Sumbawanga
NDUGU
wa marehemu Juma Dereva(38) jana walisusia kuchukua maiti ya ndugu yao huyo
kwa Madai kuwa wanaamini kuwa kifo chake kimetokana na kipigo kutoka
kwa Askari polisi wa kituo cha Mpui wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa.
Akizungumza
na rukwakwanza.blogspot.com mmoja wa ndugu hao Daniel Mohammed mkazi wa kijiji cha
Malolwa wilayani humo alisema kuwa wao wamesusia kuchukua mwili wa
marehemu wakidai kuwa wanataka uchunguzi wa kitabibu ufanyike kwakua
kifo cha ndugu yao huyo kilikuwa ni cha ghafla na alikua haumwi.
Alisema
kuwa tukio la kifo hicho lilitokea April 26 majira ya saa 9 za mchana
kwani ndugu yao huyo ambaye yeye ni baba yake mdogo alitoka nyumbani
kwake na kuwapelekea chakula mtoto wake aitwaye Loyce Mohammed pamoja
na mume wake Leonard Kaembe waliokuwa wanashikiliwa na polisi katika
kituo hicho cha Mpui.
Alisema
kuwa wanandoa hao walikuwa na ugomvi baina yao ambapo jirani yao
aliyefahamika kwa jina moja la Melkio akiwa na mtoto wake Lazaro Melkio
walikwenda kuwaamua na kisha wanandoa hao waliacha kupigana wakaanza
kumpia Mzee Melkio hadi kumvunja mguu.
Baada
ya kumvunja mguu alikwenda polisi na kupewa PF3 na kisha kwanza
kupatiwa matibabu katika kituo cha afya cha Mpui kilichopo wilayani
humo.
Siku iliyofuata
Juma Dereva aliwapelekea chakula watuhumiwa na kwenda kuwawekea dhamana
ambapo alipelekwa na bodaboda mpaka kituo cha polisi.
Baada
ya saa nzima mmoja kati ya ndugu wa marehemu alipigiwa simu na
muendesha bodaboda akiwaarifu kuwa ndugu yao aliyempeleka katika kituo
cha polisi amefariki dunia.
Aliwaeleza
kuwa mtoto wa mzee Melkio aliyefunjwa mguu baada ya kumuona marehemu
akiwapelekea chakula watuhumiwa aliwafuata na kuwaeleza askari polisi
kuwa naye aliwlmtishia maisha hali iliyopelekea askali polisi kumkamata
na kumuingiza mahabusu.
Alisema
baada ya kumuingiza mahabusu alianguka chini na kufariki dunia ndipo
yeye alipoamua kuwapigia simu kuwaarifu ndugu zake kuwa Dereva amekufa.
Polisi
baada ya kuona ameanguka walimchukua na kumpeleka katika kituo cha afya
cha Mpui lakini mganga liyempokea aliwaambia kuwa amekwisha fariki
dunia.
Ndipo ndugu wa
marehemu huyo walipofika katika chumba cha kuhifadhia maiti wakiwa na
diwani wa Kata ya Mpwapwa Abel Msumbachika ambaye alisema kuwa mwili wa
marehemu ulikuwa na jeraha kichwani huku vishikizo vya shati vikiwa
vimekatika hali ambayo ilisababisha ndugu wa marehemu kupata mashaka
ndipo walipoamua kugoma kuchukua mwili huo wakidai kuwa wanataka
kwanza uchunguzi ufanyike.
Diwani
Msumbachika alisema kuwa kufuatia Madai hayo mwili wa marehemu
ulisafirishwa kupelekwa katika hospitali ya mkoa wa Rukwa ili uchunguzi
ukafanyike kwa lengo la kuweza kujua sababu hasa za kifo cha marehemu.
Kwaupande
wake kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoani Rukwa Polycarp Urio
alipozungumza na rukwakwanza.blogspot.com alikiri kuwepo kwa tukio la mtu kufa
lakini alisema kuwa bado uchunguzi unafanyika kuhusiana na tukio hilo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment