Wednesday 26 April 2017

Wahubiri wa Injili Rukwa lawamani kwa kukwamisha jitihada za matumizi ya dawa za ARV

Gurian  Adolf
Sumbawanga

KATIBU tawala wa mkoa wa Rukwa Tikson Nzunda amewalaumu  baadhi ya wahubiri wa Injili mkoani humo  ambao wanahubiri huku wakiwaacha waumini wao wakiamini kuwa wanauwezo wa kuponya ukimwi kwa maombezi.

Katibu  tawala huyo aliwalaumu wahubiri hao wa neno la  Mungu kwa kupitia barua yake  aliyoviandikia vyombo vya habari vilivyopo mkoani humo kuwaambia wahubiri hao waache kuhubiri habari hizo kwani zinapingana na jitihada za kukabiliana na ugonjwa huo na ni upotoshaji mkubwa.

           Aliye katikati na amevaa miwani ndiye Tixson Nzunda katibu tawala mkoa wa Rukwa
Katika barua yake  Nzunda aliviandikia vyombo vya habari kuwaeleza wahubiri hao kutafuta namna  nyingine ya kuhubiri lakini kwa kutumia baadhi ya watu wanaowaombea kushuhudia kuwa wamepona virus vya ukimwi kunasababisha baadhi yao ambao walikuwa wanatumia dawa  za ARV za kufubaza virusi hivyo kuacha kutumia wakiamini kuwa wamepona.

Alieleza kuwa kitendo hicho kinakinzana na jitihada za serikali katika kuwahudumia watu wanaotumia dawa za ARV kwani baadhi yao huamua kuacha kutumia dawa hizo wakiamini kuwa wamepona kupitia maombi ya wahubiri hao wa injili.

Katibu  tawala Nzunda aliwataka kuhubiri neno la  Mungu  kuacha upotoshaji huo wanauwezo wa kuombea watu wakapona virusi vya ukimwi kwani kitendo hicho kinapelekea watu wanaotumia dawa  hizo kuacha kutumia.

Kutokana na mahubiri  pamoja na maombezi hayo baadhi ya watu wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kwaajili ya kuombewa shida na magonjwa mbalimbali ikiwemo virusi vya ukimwi.

Hata  hivyo  hivi sasa mkoani humo kumekuwa na wahubiri wakiombea watu Wenye shida na magonjwa na kisha kutumia redio zilizopo mkoani humo kuhubiri na kuwahoji ili washuhudie kuwa wamepona magonjwa mbalimbali ikiwemo virusi vya ukimwi.
Mwisho

No comments:

Post a Comment