Na Gurian Adolf
Nkasi
IMEELEZWA vitendo vya kupeana mimba baina ya wanafunzi kwa
wanafunzi vimeshika kasi katika wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa hali inayochangia
kukwamisha jitihada za kukabiliana na mimba za utotoni wilayani humo.
Hayo yalielezwa jana na hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya
hiyo Ramadhan Rugemalila wakati akitoa mada katika mkutano wa siku moja wa
kupitia utekelezaji wa mpango kazi wa kuanzia mradi wa kuzuia mimba za utotoni
unaofadhiriwa na shirika la kimataifa la Plan International wa mwezi Januari hadi Juni na kuandaa mpango
kazi wa mwezi Julai hadi mwezi Desemba mwaka huu.
Alisema kuwa kutokana na elimu inayotolewa kwa wananchi
pamoja na adhabu kali za kisheria zinazotolewa hivi sasa vitendo vya watu
wazima kuwapa mimba watoto wa kike vimepungua badala yake vimeibuka vitendo vya
kupeana mimba wanafunzi kwa wananfunzi.
Rugemalila alisema kuwa hivi sasa mahakani zimejaa kesi za
mimba kwa wanafunzi ambazo idadi kubwa ni wanafunzi wamekuwa wakipeana mimba
hali ambayo inalazimu sasa mashirika ya kutoa elimu yaelekeze nguvu mashuleni
huenda mashirika yaliyopo yalijikita kutoa elimu kwa watu wazima na wakawasahau
wanafunzi.
Hakimu huyo mfawidhi alisema kuwa pia changamoto nyingine
iliyopo ni sheria inayotoa adhabu kwa mwanafunzi anayempa mwanafunzi wa kike
ujauzito kwani haitoi adhabu kali
isipokuwa inaelekeza kupelekwa katika magereza maalumu ya watoto ambako
anakwenda kuendelea na masomo hivyo kitendo hicho kinasababisha baadhi yao kuto
ogopa wakati mwanafunzi wa kike anapoteza fursa ya masomo.
Alisema kuwa pia ipo chanagamoto kwa baadhi ya kesi kukosa
ushahidi wa kutosha kuwatia hatiani watuhumiwa ama baadhi ya mashahidi wakiwemo
waadhirika wa mimba za utotoni kutofika mahakamani hali inayosababisha baadhi
ya kesi kufutwa na watuhumiwa kuachiwa huru kitendo kinachosababisha wananchi
kuvitupia lawama vyombo vya sharia kuwa havitendi haki.
Kwaupande wake mratibu wa mradi wa kuzuia mimba za utotoni
wilayani Nkasi Frank Nestory alisema kuwa tangu mradi huo ulipoanza kutekeleza
wilayani humo kumekuwa na madiliko chanya kitendo kinachoonesha jamii hiyo
ilikosa elimu.
Alisema kuwa wapo baadhi ya wazazi walikuwa hawatambui kuwa
kumuozesha mtoto wake mdogo wa kike ni kosa kisheria kwani mlolo
huyo ni wakwake kwahiyo hakuna mtu anayeweza kumzuia kufanya hivyo mradi aamue
yeye mwenye mtoto.
Nestory alisema kuwa ni mtumaini yake mpaka mradi huo
utakapokuwa umefikia mwisho suala la mimba kwa watoto wilayani Nkasi litabaki
historia kutokana na elimu wanayoitoa sambamba na nmwitikio wa wananchi katika
kuunga mkono jitihada za kutokomeza ndoa za utotoni pamoja na mimba.
Mwisho
No comments:
Post a Comment