa kupata huduma kwa wakati kutokana na umbali mkubwa uliopo mpaka kufikia kituo cha afya.
Naye Maria Namzosha mkazi wa kata hiyo aliiomba halmashauri hiyo kuwapangia watumishi katika kituo hicho mara baada ya ujenzi kukamilika ili waondokane na kero ya kutembea umbali mkubwa kufuata matibabu kwani wameteseka kwa muda mrefu.
Mwisho

Wanao kkatisha viwanja vya ndege kukamatwa

Na Gurian Adolf
Sumbawanga
SERIKALI imeiagiza mamraka ya viwanja vya ndege nchini TAA kuwakamata na kawachukulia hatua wananchi wenye tabia ya kukatisha katika viwanja vya ndege kwa miguu ama kwa kutumia vyombo vya usafiri ili kukomesha tabia hiyo.
Naibu waziri wa ujenzi na uchukuzi anayeshughulikia usafirishaji na mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye alitoa agizo hilo jana wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani humo ambapo pia alikagua uwanja wa ndege wa mjini Sumbawanga ambao hauna uzio na baadhi ya watu wamekuwa wakikatisha kati kati ya  uwanja huo.
Alisema kuwa kumekuwa na tabia kwa baadhi ya watu kukatisha katika viwanja mbalimbali vya ndege vya mikoani ikiwemo cha Sumbawanga mjini ambapo baadhi ya wananchi wamekuwa wakikatisha kwa miguu,baiskeli,bodaboda na bajaji kitendo ambacho ni hatari kwao na kwa wasafiri wanaotumia viwanja hivyo. 
Waziri Ntitiye pia  aliiagiza mamlaka ya viwanja vya ndege nchi kuhakikisha kuwa inaweka uzio kuzunguka viwanja vya ndege ambavyo vipo wazi ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea kutokana na hali hiyo.
Pia Waziri huyo alizitaka mamlaka husika kutumia sheria ambayo inatoa adhabu kwa watu wanaokatisha katika viwanja hivyo ambapo alisema kuwa mtuhumiwa anatakaye bainika kutenda kosa hilo adhabu yake ni kulipa dola 200 au kifungo cha miezi sita ama vyote pamoja.
Awali kabla ya kukagua uwanja huo ambao umetengewa na serikali  fedha kiasi cha shilingi bilioni 55.5 kwaajili ya kuujenga kisasa,waziri huyo alikutana na wawakilishi wa wanachi ambao wana nyumba kando ya uwanja huo ambao waliiomba serikali iwalipe fidia kwani imekuwa ni muda mrefu.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao mwenyekiti wanaodai fidia hao Adrian Macheta alimwambia waziri kuwa imekuwa ni muda mrefu wakisubiri kulipwa fidia ili kupisha upanuzi wa uwanja huo wa ndege ambapo wanashindwa kukarabati nyumba zao na hivyo kuishi katika makazi chakavu ambayo ni hatari kwao.
Alisema kuwa ni zaidi ya kipindi cha miaka mitano hivi sasa hawanafaida na nyumba zao kwani baadhi yao wanakabiliwa na hali ngumu ya kimaisha ambapo wangetumia nyumba hizo kuziweka dhamana katika mabenki na tasisi nyingine za kifedha na kupata mikopo lakini wanashindwa kwakuwa zitabomolewa kupita upanuzi wa uwanja huo.
Naye Joseph Nyahende mkurugenzi wa viwanja vya ndege mikoani aliwataka wananchi kuheshimu sheria kwani kitendo cha kukatisha kinahatarisha usalama wao na watumiaji wa viwanja hivyo ambapo aliahidi kutekeleza agizo la waziri huyo la kujenga uzio katika viwanja vyote vya ndege nchini ambavyo wananchi wanakatisha katikati.
Mwisho

Thursday 15 February 2018

halmashauri yatakiwa kulipa madeni

Na Walter Mguluchuma
Katavi
Mkuu wa wilaya ya Mpanda mkoani  Katavi  Lilian  Matinga   ameitaka  halmashauri ya wilaya ya Nsimbo kuhakikisha  inawalipa   madeni wazabuni ifikapo  Machi  31  na   endapo ikishindwa kuwalipa isikope  tena kwa  wazabuni  hao mpaka  itakapo  maliza kuwalipa.
Mkuu  huyo wa  Wilaya ya   Mpanda   alitoa  agizo  hilo juzi wakati wa  kikao  cha   baraza  la  biashara la  Mkoa wa  Katavi  TCCIA   kilichofanyika   katika  ukumbi wa  idara ya   maji mjini  hapa .
Matinga  alisema kuwa halmashauri ya hiyo  ndio inayoongoza  katika  Halmashauri  zote  tano zilizopo  katika   Mkoa huo kwa  kuwa na  madeni  mengi  wanayodaiwa  na  wazabuni  mbalimbali   ambao wametoa  huduma  kwenye   halmashauri  hiyo kwa  kipindi cha  muda  mrefu sasa.
  Alisma  kuwa  yeye  kama  Mkuu wa  Wilaya   amekuwa hafurahishwi na  tabia ya   halmashauri  hiyo  kushindwa ya kuwalipa  wazabuni wake na  huku  bado wakiendelea  kukopa  madeni mengine kwa  wazabuni hao.
 Alisema ni  jambo la kusikitisha  sana  kwa halmashauri  kushindwa  kulipa  hata   mzabuni wa  chakula   hivyo   alimwagiza   Mkurugenzi wa  Halmashauri ya  Nsimbo kuhakikisha  ifikapo  Machi 31  kulipa madeni yote  wanayodaiwa  na  wazabuni wao wawe  wameyalipa   vinginevyo  waache  kabisa kukopa kwa wabuni   mpaka  hapo watakapo kuwa wamelipa.
Miongoni  mwa wazabuni wanayoidai  Halmashauri ya  Nsimbo  toka  mwaka  2012  ni  wazabuni wa  chakula ,stationary na  wakandarasi wa  majengo  mbalimbali.
Naye Mwenyekiti wa  TCCIA  wa  Mkoa wa  Katavi   Hassanal   Dalla   alisema   madai ya  wazabuni  hao  yamekuwa  ni ya  muda  mrefu  sasa  na  yamesababisha   baadhi ya  wafanya  biashara kushindwa kuendeleza   shughuli  zao na baadhi yao kufilisika kabisa .
 Alisema wazabuni wamepata  usumbufu  mkubwa  kutoka  kwenye  taasisi mbaimbali za  kibenki   ambako  wafanyabiashara  hao walichukuwa mikopo na  wameshindwa kurudisha kwa  wakati kwani wanadaiwa mara kwa mara.
Kwa upande wake Amani  Mahera mwenyekiti wa  jumuia  ya  Wafanyabiashara Tanzania   tawi la  Mkoa wa  Katavi   alisema  kuwa   hari  hiyo ya  kutolipwa  kwa  wazabuni  madai  yao kumewasababishia   baadhi yao kufunga  biashara zao na wengine kufilisika .
Hivyo  aliiomba  halmashauri  hiyo   kuwalipa  fedha  zao  wazabuni hao  ili  nao  waweze kulipa  kodi za serikali  kwani  inashangaza kwa  mfanyabiashara  kufungiwa kampuni  na  biashara  zake na  mamlaka ya kukusanya  mapato  kwa kosa  la  kushindwa  kulipa  kodi wakati  nayeye  fedha  zake zipo anaidai  halmashauri.
Mwisho

Mashine za EFDs zazua kizaa zaa

Na Gurian Adolf
Katavi

SERIKALI mkoani Katavi imetoa siku 14 kwa makampuni ambayo yalichukua fedha kwaajili ya kuwauzia mashine za EFDs wafanyabishara na mpaka sasa hawajui hatma ya fedha zao.
Mkuu wa wilaya ya Mpanda Lllian  Matinga alitoa siku hizojana  katika kikao maalumu cha kusikiliza kero za wafanyabiashara wa mkoa huo alipo mwakilisha mkuu wa mkoa huo Meja jenerali  Mstaafu  Raphae Muhuga.
Alisema kuwa amefikia uamuzi huo baada ya kuwepo kwa makampuni ambayo yalikuwa yakikusanya fedha kutoka kwa wafanyabiashara na kuahidi kuwapelekea mashine za EFDs lakini imekuwa ni tofauti.
Matiagi alisema kuwa kutokana na kuwa wafanyabiashara hao hawajui hatma ya fedha zao na mpaka sasa hawajapata mashine hizo hivyo ameamua kutoa siku hizo warudishiwe fedha zao vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa.
''natoa siku 14 kwa makampuni yote ambayo yamechukua fedha kutoka kwa wafanyabiashara wa mkuoa huu kuhakikisha kuwa wanarudisha fedha hizo haraka iwezekanavyo tofauti na hivyo serikali ya mkoa haitasita kuchukua hatua'' alisema
Awali katika kikao hicho mwenyekiti wa wafanyabiashara wa mkoa huo Hasanaal  Dalla alimwambia mkuu huyo wa wilaya kuwa wafanyabiashara wa mkoa huo wametapeliwa na makampuni ambapo yamechukua fedha zao kwa ahadi kuwa watawaletea mashine za EFDs lakini imekuwa ni tofauti.
Alisema kuwa imepita muda mrefu mpaka hivi sasa fedha za wafanyabiashara zimechukuliwa na hawajui hatma yao ni nini hivyo alimuomba mkuu huyo wa wilaya aweze kuwasaidia.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa baadhi ya wafanyabiashara wanaonekana kana kwamba hawatii agizo la serikali la kuwataka watumie mashine hizo lakini ukweli ni kwamba walikwisha lipa fedha ili wapate mashine hizo lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea.

Mwisho

Wednesday 14 February 2018

Mkoa watoa siku 14

Na Gurian Adolf
Katavi

SERIKALI mkoani Katavi imetoa siku 14 kwa makampuni na wafanyabiashara ambao walichukua fedha kwaajili ya kuwauzia mashine za EFDs wafanyabishara na mpaka sasa hawajui hatma ya fedha zao.
Mkuu wa wilaya ya Mpanda Lllian  Matinga alitoa siku hizojana  katika kikao maalumu cha kusikiliza kero za wafanyabiashara wa mkoa huo alipo mwakilisha mkuu wa mkoa huo Meja jenerali  Mstaafu  Raphae Muhuga.
Alisema kuwa amefikia uamuzi huo baada ya kuwepo kwa makampuni ambayo yalikuwa yakikusanya fedha kutoka kwa wafanyabiashara na kuahidi kuwapelekea mashine za EFDs lakini imekuwa ni tofauti.
Matiagi alisema kuwa kutokana na kuwa wafanyabiashara hao hawajui hatma ya fedha zao na mpaka sasa hawajapata mashine hizo hivyo ameamua kutoa siku hizo warudishiwe fedha zao vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa.
''natoa siku 14 kwa makampuni yote ambayo yamechukua fedha kutoka kwa wafanyabiashara wa mkuoa huu kuhakikisha kuwa wanarudisha fedha hizo haraka iwezekanavyo tofauti na hivyo serikali ya mkoa haitasita kuchukua hatua'' alisema
Awali katika kikao hicho mwenyekiti wa wafanyabiashara wa mkoa huo Hasanaal  Dalla alimwambia mkuu huyo wa wilaya kuwa wafanyabiashara wa mkoa huo wametapeliwa na makampuni ambapo yamechukua fedha zao kwa ahadi kuwa watawaletea mashine za EFDs lakini imekuwa ni tofauti.
Alisema kuwa imepita muda mrefu mpaka hivi sasa fedha za wafanyabiashara zimechukuliwa na hawajui hatma yao ni nini hivyo alimuomba mkuu huyo wa wilaya aweze kuwasaidia.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa baadhi ya wafanyabiashara wanaonekana kana kwamba hawatii agizo la serikali la kuwataka watumie mashine hizo lakini ukweli ni kwamba walikwisha lipa fedha ili wapate mashine hizo lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea.

Mwisho

Auawa kwa kukanyagwa na tembo

Na Gurian Adolf
Kalambo
MWANAMKE  aliyefahamika kwa jina la Maria Sekaye(60) mkazi wa kijijii cha Ilambila wilayani Kalambo  ameuawa baada ya kukanyagwa na tembo waliokuwa njiani wakitokea katika pori la akiba la Lwafu mkoani Rukwa kuelekea katika nchi jirani ya Zambia.
Akizungumzia tukio hilo diwani wa kata ya Mkowe Alfred Mpandasharo alisema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 4 za asubuhi wakati mwanamke huyo akiwa ametoka kutembelea shamba lake lililokuwa limevamiwa na mazao kuliwa na tembo hao.
Alisema kuwa Maria akiwa njiani kurejea kijijini ghafla alikutana na kundi kubwa la tembo waliokuwa na hasira wakiwa wamechokozwa na vijana wa kijiji hicho kutokana na kuwafukuza kwa makelele ili waondoke kijijini hapo waache kula mazao katika mashamba yao.
Diwani huyo alisema kuwa baada ya kundi hilo la tembo kumkuta mwanamke huyo lilimvamia na kuanguka chini ambapo alikanyagwa na kufa papo hapo.
Naye mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura aliwaonya wananchi wanao wafukuza hovyo tembo hao waache tabia hiyo kwani ni hatari kwa usalama wao wasubiri watendaji wa maliasili ambao watafika kwaajili ya kuwafukuza kijijini hapo.
Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa  kwa kawaida katika vijiji vya  Sundu,Mkowe Ilambila na Katete huwa ni mapito ya tembo ambapo mara kwa mara wamekuwa wakipita kuelekea nchini Zambia na baadaye kurejea tena nchini katika pori la akiba la Lwafu.
Alisema kuwa nivizuri wananchi wakaacha kufanya kilimo na kujenga makazi katika mapito ya tembo hao kwakuwa kawaida huwa hawaachi kupita hata kama itachukua miaka mingi lakini kunasiku watarejea na kupita tena hivyo ni hatari kwao.
Mwisho

Monday 12 February 2018

Waonywa kutotelekeza wagonjwa hospitalini

Na Gurian Adolf
Sumbawanga

Wakazi wa mkoani Rukwa wametakiwa kuacha tabia ya kutelekeza wagonjwa wao hospitalini kwa kisingizio cha kukwepa gharama za matibabu kwani kufanya hivyo kunazipa mzigo mkubwa hospitali wa kuwahudumia wagonjwa hao.

Katibu wa afya wa hospitali ya Kristu Mfalme, Sista Yasinta Rugabagi alisema hayo jana wakati akitoa taarifa ya hospitali hiyo wakati wa maadhimisho ya kikanisa ya siku ya wauguzi duniani yaliyoambatana na ibada ya kuwaombea wagonjwa waliolazwa hospitalini yaliyofanyika Katika hospitali hiyo iliyopo mjini hapa.

Sista Yasinta alisema kuwa kumekuwepo na tabia ya baadhi ya wananchi kutelekeza wagonjwa wao waliougua kwa muda mrefu na kulazwa Katika hospitali hiyo, kitu ambacho kinailazimu hospitali kuwahudumia kila kitu kuanzia gharama za matibabu yao na chakula kwa siku zote wanazokuwa wakipata matibabu kwenye hospitali hiyo.

Alisema hali hiyo imekuwa ikisababisha hospitali kuelemewa na mzigo mkubwa wa kuwahudumia wagonjwa wao kwa kuwa inakabiliwa na changamoto ya fedha hivyo ifike wakati jamii ibadilike na kuachana tabia hiyo kwani kuendelea kufanya hivyo ni kutokuwa na upendo kwa wagonjwa hao. 

Pia alitaka jamii kujenga utamaduni  kutembelea wagonjwa na kutoka misaada mbalimbali kwa wagonjwa si tu wanaolazwa Katika hospitali hiyo lakini na maeneo mengine kwa kuwa wagonjwa wanahitaji kufarijiwa nyakati zote.

Awali, meneja wa mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) Simon Mbaga alizitaka taasisi zilizo chini ya Kanisa Katoliki jimbo la Sumbawanga kujiunga na mfuko wa Bima ya afya ili watumishi wao wawe na uhakika wa kupata matibabu pindi wanapougua maradhi mbalimbali.

Alisema kuwa baadhi ya watumishi wa taasisi hizo wamekuwa wakitumia gharama kubwa kupata matibabu kutokana na kutojiunga na bima ya afya hivyo wana fursa ya kujiunga na mfuko huo kupitia mpango wa uanzishwaji wa vikundi.

Aisha,  Kaimu mganga mkuu wa mkoa, Emmanuel Mtika aliwataka wananchi kujenga utamaduni wa kijitolea damu ikiwa ni njia mojawapo ya kuwasaidia wagonjwa wenye mahitaji ya kuongezewa damu ili kuokoa maisha yao.

Alisema mahitaji ya damu bado ni makubwa Katika mkoa wa Rukwa, ambapo kwa mwezi huitajika lita 200 hadi 300 ambazo husaidia sana kuokoa maisha ya wakinamama wajawazito pindi wanapopungukiwa na damu baada ya kufanyiwa upasuaji. 

Mwisho

UWT Rukwa yachagua kamati ya utekelezaji

Na Gurian Adolf
Sumbawanga
WAJUMBE waliochaguliwa katika nafasi ya utekelezaji ya umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi UWT  mkoa wa Rukwa wametakiwa kuachana na dhana kuwa katika nafasi hiyo watafanikiwa kiuchumi kwani kazi yao kubwa wapon kwaajili ya kujitolea kwa maslahi ya chama.
Mwenyekiti wa umoja huo Merry  Kalula aliyasema hayo jana wakati akifunga baraza maalumu la UWT mkoa lililoketi katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga kwaajili ya kuwachagua wajumbe wanaounda kamati ya utekelezaji wa umoja huo.
Alisema kuwa iwapo kuna mjumbe amegombea nafasi ya ujumbe wa utekelezaji kwa nia ya kutafuta mashahi ni vizuri akajiuzuru ili nafasi yake ikajazwa na mjumbe mwingine kwani kazi inayofanywa ni kujitolewa na wala si kutafuta kipato.
Kalula alisema kuwa sehemu kubwa ya chama hicho wanajitolea,hakuna maslahi yoyote ya kiuchumi wanayoyapata na wanawajibika kukipigania chama hicho ili kiendelee kushika dola ndiyo lengo kubwa la umoja huo na chama cha mapinduzi kwa ujumla.
‘’napenda niwaambie wajumbe mliochaguliwa,kama kunamwanachama aligombea kwaajili ya kutafuta maslahi ya kiuchumi ni vizuri akaachia ngazi kwakua sehemu kubwa tunajitolewa asiwepo mjumbe ambaye amefuata maslahi’’ alisema.
Alisema kuwa UWT mkoa inajukumu kubwa la kuhakikisha kuwa chama hicho kinashinda chaguzi mbalimbali zinazotarajiwa kufanyika na kila mwanajumuia hiyo anapaswa kutambua anafanya jitihada ya kuongeza wanachama waaminifu watakao kuwa wakikichagua chama cha mapinduzi.
Awali akimkaribisha mwenyekiti wa umoja huo katibu wa UWT mkoa Aziza Kiduda alisema kuwa taratibu zote zimefuatwa na wagombea nane wlijitokeza katika kuwania nafasi tano zinazounda kamati ya utekelezaji ya jumuia hiyo.
Waliochaguliwa ni wajumbe wa baraza mkoa wa UWT ambao ndio walipaswa kuwa wagombea wa nafasi ya kamati ya utekelezaji kwa mujibu wa katiba ya umeoja huo.
Mwenyekiti wa umoja huo alimtangaza Ester Wafulukwizya,Rose Chilumba,Mariam Seleman,Rehema Kauzeni pamoja na Mariam Meghji kuwa ndio walioshinda katika uchaguzi huo na kuwa watakuwa wajumbe wa kamati hiyo kwa miaka mitano ijayo.
Akitoa shukrani kwa wapiga kura mmoja wa washindi Ester Wafulukwizya aliwashukuru wajumbe kwa imani kubwa kwa kuwachagua,na pia aliwasihi wale ambao hawakuchagulia wasijioni kuwa hawafai kwani nafasi zilikuwa tano na wagombea ni wanane hivyo lazima wengine wangekosa nafasi.
Alisema kuwa kilichopo ni kushikamana ili kukijenga chama hicho kwani kila mmoja anawajibika kuhakikisha CCM inapata ushindi lakini kama watajitokeza wa kuanzisha mivutano itasababisha kudhoofisha ushindi wa chama hicho katika chaguzi mbalimbali zijazo.
Mwisho