Na Gurian Adolf
Katavi
SERIKALI mkoani Katavi imetoa siku 14 kwa makampuni na wafanyabiashara ambao walichukua fedha kwaajili ya kuwauzia mashine za EFDs wafanyabishara na mpaka sasa hawajui hatma ya fedha zao.
Mkuu wa wilaya ya Mpanda
Lllian Matinga
alitoa siku hizojana katika kikao maalumu cha kusikiliza kero za wafanyabiashara wa mkoa huo alipo mwakilisha mkuu wa mkoa huo Meja jenerali Mstaafu Raphae Muhuga.Katavi
SERIKALI mkoani Katavi imetoa siku 14 kwa makampuni na wafanyabiashara ambao walichukua fedha kwaajili ya kuwauzia mashine za EFDs wafanyabishara na mpaka sasa hawajui hatma ya fedha zao.
Awali katika kikao hicho mwenyekiti wa wafanyabiashara wa mkoa huo Hasanaal Dalla alimwambia mkuu huyo wa wilaya kuwa wafanyabiashara wa mkoa huo wametapeliwa na makampuni ambapo yamechukua fedha zao kwa ahadi kuwa watawaletea mashine za EFDs lakini imekuwa ni tofauti.
Alisema kuwa
imepita muda mrefu mpaka hivi sasa fedha za wafanyabiashara
zimechukuliwa na hawajui hatma yao ni nini hivyo alimuomba mkuu huyo wa
wilaya aweze kuwasaidia.
Mwenyekiti huyo
alisema kuwa baadhi ya wafanyabiashara wanaonekana kana kwamba hawatii
agizo la serikali la kuwataka watumie mashine hizo lakini ukweli ni
kwamba walikwisha lipa fedha ili wapate mashine hizo lakini mpaka sasa
hakuna kinachoendelea.
Mwisho
Mwisho
No comments:
Post a Comment