Na Gurian Adolf
Kalambo
MKOA wa Rukwa
umezindua kampeni ya upandaji miche ya miti kwa lengo la kuhifadhi mazingira
ambapo katika kipindi cha mwaka huu unatarajia kupanda jumla ya miche milioni sita katika halmashauri zote nne
za mkoa huo.
Akizundua kampeni katika halmashauri ya wilaya ya Kalambo,
katika mji wa Matai mkuu wa mkoa huo Joachim Wamgabo alisema kuwa kila
halmashauri italazimika kupanda miche isiyopungua milioni 1.5 ambapo mpaka sasa
tayari mkoa mzima umeotesha miche milioni 2,173,649 sawa na asilimia 36 ya
miche itakayo pandwa.
Alisema kuwa yeye amezindua kampeni hiyo kinachofuata ni
watendaji wa serikali kuhakikisha kuwa wanasimamia na kutekeleza na
itakapofikia mwishoni mwa mwaka halmashauri ambayo haitafikia lengo itatozwa
faini ya shilingi milioni moja na fedha hizo itakabidhiwa halmashauri ambayo
imetekeleza kampeni hiyo kwa asilimia mia moja.
Awali kabla ya kuzindua kampeni hiyo Wangabo alimuagiza
mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kalambo Simon Ngagani amwajibishe Afisa
mtendaji wa kiji cha Matai Ester Mwashambwa kwa kitendo cha kushindwa kuwahamasisha
wananchi wananchi wajitokeze katika uzinduzi wa kampeni hiyo kwani waliofika
walikuwa ni wanafunzi wa shule ya sekondari Matai na watumishi wa serikali.
Alisema kuwa wananchi ni wadau wakubwa katika suala la
uhifadhi mazingira na ndiyo wakataji miti wakubwa kwa lengo la kupata nishati
ya mkaa na kuni lakini kitu cha ajabu hawakuwepo katika uzinduzi huo hali
iliyomkera mkuu huyo wa mkoa.
‘’nakuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kalambo
kumwajibisha afisa mtendaji wa kijiji kwani ameshindwa kuwahamasisha wananchi
wajitokeze,kitendo hiki sijakipenda inaonekana huu ni utendaji mbovu,serikali
haiwezi kuwavumilia watendaji wa aina hii’’ alisema
Naye mwakilishi wa wakara wa misitu Tanzania TFS wilaya ya
Kalambo, Herman Ndanzi alisema kuwa wakara huo unajumla ya hekta 1192 ambazo
unazihudumia licha ya kuwa bado jitihadazinzfanyika za kupanda miti ili
kuongeza misitu.
Alisema kuwa wakara huo umewapatia wananchi kilogramu 6 za
mbegu za miti ya aina tofauti ili wakaipande ambapo itasaidia kuhifadhi
mazingira na kuwa inaendelea na suala kuwaelimisha wananchi waache kuharibu
misitu.
Mwisho
No comments:
Post a Comment