Thursday 24 December 2015

wananchi wajutia kuipa ardhi Serikali.

Na Gurian  Adolf

SERIKALI ya wilaya ya Mlele mkoani Katavi imesema kuwa  imeamua kufunga safari na kwenda kumuona waziri wa Afya ili waweze kupewa uhakika wizara yake itatoa fedha lini za kuwalipa fidia wananchi waliotoa ardhi yao ili iweze kujengwa hospitali ya wilaya hiyo kwani imekuwa ni muda mrefu hivi sasa.
Mkuu wa wilaya hiyo Issa Njiku aliwaambia wananchi wa wilaya hiyo wawe wavumilivu kwani baada ya muda mfupi watapewa majibu ambayo yatamaliza tatizo la muda mrefu la wao kudai fedha zao za fidia kutokana na kutoa ardhi ili ijengwe hospitali hiyo.

Alisema wananchi wamekuwa wakidai fedha zao ili waweze kulipwa na wanunue ardhi katika maeneo mengine ambapo wataweza kuendelea na shughuli za uzalishaji ikiwa ni pamoja na kilimo, ufugaji na ujenzi wa nyumba bora na  za kisasa.

Njiku alisema kuwa mara kadhaa serikali ya wilaya hiyo wamekuwa wakiwasiliana na watendaji wa wizara ya afya na kupewa majibu ambayo hayawaridhishi wananchi hivyo yeye, mkurugenzi wa halmashauri hiyo pamoja na mganga mkuu wa hospitali hiyo watafunga safari kwenda wiazara ili wakaelezwe ni lini fedha hizo zitakuwa tayari.

Alisema imefika wakati wananchi wameanza kupoteza imani na viongozi hao wa wilaya inaonekana kama hawalipi uzito suala lao na wao ndiyo wanaoishi na wananchi hao na hivyo lawama zote wanazibeba wao hivyo wanajisikia vibaya.

Mmoja wa wananchi wanaodai fidia Fransis  Mikidadi alisema kuwa wamechoka kuvumilia na hawaamini kuwa viongozi wao wanalifuatilia suala lao kwa umakini kwani lingekuwa limekwisha malizika kwani serikali haiwezi ikakosa fedha za kuwalipa deni lao.

Alisema wananchi hao wanaendelea kuchangishana fedha kwaajili ya naauri ili baada ya sikukuu ya mwaka mpya wafunge safari kwenda kuonana raisi John Magufuli ili aweze kuwasaidi wapatiwe fedha hizo ama ikibidi akiisoma habari hii katika gazeti la Nipashe awasaidie kwani wanateseka na wanazidi kuwa masikini kwa ujinga wa kutoa ardhi yao na kuipa serikali inayowasumbua.

mwisho

No comments:

Post a Comment