Na Gurian Adolf
Kalambo
WAKAZI wa kata ya Legezamwedo wilayani Kalambo mkoani Rukwa
wanatarajia kuondokana na adha ya
kufuata huduma za afya umbali wa zaidi ya kilomita 50 baada ya serikali kutoa
shilingi milioni 700 kwaajili ya kujenga kituo cha afya katika kata hiyo.
Mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura aliwaambia jana
wakazi hao wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika kata hiyo kuwa
halmashauri ya wilaya ya Kalambo tayari imekwisha pokea fedha hizo na ujenzi wa
kituo hicho cha afya utaanza ndani ya muda mfupi baada ya kukamilika taratibu
zote.
Alisema kuwa fedha hizo zipo kinacho subiriwa ni kukamilisha
taratibu ndogo ndogo na ujenzi utaanza baada ya muda si mrefu nay eye amekwisha
agiza ukamilike ndani ya siku 90 ili wananchi waanze kupata huduma za afya
katika kituo hicho cha afya.
Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa kinachotakiwa ni wananchi
wa kata hiyo kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano kwa kujitolea
nguvu kazi pindi zinapo hitajika kwani zipo kazi kama za kuchima mitaro,kubeba
zege na kusogeza tofali zinaweza kufanya na wananchi hao kwa kadiri ya
maelekezo ya mafundi ujenzi.
‘’ndugu wanachi serikali imekwisha toa shilingi milioni
700,kinachotakiwa ni nyinyi kuunga mkono katika mchakato mzima wa ujenzi,sitaku
kusikia kuna watu wanahujumu jitihada za serikali kwa kuiba vitendea kazi ili
ujenzi huo ukamilike kwa wakati’’ alisema
Alisema kuwa serikali imetambua shida wanayopata wananchi
hao ndiyo maana imetoa fedha hizo ambazo zinapaswa kutumika kama zilivyo
kusudiwa ambapo kata hiyo itapata kituo cha afya na wananchi watatibiwa katika
kata hiyo bila usumbufu.
Awali kabla ya kumbalibisha mkuu huyo wa wilaya diwani wa
kata hiyo Mwakyusa Larmeck aliishukuru serikali kwa kutoa fedha hizo ambapo
alisema wananchi wa kata hiyo walikuwa wakipata matibabu katika kituo cha afya
cha Mwimbi kilicho umbali wa kilomita 50.
Alisema kuwa kituo hicho cha afya kitasaidia kupunguza idadi
ya vifo vya wakina mama wajawazito na watoto ambao wangekufa kutokana na
kuchelewa kupata huduma kwa wakati kutokana na umbali mkubwa uliopo mpaka
kufikia kituo cha afya.
Naye Maria Namzosha mkazi wa kata hiyo aliiomba halmashauri
hiyo kuwapangia watumishi katika kituo hicho mara baada ya ujenzi kukamilika
ili waondokane na kero ya kutembea umbali mkubwa kufuata matibabu kwani
wameteseka kwa muda mrefu.
Mwisho
No comments:
Post a Comment