Thursday 24 December 2015

wananchi watakiwa kutoa taarifa za polisi waharifu

Na Gurian  Adolf                                                              
                                                                
JESHI la polisi mkoani Rukwa limetoa wito kwa wakazi wa mkoa huo
kutowafichia siri watendaji wa jeshi hilo pindi wanapokuwa wakifanya
vitendo ambavyo ni kinyume na maadili ya kazi yao ili waweze
kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo ni pamoja na kutimuliwa kazi.

Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai mkoani humo Allan Bukumbi
akizungumza na gazeti hili alisema kuwa huu ni wakati ambao si
wakulaumiana ila ni wakila mtu kuwajibika na hivyo kuwataka wananchi
kuacha kulalamika kuhusiana na mwenendo wa watendaji wa jeshi hilo ila
kutoa taarifa hatua ziweze kuchukuliwa.

Alisema baadhi ya wananchi wamekuwa wakilalamika bila kutoa taarifa
kwa viongozi wa jeshi hilo na kama wanaona kunaudhaifu kwa baadhi ya
askari polisi wanachopaswa kufanya ni kutoa taarifa ili hatua
zichukuliwe.

''tunaomba wananchi wasiogope watoe taarifa kwa viongozi wa polisi
kuhusiana na tabia mbaya za askari, wanaochukua rushwa na walevi ili
tuwawajibishe kwani sisi ndiyo tunapaswa kuwa mfano wa kuigwa lazima
tuwe waadilifu''  alisema Bukumbi.

Mkuu huyo wa upelelezi wa makosa ya jinai alisema jeshi la polisi
halipo tayari kuchafuliwa na watendaji wake wasiokuwa na maadili ni
bora wakatimuliwa kwani hawafai kuwa sehemu yao kwani sifa za kuwa
mtendaji wa jeshi hilo uadilifu na utii ni sifa za msingi za jeshi
hilo.

Aidha alitoa wito kwa wakazi wa mkoa huo kuwa makini katika sikukuu
hizi za Krismas na Mwaka mpya kwa kuwaangalia watoto ambao wamekuwa ni
waathirika wa vitendo vibaya kutokana na wazazi wao kuendekeza starehe
na kuwaacha watoto bila uangalizi wa kutosha.

Alisema nyakati hizi za sikukuu kumekuwa na matumizi ya vilevi kupita
kiasi hali ambayo inasababisha madereva na watembea kwa miguu kupoteza
utashi wawapo barabarani na hivyo kusababisha ajali ambazo zingeweza
kuepukika.

Mwisho

No comments:

Post a Comment