Tuesday 25 April 2017

Wazazi waja juu baada ya watoto wao kufungiwa kutwa nzima katika ofisi ya mtendaji wa kijiji

Gurian  Adolf
Sumbawanga

BAADHI ya wazazi katika mji wa Matai wilayani Kalambo mkoani Rukwa  wamelalamikia kitendo cha mtendaji wa kijiji hicho  Ester  Mwashambwa kuwakamata watoto wao ambao ni  wanafunzi wa shule ya msingi  Matai A na kisha kuwafungia katika ofisi yake kwa zaidi ya masaa 10 bila kula wala kunywa kwa madai kuwa anafanya hivyo ili wazazi wao wafike kulipa faini kwa kosa la watoto hao kuto kwenda shuleni.

Akizungumza na rukwakwanza.blogspot.com i kwa niaba ya wazazi wengine mmoja wa wazazi hao Mulele Mulenga alisema kuwa tukio hilo lilitokea jana ambapo afisa mtendaji huyo akishirikiana na mwenyekiti wa kijiji Nikasi Kamande waliwakamata watoto wao na kisha kuwafungia katika ofisi ya kijiji kwa madai kuwa hawaendi shuleni na iwapo mzazi alifika kumkomboa mtoto wake alipaswa alipe faini ya shilingi 10,000 ili aachiwe mtoto wake.

Alisema kuwa mtendaji wa kijiji  wakishirikiana na mwenyekiti wa kijiji pamoja na mgambo wa kijiji hicho waliendesha operesheni ya kuwakamata wanafunzi ambao walikuwa na sare za shule lakini waliwakuta mitaani na kisha kuwafungia katika ofisi ya kijiji kwa madai kuwa hawajaenda shule na shule yao ilikuwa imefunguliwa siku hiyo ya jumatatu baada ya likizo ya mapumziko ya pasaka.

Mulenga ambaye alikuwa akizungumza kwanjia ya simu  na mwandishi wa rukwakwanza.blogspot.com alisema kuwa siku ya tukio hilo yeye alimuacha nyumbani mtoto aitwaye Tumain Mlele(9) ambaye ni mtoto wa kaka yake akiwa anajiandaa kwaajili ya kwenda shule kisha yeye akaenda shambani.
Alisema kuwa aliporudi jioni kutoka shambani aliambiwa kuwa Tumaini amekatwa pamoja na wanafunzi wengine na wamefungiwa katika ofisi ya mtendaji kwa kosa la kuto kwenda shule ambapo alikwenda katika ofisi hiyo ya kijiji na alifika ilikuwa majira ya saa 2;08 za usiku ambapo alimkuta mtoto huyo akiwa na wanafunzi wengine wanne ambao walikuwa hawajakombolewa na aliwakuta wazazi wao wakibembeleza kupunguziwa faini ili walipe wawachukue watoto wao.
Mulenga alisema kuwa baada  ya kumuona mtoto wake huyo alijisikia uchungu sana kwakuwa alikuwa hajala chakula kutwa nzima huku watoto hao wakiwa wamejisaidia katika ofisi hiyo ya mtendaji ambapo alichukia na kuanza kumfokea mtendaji huyo hali ambayo iliibua zogo baina yao.
‘’Ndugu mwandishi kwakweli roho iliniuma sana baada ya kuona watoto wetu wakiwa wamefungiwa katika ofisi ya mtendaji wa kijiji na wakiwa wamejisaidia haja ndogo humo humo kama nguruwe wako zizini nilitamani nirushe ngumi lakini nikaona ntakua nimevunja sheria’’…alisema  Mulenga
Baada ya mwandishi kumsikiliza mzazi huyo alimtafuta Afisa mtendaji mwashambwa kwa njia ya simu alikata simu na alipo muandikia ujumbe mfupi  na kujitambulisha na kutaka ufafanuzi kuhusiana na malalamiko hayo ujumbe huo ujumbe ulimfikia lakini haukujibiwa na baada hapo simu hiyo ikazimwa na hakupatikana tena.
Hata hivyo mwandishi wa habari hii alimtafuta afisa mtendaji wa kata ya Matai B, Mozes Nkinda ili aweze kujua pengine mwenyekiti wa kijiji hicho alikuwa akitekeleza sheria walizojiwekea katika kata yao kupitia kikao cha maendeleo ya kata WODC simu yake iliitwa lakini ikakatwa na alipomwandikia ujumbe  naye simu yake haikuweza kupatikana tena.
Kutokana na hali hiyo ndipo alipotafuta mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Nkasi Simoni Ngagani na baada ya kumpigia simu ilikatwa ndipo  alipo mwandikia ujumbe huu
".Mkurugenzi habari za kazi! Pole na majukumu. Samahani Mimi ni mwandishi wa habari naitwa Gurian Adolf nimekupigia simu naona haijapokelewa. Samahani nia yangu ni kutaka ufafanuzi kutoka  kwako  maana Jana nilipokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Matai walalamikia kitendo cha Mtendaji wa kijiji cha Matai (B) Ester Mwashambwa kuwafungia watoto wao ambao ni wanafunzi wa shule ya msingi Matai B, akishirikiana na Mwenyekiti wa kijiji hicho Nikasi Kamande waliwafungia ofisini kwake kutwa nzima  bila kula chakula kwamadai kuwa anawashikilia kwa kosa la  kutokwenda shule ili wazazi wao wafike walipe faini ya sh 10,000 ndipo  awaachie'' hakujibu kitu.
 Nimempigia simu Mtendaji huyo hakupokea, nikamuandikia ujumbe mfupi kutaka kujua alikua anatekeleza hilo kupitia sheria gani, meseji ilipoingia amezima na simu. Sasa nimeona niwasiliane na wewe mwenye  Halmashauri huenda nikapata ufafanuzi zaidi. Ni hilo tu. Kazi njema". hakujibu kile mwandishi wa habari alichomwandikia.
Hata  huyo  alizungumza na katibu Tawala wa Wilaya hiyo Frank Sichalwe alikiri kupata taarifa za tukio hilo lakini alisema kuwa bado anasubiri taarifa kamili kutoka kwa watendaji wa halmashauri hiyo ili aweze kufahamu kwa undani nini  hasa  kilitokea na hatua gani ziweze kuchukuliwa kufuatia tukio hilo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment