Na Gurian Adolf
Sumbawanga
Mkuu
wa wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa, Dk. Halfan Haule amewataka wakazi
wa bonde ziwa Rukwa, kuacha tabia ya kuwapeleka wagonjwa wa
kipindupindu kwa waganga wa kienyeji badala yake wawapeleke vituo
vinavyotoa huduma za afya ili kupata tiba za kitaalamu.
Mkuu huyo wa wilaya alisema hayo leo wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Mtowisa wilayani Sumbawanga mkoani humo.
Alisema
tabia ya baadhi ya wananchi kuendekeza imani za kushirikina na
kuwapeleka wagonjwa wa kipindupindu kwa waganga wa kienyeji
kunahatarisha maisha ya wagonjwa hao na wakati mwingine kusababisha
vifo.
Alisema jamii ya watu wa bonde la ziwa
Rukwa ambako ugonjwa huo umeenea ipo haja sasa kubadilika na kuachana na
tabia hiyo, kwani ugonjwa huo unatokana na uchafu na si kulogwa hivyo
wanapaswa kuwapeleka wagonjwa katika zahanati, vituo vya afya na
hospitali ili wapate tiba sahihi ambazo zitaokoa maisha yao.
Dk.
Haule alipiga marufuku tabia ya kaya moja kutumia choo kimoja badala
yake alitaka kila kaya kuwa na choo chake na kaya isiyokuwa na choo
hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Awali,mganga
mkuu wa wilaya hiyo,Fani Mussa alisema kuwa tangu ugonjwa wa
kipindupindu uingie katika halmashauri hiyo siku 53 zilizopita jumla ya
wagonjwa 165 wameugua kulazwa katika vituo vinavyotoa huduma ya afya
ambapo nane kati yao wamefariki dunia.
Alisema
hatua mbalimbali zimechukuliwa ikiwa pamoja na kuchukuliwa kwa sampuli
15 ambazo zilithibitisha kuwa na ugonjwa huo hivyo kusambaza dawa na
vifaa tiba katika kambi mbalimbali zilizofunguliwa kwa ajili ya
kuhudumia wagonjwa hao.
Alisema kuwa elimu ya
afya inayolenga kuwahamasisha wananchi kuzingatia kanuni za afya, ikiwa
pamoja na kuchemsha maji kabla kunywa na kunawa mikono baada kutoka
chooni imetolewa kwa wakazi wa bonde la ziwa Rukwa ambalo vijiji vyake
vingi vimeathirika na malazi hayo.
Dk. Mussa
alisema watu 14 kati ya 58 Waliokamatwa kwa kukiuka kanuni za afya ikiwa
pamoja na kaya zao kutokuwa na vyoo wamehukumiwa kifungo cha miezi
mitatu jela.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment