Katavi
PADRE wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda mkoani Katavi, Leonald Kasimila ameishauri serikali ya mkoa huo kuanza kuwachukulia hatua za kisheria wasichana wanaopata mimba wakiwa na umri mdogo pamoja na wanaume waliowapa ujauzito ili iwe ni njia ya kupunguza tatizo la ongezeko la mimba za utotoni katika mkoa huo.
Ushauri huo aliotoa jana kwenye kikao cha kamati ya ushauri cha mkoa wa Katavi RCC Kilichofanyika jana mkoani humo.
Padre Kasimila alikiambia
kikao hicho kuwa
mimba za utotoni kwa
asilimia 80 zimekuwa zikichangiwa na wanaume na
vijana wa kiume huku asilimia 20 zikisababishwa na wasichana
wenyewe.
Alisema ilikukabiliana na
tatizo hilo ni vizuri
sasa ukaanzishwa utararibu na
sheria ya kuwakamata na kuwafungulia
mashitaka wasichana wanaopata mimba badala ya
utaratibu wa sasa wa kuwakamata
wanaume peke yao.
Aliwaeleza
wajumbe wa kikao hicho kuwa kitendo cha kutowachukulia hatua
wasichana wanaopata ujauzito wakiwa
na umri mdogo
kunazidi kuwafanya waone jambo hilo
ni kitu cha kawaida.
Naye mbunge wa jimbo la
Mpanda Vjijini Moshi
Kakoso alisema kuwa
idadi ya wanafunzi wanaoanza kusoma darasa
la kwanza na
wanaofanikiwa kumaliza shule huwa hailingani kwa wanafunzi wa mkoa huo
kutokana na baadhi yao kupata ujauzito wakiwa wanasoma.
Alisema zipo
sababu zinazosabisha wasichana
wengi kupata ujauzito na
kuwafanya wakatishe masomo
yao kwa wanafunzi wa Shule
za Msingi na Sekondari ambapo
alitaja miongoni mwa sababu za
kuwepo kwa mimba za utotoni
kuwa ni utoro uliokithiri.
Wanafunzi
kutembea umbali mrefu
kwenda
shule hali
ambayo imekuwa ikiwafanya
wasichana kupata vishawishi
wakati wakiwa njiani.
Aliomba
Serikali ya Mkoa wa
Katavi ihakikishe maeneo
ambayo hayana vijiji
rasmi watu wasiruhusiwe kuishi
kwani ndio wamekuwa wakisababisha watoto wao
kuwa mbali na
shule wanazo soma.
Afisa Elimu wa Mkoa
wa Katavi Ernesti
Hinju alisema tatizo
la mimba za
utotoni kwa Mkoa wa Katavi
lipo na kwa
takwimu zilizotolewa hivi
karibuni Mkoa huo
unaasilimia 45 za mimba
za utotoni hali ambayo inaufanya Mkoa
huo kuongoza kwa
kuwa na idadi kubwa za mimba za utotoni hapa nchini.
Alisema mimba hizo
zimekuwa pia zikitokea
kwa wanafunzi wa sekondari
wakati ambao wanapokuwa
wapo likizo hivyo jukumu
la kumlinda mtoto wa
kike sio la walimu
na mzazi wa mtoto peke yao bali
ni la jamii nzima.
Mkuu wa Wilaya
ya Mlele Rachae
Kasanda aliwaeleza wajumbe wa kikao hicho
kuwa katika Wilaya
yake ya Mlele ameisha anza kuwachukulia hatua
wazazi wa wasichana wanaopata ujauzito wakiwa na
umri mdogo .
Pia katika Wilaya
hiyo wameweka utaratibu wa kufanya
msako kwenye kumbi
za starehe na
endapo watamkuta mtoto
mwenye umri mdogo
huwa wanamkamata yeye
na wazazi wake.
Mwisho
No comments:
Post a Comment