Wednesday 21 February 2018

Wanao kkatisha viwanja vya ndege kukamatwa

Na Gurian Adolf
Sumbawanga
SERIKALI imeiagiza mamraka ya viwanja vya ndege nchini TAA kuwakamata na kawachukulia hatua wananchi wenye tabia ya kukatisha katika viwanja vya ndege kwa miguu ama kwa kutumia vyombo vya usafiri ili kukomesha tabia hiyo.
Naibu waziri wa ujenzi na uchukuzi anayeshughulikia usafirishaji na mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye alitoa agizo hilo jana wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani humo ambapo pia alikagua uwanja wa ndege wa mjini Sumbawanga ambao hauna uzio na baadhi ya watu wamekuwa wakikatisha kati kati ya  uwanja huo.
Alisema kuwa kumekuwa na tabia kwa baadhi ya watu kukatisha katika viwanja mbalimbali vya ndege vya mikoani ikiwemo cha Sumbawanga mjini ambapo baadhi ya wananchi wamekuwa wakikatisha kwa miguu,baiskeli,bodaboda na bajaji kitendo ambacho ni hatari kwao na kwa wasafiri wanaotumia viwanja hivyo. 
Waziri Ntitiye pia  aliiagiza mamlaka ya viwanja vya ndege nchi kuhakikisha kuwa inaweka uzio kuzunguka viwanja vya ndege ambavyo vipo wazi ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea kutokana na hali hiyo.
Pia Waziri huyo alizitaka mamlaka husika kutumia sheria ambayo inatoa adhabu kwa watu wanaokatisha katika viwanja hivyo ambapo alisema kuwa mtuhumiwa anatakaye bainika kutenda kosa hilo adhabu yake ni kulipa dola 200 au kifungo cha miezi sita ama vyote pamoja.
Awali kabla ya kukagua uwanja huo ambao umetengewa na serikali  fedha kiasi cha shilingi bilioni 55.5 kwaajili ya kuujenga kisasa,waziri huyo alikutana na wawakilishi wa wanachi ambao wana nyumba kando ya uwanja huo ambao waliiomba serikali iwalipe fidia kwani imekuwa ni muda mrefu.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao mwenyekiti wanaodai fidia hao Adrian Macheta alimwambia waziri kuwa imekuwa ni muda mrefu wakisubiri kulipwa fidia ili kupisha upanuzi wa uwanja huo wa ndege ambapo wanashindwa kukarabati nyumba zao na hivyo kuishi katika makazi chakavu ambayo ni hatari kwao.
Alisema kuwa ni zaidi ya kipindi cha miaka mitano hivi sasa hawanafaida na nyumba zao kwani baadhi yao wanakabiliwa na hali ngumu ya kimaisha ambapo wangetumia nyumba hizo kuziweka dhamana katika mabenki na tasisi nyingine za kifedha na kupata mikopo lakini wanashindwa kwakuwa zitabomolewa kupita upanuzi wa uwanja huo.
Naye Joseph Nyahende mkurugenzi wa viwanja vya ndege mikoani aliwataka wananchi kuheshimu sheria kwani kitendo cha kukatisha kinahatarisha usalama wao na watumiaji wa viwanja hivyo ambapo aliahidi kutekeleza agizo la waziri huyo la kujenga uzio katika viwanja vyote vya ndege nchini ambavyo wananchi wanakatisha katikati.
Mwisho

No comments:

Post a Comment