Thursday 29 June 2017

Amuua rafiki yake akimdai mbao mbili

Na Gurian  Adolf
Sumbawanga
MTU mmoja anayefahamika kwa jina la Fokas Pera(48)  mkazi wa kitongoji cha Ilemba B, kata ya Nankanga tarafa ya Laela wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa ameuawa na rafiki yake kwa kumkata na kitu chenye ncha kali kinachodhaniwa kuwa ni panga kichwani kwa madai kuwa alimdhurumu mbao mbili.
Tukio la  mauaji hayo kilitokea Juni 28 majira ya saa  3:00 asubuhi katika kitongoji hicho baada ya kumhadaa marehemu na kwenda naye porini ambako  yalifanyika mauaji hayo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Rukwa George Kyando alisema kuwa marehemu alikuwa akidaiwa mbao  mbili na rafiki yake aitwaye Paul Kayuni (50) mkazi wa kitongoji hicho ambazo anadaiwa alimpa rafiki yake huyo.
Baada ya kumdai  kwa muda mrefu Pera  alikuwa akisumbua kulipa hali iliyomkasilisha mtuhumiwa na kupanga kumpiga  kutokana na usumbufu aliokuwa  akiufanya.
Siku hiyo mtuhumiwa alimtumia rafiki zake marehemu kuwa waende porini wakamuuzie mbao naye alikubali na alipofika kule polini alimkuta mtu  anayemdai ambapo alianza kumshushia kipigo.
Akiwa anampiga marehemu naye aliamua  aanze kupigana  hali ambayo ilimfanya mtuhumiwa kuchukua panga  aliyokuwa ameficha porini na kumkata  nayo  kichwani ambapo alimsababishia jeraha kubwa lililoanza kuvuja damu nyingi.
Baada ya kuvuja damu nyingi katika jeraha hilo alianguka chini  na kupoteza fahamu ambapo walimchukua na kumkimbiza katika zahanati ya kijiji kwaajili ya matibabu.
Alipofikishwa katika zahanati ya kijiji hicho mganga wa zamu alipompokea na kumfanyia uchunguzi aliwaambia amekwisha  fariki kutokana na kuvuja damu nyingi kutokana na jeraha alilopata.
Polisi inamshikilia mtuhumiwa wa mauaji hayo na atafikishwa mahakamani pindi upelelezi wa awali utakapokuwa umekamilika.

Mwisho

No comments:

Post a Comment