Thursday 27 April 2017

Wauza pembejeo za kilimo Rukwa waonywa kutouza pembejeo za bandia

Gurian  Adolf
Sumbawanga

WAUZAJI wa pembejeo za kilimo mkoani Rukwa wameonywa kuacha kufanya mzaha wa kuuza pembejeo bandia kwani athari zake ni kubwa na zinaathiri uchumi wa mkulima mmoja mmoja mpaka taifa kwa ujumla.

Onyo  hilo limetolewa  na Mkuu wa mkoa huo Zelote Steven wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa wauza pembejeo za kilimo katika mkoa huo yaliyo fadhiliwa na shirika la  maendeleo la  Uholanzi SNV ambayo yanalengo la  kuwajengea uwezo ili waweze kuuza pembejeo ambazo  ni sahahi ili kuepusha hasara kwa wakulima.
  Mkuu wa mkoa wa Rukwa Zelote Steven akihutubia wauza pembejeo za kilimo wanao hudhuria mafunzo ya siku tatu katika ukumbi wa mikutano uliopo katika ukumbi wa jengo la ofisi ya mkuu wa mkoa

Alisema kuwa hivi sasa si wakati kwa wafanyabiashara ya pembejeo kufanya mzaha katika biashara hiyo kwani kitendo cha kuuza pembejeo bandia kimekua kikisababisha hasara kwa wakulima na hivyo  inabidi kikemewe kwa nguvu zote.

Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa imefika  wakati suala hilo lazima limalizwe kabisa mkoani Rukwa kwani mkoa huo umekuwa ukitegemewa kuzalisha chakula  kwaajili ya taifa  na iwapo suala hilo likifumbiwa macho ni kulitia  hasara taifa. 

Aliziagiza mamlaka zinazohusika katika kudhibiti ubora wa pembejeo hizo katika mkoa wa Rukwa kuhakikisha zinawajibika ili kuondoa pembejeo hizo kwani wafanyabiashara hao wakiachwa wafanye wanavyotaka watasababisha hasara kubwa.
Wauza pembejeo za kilimo kutoka katika wilaya zote za mkoa wa Rukwa wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Rukwa Zelole Steven wakati akifungua mafunzo ya siku tatu yenye lengo la kuwajengea uwezo ili waepuke kuuza pembejeo za kilimo  za bandia mkoani humo.

Hata hivyo  alisema kuwa serikali ya awamu ya tano  inatilia mkazo katika suala la  viwanda hivyo  kama uzalishaji wa mazao utaathiriwa na wauza pembejeo kwa kuwauzia wakulima pembejeo bandia viwanda hivyo  havitapata malighafi za kuzalisha bidhaa hivyo  suala la  kuongeza  thamani litashindikana kwakua wakulima hawatazalisha kwa tija. 

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi miradi ya shirika hilo, meneja mradi wa SNV Robert Kessy  alisema kuwa shirika hilo lilianza shughuli zake katika mkoa huo tangu  mwaka  2015.

Alisema kuwa shirika hilo linajikita katika Miradi ya kilimo, Maji na nishati ambapo linawajengea uwezo wananchi ili waweze kufanya vizuri katika uzalishaji katika sekta ya kilimo, kuhifadhi Maji na kutunza nishati ili iweze kuwe endelevu.

Mwisho

No comments:

Post a Comment