Monday 28 May 2018

Nkasi kinara kwa ujauzito

Na Gurian Adolf
Nkasi
HALMASHAURI ya wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa imetajwa kuwa ndiyo inayo ongoza kwa wanafunzi wanafunzi kupata ujauzito mkoani Rukwa na katika kipindi cha miezi tisa jumla ya wanafunzi 74 wamekatiza masomo kutokana na kupata ujauzito.
Akizungumza jana  kwenye kikao cha baraza la madiwani afisa serikali za mitaa mkoani humo Albinus Mgonya alisema kuwa kwa kipindi cha kuanzia mwezi Julai mwaka jana hadi april 30 mwaka huu  wanafunzi 36 wanafunzi wa shule za msingi na wanafunzi38 wa sekondari walipata ujauzito.
Alisema kuwa kulingana na takwimu hizo inamaana kuwa wanafunzi wanaopata ujauzito ni sawa na kuwa kila mwezi wanafunzi  wanne wa shule za msingi  wanapata mimba sambamba na wanne wa sekondari wanapata ujauzito.
Mgonya alisema kuwa kutokana na hali hiyo ameiagiza halmashauri ya wilaya Nkasi kuandaa taarifa itakayoainisha idadi ya Watoto wenye mimba  mahali walipo,wazazi  wao ikiwa ni pamoja na viongozi wa maeneo yao hasa Watendaji wao wa vijiji na kata ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Katika hatua nyingine afisa huyo wa serikali za mitaa ameipongeza halmashauri ya wilaya Nkasi kwa kufanya vizuri katika makusanyo ya ndani ambapo hadi sasa makusanyo ni asilimia 76 na kuwa wilaya hiyo inaongoza kimkoa katika suala zima la makusanyo ikiwa ni pamoja na wilaya kuendelea kupata hati safi.
Kwa upande wake Katibu tawala wa wilaya hiyo Festo Chonya ameitaka halmashauri hiyo kutowahamisha watendaji wabovu bali washughulikiwe pale pale walipo ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi kwani serikali ya sasa haiwezi kuwahamisha watendaji wabovu kutoka eneo moja kwenda jingine.
Alisema kuwa katika mjadala ulioendelea katika kikao hicho madiwani walisema  kuwa yupo afisa mtendaji mmoja wa kijiji ambaye ameonyesha uwezo mdogo wa kiutendaji  na kuiomba halmashauri  imuhamishe kutoka katika kijiji alipo na  kwenda eneo jingine.
Chonya alisema kuwa  serikali ya awamu ya tano haimuhamishi mtumishi ambaye ameshindwa katika eneo moja  na kwenda eneo jingine na kuwa mawazo hayo ya madiwani si sahihi bali kama mtendaji huyo ameshindwa kuwajibika waanze mchakato mwa kumfukuza kazi na aajiriwe mwingine mwenye uwezo wa kazi.
Naye mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Zeno Mwanakulya aliwataka watendaji wa halmashauri kuyasimamia yale yote yaliyoagizwa katika kikao hicho ,huku akisisitiza suala la uwajibikaji ili kuweza kufikia malengo waliyojiwekea.
Kaimu mkurugenzi  wa halmahsauri ya wilaya hiyo  Missana Kwangula alisema kuwa halmashauri ya wilaya inafanya kazi vizuri na ndiyo maana kila mwaka imekua ikipata hati safi hasa katika eneo la makusanyo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment