Na Gurian Adolf
Sumbawanga
HALI
ya ugonjwa wa kipindu pindu bado ni tete wilayani Sumbawanga mkoani
Rukwa ambapo idadi ya wagonjwa imeendelea kuongezeka ambapo hivi sasa
imefikia vifo 15 na wagonjwa 397 waliougua ugonjwa huo tangu ulipolipuka
tena Mei 6 mwaka huu.
Mganga
mkuu wa wilaya ya Sumbawanga Fani Mussa akizungumza na mwandishi wa
habari hizi amesema kuwa ugonjwa huo bado haujaisha na watu wamekuwa
wakiendelea kuugua.
Alisema
kuwa mpaka kufikia jana jumla ya watu 397 wameugua kufa na wengine
kupona ambapo mpaka hivi sasa kuna wagonjwa saba ambao bado wapo wodini
wakitibiwa ugonjwa huo.
Mganga
mkuu huyo alisema kuwa changamoto kubwa iliyopo ni wananchi kutofuata
kanuni bora za afya hasa kunywa maji yasiyosalama sambamba na
kutojisaidia kwenye vyoo.
Alisema
kuwa hivi sasa wakulima wanavuna mpunga na maji wanayotumia kwa kunywa
ni ya kwenye majaruba ambayo si salama kiafya kwakuwa hayajachemshwa na
baadhi yao wakijisaidia porini.
Dkt
Mussa alisema kuwa idara ya afya inajitahidi kutoa elimu lakini bado
wananchi hawafuati taratibu za kujikinga na ugonjwa huo licha ya kwamba
sheria kali pia zinatumika lakini bado ugonjwa huo unaendelea.
Alisema
katika kipindi cha November mwaka jana ugonjwa huo ulilipuka na
ulidhibitiwa ilipofika mwezi March mwaka huu lakini bila matarajio
ugonjwa huo ulilipuka tena mwezi mei mwaka huu na katika siku si nyingi
umeua watu 15 tofauti na mwaka jana ambapo watu 7 ndiyo waliopoteza
maisha.
Mwisho
No comments:
Post a Comment