Na Gurian Adolf
Nkasi
BAADHI ya wafugaji wilayani Nkasi mkoani Rukwa wamelaumiwa kwakuwa ni kikwazo cha sheria kuchukua mkondo wake katika jitihada za kupambana na mimba za utotoni.
Akizungumza hivi karibuni mwenyekiti wa kijiji
cha Mtenga Soatenes Kalikwenda katika kikao cha siku moja kilichofanyika
katika hicho na kufadhiliwa na
shirika lisilo la kiserikali la Plan International chenye lengo la
kupitia utekelezaji wa mradi wa kupambana nandoa pamoja na mimba za
utotoni mwaka 2017 na kuandaa mpango mkakati wa mwaka 2018.Nkasi
BAADHI ya wafugaji wilayani Nkasi mkoani Rukwa wamelaumiwa kwakuwa ni kikwazo cha sheria kuchukua mkondo wake katika jitihada za kupambana na mimba za utotoni.
Diwani huyo alisema kuwa changamoto nyingine ni mtoto mjamzito kufundishwa akataje mahakamani mtuhumiwa zaidi ya mmoja na baada ya kufanya hivyo watuhumiwa huachiwa huru kwakuwa hakuna ujauzito ambao unawahusika wa kiume wawili.
Awali akizungumza wakati wa
kupitia mpango kazi huo mratibu wa mradi wa kuzuia mimba za utotoni
wilayani humo,kutoka shirika lisilo la kiserikali la
Plan International Nestory Frank alisema kuwa shirika hilo limekwisha baini michezo
hiyo lakini isiwe sababu ya kuwakatisha tamaa.
Alisema kuwa
kila kazi inachangamoto zake lakini pamoja na mapungufu yaliyopo
mafanikio ni makubwa kuliko hapo awali hivyo wanapaswa kuandaa mikakati
mipya ya kukabiliana na suala hilo kwani wanaopata madhara ni watoto hao
wakike ambao baadhi yao hawajui kuwa wanachokifanya kinaharibu maisha
yao ya baadaye.
Mratibu huyo aliisihi jamii wilayani
humo kujiandaa kuendeleza mapambano ya tatizo hilo kwakuwa mradi huo upo
katika awamu ya tatu na yamwisho na unatarajia kufikia mwisho mwakani.
Mwisho
No comments:
Post a Comment