Gurian Adolf
Sumbawanga
Waziri
wa Nchi anayeshughulia masuala ya Muungano na Mazingira Mhe. January
Makamba, amesema kuwa changamoto za Muungano wa iliyokuwa Tanganyika na
Zanzibar zimetatuliwa kwa kiasi kikubwa kutoka 15 mwaka 2006 hadi
kufikia changamoto 3 kwaka huu 2017, Muungano umetimiza miaka 53.
Waziri
Makamba amezungumza hayo leo Mjini Dodoma alipokuwa katika mkutano na
waandishi wa habari ulioandaliwa na waratibu wa sherehe za kitaifa Ofisi
ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi Vijana Ajira na Walemavu na kusimamiwa
na Waziri Mwenye dhamana Mhe Jenista Mhagama.
Picha hii ilipigwa tarehe na mwezi kama wa leo 26/4 miaka 53 ilyopita ambapo hayati baba wa taifa Mwl Julisu K. Nyerere alipokuwa akichanganya mchanga kutoka nchi ya Tanganyika na nchi ya Zanzibar kisha ikazaliwa nchi ya Tanzania.
Picha hii ilipigwa tarehe na mwezi kama wa leo 26/4 miaka 53 ilyopita ambapo hayati baba wa taifa Mwl Julisu K. Nyerere alipokuwa akichanganya mchanga kutoka nchi ya Tanganyika na nchi ya Zanzibar kisha ikazaliwa nchi ya Tanzania.
Mhe.
Makamba amezitaja changamoto zilizobakia kuwa ni pamoja na usajili wa
vyombo vya moto unaorahisisha kusafirisha magari kutoka Zanzibar kwenda
Bara na kutoka Bara kwenda Zanzibar na kusema kuwa swala hili
linafanyiwa kazi kwa kumalizwa kwa taratibu za kisheria.
Alisema
kuwa changamoto nyingine inahusu Hisa za Zanzibar kwa iliyokuwa bodi ya
safari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Pamoja na Mapendekezo ya tume ya
Pamoja ya fedha.
Awali
akizungumzia Muungano huo unaotimiza miaka 53, Waziri Makamba Alisema
kuwa umekuwepo kisheria na umerasimisha udugu na ushirikiano uliyokuwepo
kati ya Bara na Visiwani.
Hiyo hapo juu ndiyo kauli mbiu ya maadhimisho ya muungano kwa mwaka huu ambapo maadhimisho hayo yataongozwa na amiri jeshi mkuu wa vikosi vya ulinzi na usalama wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli na sherehe hizo zinaadhimishwa kitaifa mkoani Dodoma.
rukwakwanza.blogspot.com
inautakia kheri fanaka na maisha marefu muungano wa zikizokuwa nchi
hizi mbili yaani Tanganyika na Zanzibar na kuzaliwa kwa Tanzania miaka
53 ikiyopita.
Hakika
ni muda mrefu ambao hata mataifa mengi makubwa na tajiri,yenye nguvu
za kiuchumi na kijeshi yameshindwa lakini sisi tunaweza.
Tuendelee
kuwa pamoja na viongozi wetu waendelee kuuenzi, tuwapuuze watu wachache
wasioutaka muungano wetu inawezekana kwa maslahi yao wenyewe na si ya
wanamuungano huu.
kwani hivi sasa dunia inafikiria katika kuungana ndipo nguvu inakuwa kubwa kwa kila jambo.
Mfano
hata wafanyabiashara wakubwa na wadogo wanashauriwa kuungana kwa
kitendo hicho huwawezesha kuwa na nguvu zaidi ya kimtaji na kuweza
kufanya makubwa zaidi.
Lakini hata maneno na methali zetu zimekuwa zikituasa "umoja ni nguvu" popote palipo umoja inamaana kuna muungano.
Katika
kila muungano changamoto huwa hazikosekani, na iwapo walioungana
wakikosa changamoto basi ujue yupo ambaye anavumilia tu ama amekubali
kuumia ili amfurahishe mmoja kati ya hao wawili.
Nitashangaa
sana kama changamoto zitamalizika kwa kuwa zinaweza tatuliwa zilizopo
lakini mbele ya safari zikaibuka nyingine kutokana na wakati, mazingira,
maslahi na kizazi.
Kubwa
zaidi ni sisi watanzania kutafuta namna bora ya kuzitatua changamoto
husika kila zinapotokea, kuliko kufikiria kutengana.
Hakika hili ni tunu ambalo waasisi wetu wametuachia na hatunabudi kuuenzi lakini tukitatua changamoto zinazoibuka.
rukwakwanza.blogspot.com inautakia maisha marefu muungano wetu Leo na kwa vizazi vijavyo kwani bado faida za kuungana ni kubwa kuliko kutengana.
Kila lakheri muungano wetu.
No comments:
Post a Comment