Thursday 15 February 2018

halmashauri yatakiwa kulipa madeni

Na Walter Mguluchuma
Katavi
Mkuu wa wilaya ya Mpanda mkoani  Katavi  Lilian  Matinga   ameitaka  halmashauri ya wilaya ya Nsimbo kuhakikisha  inawalipa   madeni wazabuni ifikapo  Machi  31  na   endapo ikishindwa kuwalipa isikope  tena kwa  wazabuni  hao mpaka  itakapo  maliza kuwalipa.
Mkuu  huyo wa  Wilaya ya   Mpanda   alitoa  agizo  hilo juzi wakati wa  kikao  cha   baraza  la  biashara la  Mkoa wa  Katavi  TCCIA   kilichofanyika   katika  ukumbi wa  idara ya   maji mjini  hapa .
Matinga  alisema kuwa halmashauri ya hiyo  ndio inayoongoza  katika  Halmashauri  zote  tano zilizopo  katika   Mkoa huo kwa  kuwa na  madeni  mengi  wanayodaiwa  na  wazabuni  mbalimbali   ambao wametoa  huduma  kwenye   halmashauri  hiyo kwa  kipindi cha  muda  mrefu sasa.
  Alisma  kuwa  yeye  kama  Mkuu wa  Wilaya   amekuwa hafurahishwi na  tabia ya   halmashauri  hiyo  kushindwa ya kuwalipa  wazabuni wake na  huku  bado wakiendelea  kukopa  madeni mengine kwa  wazabuni hao.
 Alisema ni  jambo la kusikitisha  sana  kwa halmashauri  kushindwa  kulipa  hata   mzabuni wa  chakula   hivyo   alimwagiza   Mkurugenzi wa  Halmashauri ya  Nsimbo kuhakikisha  ifikapo  Machi 31  kulipa madeni yote  wanayodaiwa  na  wazabuni wao wawe  wameyalipa   vinginevyo  waache  kabisa kukopa kwa wabuni   mpaka  hapo watakapo kuwa wamelipa.
Miongoni  mwa wazabuni wanayoidai  Halmashauri ya  Nsimbo  toka  mwaka  2012  ni  wazabuni wa  chakula ,stationary na  wakandarasi wa  majengo  mbalimbali.
Naye Mwenyekiti wa  TCCIA  wa  Mkoa wa  Katavi   Hassanal   Dalla   alisema   madai ya  wazabuni  hao  yamekuwa  ni ya  muda  mrefu  sasa  na  yamesababisha   baadhi ya  wafanya  biashara kushindwa kuendeleza   shughuli  zao na baadhi yao kufilisika kabisa .
 Alisema wazabuni wamepata  usumbufu  mkubwa  kutoka  kwenye  taasisi mbaimbali za  kibenki   ambako  wafanyabiashara  hao walichukuwa mikopo na  wameshindwa kurudisha kwa  wakati kwani wanadaiwa mara kwa mara.
Kwa upande wake Amani  Mahera mwenyekiti wa  jumuia  ya  Wafanyabiashara Tanzania   tawi la  Mkoa wa  Katavi   alisema  kuwa   hari  hiyo ya  kutolipwa  kwa  wazabuni  madai  yao kumewasababishia   baadhi yao kufunga  biashara zao na wengine kufilisika .
Hivyo  aliiomba  halmashauri  hiyo   kuwalipa  fedha  zao  wazabuni hao  ili  nao  waweze kulipa  kodi za serikali  kwani  inashangaza kwa  mfanyabiashara  kufungiwa kampuni  na  biashara  zake na  mamlaka ya kukusanya  mapato  kwa kosa  la  kushindwa  kulipa  kodi wakati  nayeye  fedha  zake zipo anaidai  halmashauri.
Mwisho

No comments:

Post a Comment