Friday 19 January 2018

Rukwa kupanda miti milioni sita

Na Gurian Adolf
Kalambo

MKOA wa  Rukwa umezindua kampeni ya upandaji miche ya miti kwa lengo la kuhifadhi mazingira ambapo katika kipindi cha mwaka huu unatarajia kupanda jumla ya  miche milioni sita katika halmashauri zote nne za mkoa huo.

Akizundua kampeni katika halmashauri ya wilaya ya Kalambo, katika mji wa Matai mkuu wa mkoa huo Joachim Wamgabo alisema kuwa kila halmashauri italazimika kupanda miche isiyopungua milioni 1.5 ambapo mpaka sasa tayari mkoa mzima umeotesha miche milioni 2,173,649 sawa na asilimia 36 ya miche itakayo pandwa.

Alisema kuwa yeye  amezindua kampeni hiyo kinachofuata ni watendaji wa serikali kuhakikisha kuwa wanasimamia na kutekeleza na itakapofikia mwishoni mwa mwaka halmashauri ambayo haitafikia lengo itatozwa faini ya shilingi milioni moja na fedha hizo itakabidhiwa halmashauri ambayo imetekeleza kampeni hiyo kwa asilimia mia moja.

Awali kabla ya kuzindua kampeni hiyo Wangabo alimuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kalambo Simon Ngagani amwajibishe Afisa mtendaji wa kiji cha Matai Ester Mwashambwa kwa kitendo cha kushindwa kuwahamasisha wananchi wananchi wajitokeze katika uzinduzi wa kampeni hiyo kwani waliofika walikuwa ni wanafunzi wa shule ya sekondari Matai na watumishi wa serikali.

Alisema kuwa wananchi ni wadau wakubwa katika suala la uhifadhi mazingira na ndiyo wakataji miti wakubwa kwa lengo la kupata nishati ya mkaa na kuni lakini kitu cha ajabu hawakuwepo katika uzinduzi huo hali iliyomkera mkuu huyo wa mkoa.

‘’nakuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kalambo kumwajibisha afisa mtendaji wa kijiji kwani ameshindwa kuwahamasisha wananchi wajitokeze,kitendo hiki sijakipenda inaonekana huu ni utendaji mbovu,serikali haiwezi kuwavumilia watendaji wa aina hii’’ alisema

Naye mwakilishi wa wakara wa misitu Tanzania TFS wilaya ya Kalambo, Herman Ndanzi alisema kuwa wakara huo unajumla ya hekta 1192 ambazo unazihudumia licha ya kuwa bado jitihadazinzfanyika za kupanda miti ili kuongeza misitu.

Alisema kuwa wakara huo umewapatia wananchi kilogramu 6 za mbegu za miti ya aina tofauti ili wakaipande ambapo itasaidia kuhifadhi mazingira na kuwa inaendelea na suala kuwaelimisha wananchi waache kuharibu misitu.

Mwisho

No comments:

Post a Comment