Wednesday 14 March 2018

Wavuvi Rukwa walilia viwanda

Na Gurian Adolf
Kalambo

BAADHI ya wavuvi mkoani Rukwa wameiomba serikali kuiokoa sekta hiyo kwa kualika wawekezaji wakubwa ili wawekeze viwanda vya kusindika samaki hali itakayo saidia kuwa na soko la uhakika la samaki mkoani sambamba na kuifikisha nchi katika uchumi wa viwanda.
Wakizungumza na gazeti hili walisema kuwa hivi sasa sekta ya uvuvi mkoani humo inakabiliwa na hali ngumu baada ya serikali ya Zambia kupiga marufuku uvuvi katika ziwa Tanganyika sambamba na kuingiza samaki kutoka katika nchi jirani za Tanzania na Kongo kutokana na kipindupindu kwasababu mkoani humo hakuna viwanda vya kusindika mazao ya ziwani.
Mmoja wavuvi aliyepo katika kijiji cha Kasanga wilayani Kalambo mkoani Rukwa Skeva Sinyangwe alisema kuwa hivi sasa sekta ya uvuvi imekabiliwa na changamoto kutokana na kukosa soko la samaki ambapo kilogramu moja ya samaki wamekuwa wakiuza chini ya shilingi 1,000 kutoka shilingi 5,000 waliyokuwa wakiuza hapo awali.
Alisema kuwa wavuvi wa mkoani Rukwa walikuwa wakitegemea kuuza samaki wao nchini Zambia ambako kuna makampuni yapatayo 12 ambapo yalikuwa yakinunua mpaka tani 1,200 ambao walikuwa wakiuza katika makasha ya mbao yenye uzito wa kilogramu 30 kwa shilingi 125,000 lakini tangu nchi hiyo ikabiliwe na kipindupindu na kuzuia ununuaji wa samaki wababich bei imeporomoka.
Naye Frances Simzosha mkazi wa Kasanga alisema kuwa kwakuwa hivi sasa serikalin ya awamu ya tano imejikita katika uchumi wa viwanda ni vizuri sasa ikafungua milango na kuwaalika wawekezaji wakubwa waweze kufika mkoani Rukwa na kuwekeza katika viwanda vya kusindika samaki ambao wanaonekana kukosa soka hivi sasa.
Alisema kuwa nia ya serikali ya awamu ya tano ni kuona nchi inakwenda katika uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda sambamba na kupatikana kwa ajira hali ambayo fursa ipo kupitia sekta ya uvuvi katika ziwa hilo.
Simzosha alisema kuwa sambamba na hayo pia nchi itapata fedha nyingi kutokana na malipo ya kodi kitu ambacho raisi wa awamu ya tano John Magufuli anataka kukiona na inawezekana iwapo yakiandaliwa mazingira mazuri.
Aliiomba serikali kuitumia fursa hiyo vizuri  ya kuanzisha viwanda ambayo itawakwamua wavuvi katika lindi la umasikini,wananchi wanaohitaji ajira sambamba na kuongeza pato la serikali litakalo iwezesha kupata fedha za kuwahudumia wanchi wake.
Mwisho

No comments:

Post a Comment