Na Gurian Adolf
Katavi
WAZIRI wa ujenzi uchukuzi na
Mawasiliano mhandisi Isack
Kamwelwe ameyaagiza
Makampuni ya ujenzi kuhakikisha kuwa
wanamwagia maji kwenye
sehemu za makazi ya watu
pindi wanapokuwa wakitengeneza
barabara ili kuwaondolea
vumbi na kuwaepusha na magonjwa .
Alitoa agizo hilo jana kwa nyakati
tofauti katika maeneo ya Majalila
Wilayani Tanganyika na
katika Kijiji cha
Inyonga Wilayani Mlele mkoani Katavi wakati akikagua ujenzi wa
barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mpanda mkoani katavi
hadi sikonge Mkoani Tabora.
Alisema kuwa kumekuwa
na tabia ya wakandarasi wa makampuni ya
kichina wanaotengeneza
barabara kwenye maeneo
mbalimbali hapa nchini kutomwagilia
maji kwenye maeneo ya
makazi wanayoishi watu hivyo kuwasababishia kero kubwa ya vumbi.
Alisema kuwa ni wajibu wa
kila kampuni inayotengeneza barabara
kumwagia maji kwenye maeneo
wanayoishi watu kwani
kwenye mikataba yao wanatakiwa kufanya
hivyo na wanalipwa
fedha na Serikali hivyo
swala la uwagiliaji wa maji ni la lazima.
Waziri huyo alisema kuwa
matokeo ya kutomwagia maji
kwenye maeneo ya
makazi kwanasababisha wananchi
kupata maradhi ya ugonjwa
wa vifua na mafua.
Alisema kuwa licha ya ujenzi
wa barabara ya
Mpanda Tabora kwa
kiwango cha lami pia serikali imepanga kutengeneza
barabara yenye urefu wa
kilometa 128 kwa kiwango cha lami kutoka Mpanda hadi
Karema mwambao mwa ziwa
Tanganyika Mkoani Katavi .
Aliongeza kuwa barabara hiyo ni
muhimu sana kwaajiri ya kusafirisha
mizigo kwenda nchi ya Demokrasia ya
Kongo kupitia bandari inayojengwa
karema kwani lengo la
Serikali ni kutaka kusafirishia
mizigo kupitia bandari ya
karema kwenda kwenye
miji ya Momba na
Karemii nchini Kongo .
Pia
alisema serikali imepanga kuanzisha safari za
ndege katika uwanja wa
ndege wa Mpanda ifikapo
mwezi desemba mwaka
huu baada ya Wizara ya
ujenzi na uchuzi na mawasiliano
kuagiza magari sita
ya zima moto
ambapo moja litapelekwa uwanja wa
ndege wa Mpanda na safari
za ndege kutoka Dares
salaam hadi Mpanda
kwani tatizo lilikuwa
likisababisha kutokuwepo safari za
ndege ilikuwa ni uwanja wa Mpanda kutokuwa na
gari ya zima moto .
Alisema kuanza
kwa safari za ndege
kutasaidia watalii
kuongezeka katika hifadhi ya
Katavi kwani walikuwa wanashindwa kwenda
kwa wingi kutokana na kutokuwepo kwa usafiri wa
ndege.
Naye Meneja wa TANROADS mkoa wa Katavi
muhandisi Martin Mwakabenda
alisema kuwa kumekuwepo na changamoto
mbalimbali kwenye ujenzi wa barabara ya kutoka Mpanda
kwenda mkoani Tabora yenye
urefu wa Zaidi ya kilometa
340 inayotarajiwa kukamilika
baada ya miezi
36.
Alitaja
baadhi ya changamoto kuwa ni
wizi wa mafuta unaofanywa
na watumishi wasio
waaminifu wa vibarua wanaoshirikiana na
wananchi wanaoishi jirani
na Kambi za
ujenzi wa barabara .
Mmoja wa wakazi wa
Kijiji cha Inyonga John Samoja alimweleza Waziri Kamlwelwe kuwa wamekuwa
wakipata tabu sana kutokana na vumbi kwenye maeneo
wanayoishi hivyo wanaomba
wakandarasi wawe watii agizo la waziri siku zote na si tu kumwagia maji pindi
wanapo sikia waziri anafanya ziara ya kukagua barabara wanazo jenga.
MWISHO
No comments:
Post a Comment