Na Gurian Adolf
Kalambo
SERIKALI mkoani Rukwa imeshauri mwanamuziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul (Diamond) atumike kuyatangaza maporomoko ya Kalambo Falls yaliyopo mpakani mwa nchi ya Zambia na Tanzania katika kijiji cha Kapozwa wilaya ya Kalambo mkoani humo.
Mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo
alitoa ushauri huo juzi wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi na
aliyatembelea maporomoko hayo ambayo ni yapili kwa urefu barani Afrika
yenye urefu wa kina zaidi ya mita 230 kwenda chini.Kalambo
SERIKALI mkoani Rukwa imeshauri mwanamuziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul (Diamond) atumike kuyatangaza maporomoko ya Kalambo Falls yaliyopo mpakani mwa nchi ya Zambia na Tanzania katika kijiji cha Kapozwa wilaya ya Kalambo mkoani humo.
Akizungumzia
kauli hiyo ya mkuu wa mkoa mmoja wa wakazi wa kijiji cha Kapozwa
wilayani Kalambo ambapo yapo maporomoko yako John Simtowe alisema kuwa
anamshukuru mkuu huyo wa mkoa wa Rukwa Wangabo kwa uamuzi wa kuyatangaza
maporomoko hayo kwani alisema kuwa iwapo yatafahamika na watalii kuanza
kuyatembelea watanufaika kiuchumi.
Alisema kuwa
maporomoko ya Kalambo kuwepo katika kijiji hicho ni fursa kwao kwakuwa
watafanya biashara kwa watalii watakao kuwa wanayatembelea na kupata
fedha tofauti na hivi sasa ambapo hawapati fedha licha ya kuwepo kwa
utajiri huo mkubwa ambao bado hauja tangazwa ipasavyo.
Mwisho
No comments:
Post a Comment