Thursday 29 June 2017

Marufuku kuchungia mifugo ndani ya hifadhi

Na Gurian Adolf
Katavi
Wizara ya  Maliasili na  Utalii imewaonya wafugaji hapa nchini kuacha tabia yakwenda kuchungia mifugo yao katika hifadhi za taifa na mapori ya akiba kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria na watambue kuwa hawataepuka mkono wa sheria iwapo watabainika wakiingiza mifugo yao humo.
Amewataka  Wahifadhi wote  kushirikiana  na  Mamlaka za  Mikoa  na  Wilaya  ili kuweza  kukabiliana  na  tatizo  la uvamizi  wa maeneo  ya  hifadhi  yanayofanywa  kwa ajili ya shughuli za kibinadamu  hususani  uvamizi wa mifugo  kwenye  maeneo ya hifadhi .
Onyo hilo limetolewa jana na  Katibu  Mkuu  wa   Wizara ya   Maliasili na  Utalii  Meja Generali  Gaudence  Milanzi alipokua  akifunga   mafunzo  ya uongozi  kwa maafisa   Wanyama  pori   yenye  lengo  la kuwafanya wafanye  kazi  kutoka  mfumo wa kiraia   na kuwa mfumo wa kijeshi yaani Jeshi usu, yaliofanyika  katika kituo cha  mafunzo   Mlele  Mkoani  Katavi .
Alisema kuwa hivi sasa  uhifadhi unakabiliwa  na tatizo  la uvamizi  unaonywa kwa shughuli za kibinadamu  hususani  uchungaji wa mifugo  kwenye  maeneo ya hifadhi baadhi ya maeneo hata binadamu kujenga na kuishi ndani ya maeneo ya uhifadhi kitendo ambacho ni kosa kisheria na kamwe hakita vumiliwa.
 Meja Jenerali huyo alisema kuwa Wizara  inatoa wito  kwa   Wahifadhi wote  na kwa kushirikiana  na  Mamlaka  za  Mikoa  na  Wilaya  husika  kulimaliza kabisa  tatizo  hilo.
  Aliwaagiza wahitimu wa  mafunzo  hayo  washirikiane na wakuu  wao  kupanga mipango  itakayo  washirikisha  wananchi  katika  kumaliza  tatizo  la uvamizi  wa mifugo  kwenye  maeneo  ya  hifadhi  na  migogoro ya mipaka   kati ya  maeneo  ya  hifadhi  na  Vijiji kwani nalo zimekuwa ni changamoto kubwa.
Milanzi  aliwaomba  wananchi  wote kuendelea  kuheshimu   sheria  za  nchi  na kuacha  kufanya  shughuli  za  kibinadamu  kwenye  maeneo ya  hifadhi  kwani watambue kuwa kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Alisema  kwa  kipindi  cha  miaka  ya  hivi  karibuni wizara ya   Maliasili na   Utalii  imeshuhudia  baadhi ya  matukio  ya mmomonyoko  mkubwa wa  maadili  hasa   kwa watumishi  wa  kada  ya   Askari  wao  wenyewe kujihusisha  na vitendo  vya  ujangili  na  mengine  mambo yasiyo faa  katika utumishi wa umma.
 Alieleza kuwa  mafunzo waliopatiwa    wahitimu  hao   anaamini kuwa  kwa  kuwa wao ndio  viongozi wakuu wa  askari  watakwenda  kusaidia  kurudisha  nidhamu kwa  askari  na watumishi  wa chini yao kwa kuwaelekeza   mambo mazuri  ya kujenga  wanayotakiwa  kuyafanya  ili kuhakikisha  kunakuwepo na uhifadhi endelevu wa maliasili  za  nchi.
Kaimu   kwaupande wake Mkurugenzi  Mkuu wa  Mamlaka ya  Wanyama  pori Tanzania   Martin  Loibooki  alisema  ulinzi wa  rasilimali  za  Wanyama  pori  umeendelea  kuimarika ndani  na  nje  ya  mapori ya  akiba na   tengefu  sambamba  na kuimarisha  ukaguzi wa  nyara  katika  maeneo  ya  mipakani  kwa kushirikiana   na wadau wengine.
  Chini  ya uongozi wa  Wizara  TAWA   imeshirikiana  na idara  ya Wanyama pori ,TANAPA  na  mamlaka  ya  hifadhi  Ngorongoro NCCA  katika  kutekeleza  kazi  mbalimbali.
Mafunzo  hayo ya  wiki sita  yaliwashirikisha  wahitimu 97 wakiwemo   Maafisa  wandamizi  20 na    maafisa wa  kati 77 wa  kutoka Mamlaka  ya  Wanyama  pori   Tanzania   TAWA.
Mwisho

No comments:

Post a Comment