Walter Mguluchuma
Katavi.
Mwenyekiti wa CCM
wa Tawi la
Itenka Kata ya Itenka B Tarafa
ya Nsimbo Wilayani
Mpanda Mkoani Katavi
Hapiam Salvatory(50)
ameuwawai kwa kukatwa kaatwa na
mapanga katika sehemu
mbalimbali za mwili wake na kichwa kutenganishwa na kiwili wili cha mwili wake.
Kwa mujibu wa Kamanda wa
Jeshi la Polisi wa
Mkoa wa Katavi Damas
Nyanda aliwaeleza wandishi wa
Habari kuwa tukio hilo la mauaji lilitokea April 24
majira ya saa saba mchana.
Alisema kuwa
siku hiyo ya tukio Hapiam
aliaga nyumbani kwake kuwa anakwenda
mtoni kwenye shughuli
zake alizokuwa akifanya kila
siku za kuvua samaki kwenye mto Itenka uliopo
Kijijini hapo.
Wakati akiwa njiani kuelekea mtoni alivamiwa na watu ambao walikuwa na mapanga
na kumkatakata katika sehemu mbalimbali za mwili wake
na kuutenganisha kiwili wili na
kichwa hadi kufariki Dunia hapo hapo.
Wananchi wawili ambao wakuwa wakipita kwenye
eneo hilo waliuona mwili huo
ndipo walipokwenda kutoa taarifa kwa
uongozi wa Kijiji ambao nao walitoa taarifa
kwa jeshi la Polisi,
ambalo lilifika kwenye eneo hilo
huku wakiongozwa na yeye Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi na
walikuta mwili wa marehemu huyo ukiwa umelazwa barabarani..
Alieleza kuwa
katika tukio hilo
watu watatu wanashikiliwa na jeshi la
Polisi kwa tuhuma za mauaji hayo.
Kamanda Nyanda
ametoa wito kwa wananchi wa
Mkoa wa Katavi
kuacha tabia ya kujichukulia sheria
mikononi kwani kufanya hivyo ni
kosa kisheria.
mwisho
No comments:
Post a Comment