Nkasi
Agizo
hilo alilitoa jana katika baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya
ya Nkasi baada ya kumebaini kuwa viongozi hao walikua wanalifahamu tukio
hilo na wakakaa kimya bila kuchukua hatua yoyote kutokana na uzembe
huo wanatakiwa kuchukuliwa hatua.
Alisema
kuwa wao wamefanya uchunguzi na kubaini kuwa mwalimu mkuu huyo amekuwa
na tabia hiyo ya kuwapa mimba Wanafunzi ambapo mpaka sasa wanafunzi
watatu wamezalishwa na mwalimu huyo huku wao wakikaa kimya pasipo
kuchukua hatua zozote na kuwa na wao wanaingia moja kwa moja katika
adhabu.
Mkuu
huyo wa wilaya alisema kuwa inashangaza kuona jambo kama hilo
linafanywa na mwalimu mkuu wakati wao wanafahamu vita vilivyopo sasa
katika wilaya Nkasi ya kupambana na mimba kwa Wanafunzi na viongozi wa
maeneo hayo wanakaa kimya na kuwa sasa ni lazima Watendaji hao wawe
mfano ili na waweze kujifunza namna ya kuchukua hatua za haraka pale
wanapoona mambo hayaendi sawa
“kama
viongozi hao wa vijiji na kata wangechukua hatua za haraka mwalimu mkuu
huyo angekamatwa na asingepata nafasi ya kutoroka na watendaji wa namna
hiyo hawatakiwi katika serikali ya awamu hii ya tano.
Sambamba
na hilo aliwataka madiwani kuendelea kuisimamia halmashauri yao vizuri
na kuwa mpaka sasa wilaya ipo vizuri hasa kwa kufanya vizuri katika
makusanyo na kuongoza katika halmshauri zote nne za mkoa wa Rukwa
ambapo makusanyoi ya ndani yamefikia asilimia 89.97 kiwango ambacho ni
kikubwa.
Aliwataka
madiwani kuyasimamia mapato hayo vizuri ili kuona kuwa zinarudi kwa
wananchi kwa kusaidia nguvu za Wananchi katika miradi mbalimbali ya
maendeleo waliyoianzisha ili waone kuwa makusanyo yao yanawasaidia ili
waweze kutoa mchango zaidi wa kuhakikisha kuwa halmashauri inakusanya
zaidi na kuwa walinzi kwa wale wanaotorosha mapato.
Kwa
upande wake mwenyekiti wa halmashauri hiyo Zeno Mwanakulya aliahidi
kuendelea kuisimamia halmashashauri vizuri na kuwa maagizo yote ya
serikali watayatekeleza.
Naye
mkurugenzi wa wilaya hiyo Missana Kwangula alisema kuwa wao kama
halmashasuri wataendelea kusimamia misingi ya kiutumishi na kusimamiana
ili kila mmoja aweze kutimiza wajibu wake kwa kutoa huduma bora kwa
Wananchi
Mwisho
No comments:
Post a Comment