Saturday 10 March 2018

RC awaijia juu watendaji


Na Gurian Adolf
Sumbawanga
MKUU wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo amewaijia juu watendaji wa serikali mkoani humo kutokana na kuwa na tabia ya kuwasilisha takwimu zisizo na mabadiriko katika vikao mbalimbali kwani kitendo hicho kinaonekasha ni wavivu wa kutekeleza majukumu yao.
Akizungumza katika kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa huo hivi karibuni, Wangabo alisema kuwa tangu amefika amekuwa akipewa taarifa ambazo takwimu zake hazibadiriki kwa kuonekana kupungua ama kuongezeka kwa jambo wanalowasilisha.
Alisema kuwa alipopangiwa teuliwa kuwa mkuu wa mkoa huo na kupangiwa kazi aliongoza kikao cha kwanza cha RCC na alielezwa kuwa katika mkoa huo kunachangamoto kubwa ya mimba kwa wanafunzi ambapo taarifa hiyo ilieleza katika kipindi cha Januari mpaka Juni mwaka jana kuna wanafunzi 325 waliopata ujauzito na hakuna hata mtuhumiwa mmoja aliyehukumiwa kwa kosa hilo.
Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa taarifa hiyo ilieleza kuwa katika kipindi cha juni mpaka desemba mwaka jana takwimu zilionesha kuwa bado idadi ya wanafunzi waliopata ujauzito iko vilevile hakuna ongezeko wala kupungua.
Wangabo alisema kuwa hivi sasa taarifa iliyotolewa katika kipindi cha januari mpaka mwezi machi mwaka huu inaonesha kuwa kunamimba kwa wanafunzi wa shule za msingi 37 na sekondari 288 ambapo jumla yake ni 325 ambapo hakuna tofauti yoyote tangu alipoanza kupewa taarifa ya suala hilo.
Alisema kuwa kinacho onekana watendaji wa mkoa huo wamekuwa wakinakiri taarifa ileile na kuiwasilisha katika vikao bila kufanyia marekebisho hali inayoonesha ni uvivu katika utekelezaji wa majukumu yao.
Mwenyekiti huyo wa RCC alisema kuwa yeye binafsi amefanya jitihada za kutosha kutoa elimu kuhusiana na suala la mimba lakini takwimu hazibadiriki hali inayosababisha agundue kuwa kunauzembe katika kuwajibika kwa watendaji hao.
Katika kikao hicho baadhi ya wajumbe walishangazwa mkoa huo kuwa na viwanda 901 lakini bado wananchi wake ni masikini kitu ambacho walisema kuwa nilazima wajitafakari kwakuwa haiwezekani mkoa kama warukwa kuwa na viwanda vyote hivyo lakini wananchi ni masikini.
Mwanasiasa mkongwa Chrisant Mzindakaya alisema kuwa lengo la serikali kujikita katika uchumi wa viwanda ni zuri na lina nia ya kuwakomboa wananchi kutoka katika umasikini lakini changamoto ni watendaji wa serikali ambao wamekuwa ni mabingwa wa kuzungumza bila vitendo.
Alisema kuwa mkoa huo umekuwa na mikakati mingi mizuri kwa miaka mingi lakini tatizo ni namna ya kuitafsiri mikakati hiyo katika vitendo ili iweze kufanikiwa na wanachi wa mkoa huo waweze kupiga hatua na kuwa na maisha bora.
Pia alisema kuwa jitihada zifanyike za kushawishi wawekezaji wawekeze viwanda vikubwa ambavyo vitatoa ajira nyingi kwa wakazi wa mkoa huo tofauti na hivi sasa viwanda vilivyo vingi ni vyerehani ambavyo vinaajiri mtu mmoja ndiyo maana pamoja na kusema kuwa mkoa wa Rukwa unaidadi kubwa ya viwanda lakini bado wananchi wake ni masikini na wanakabiliwa na tatizo la ajira.
Mwisho

No comments:

Post a Comment