Sunday 8 October 2017

Pinda aukwaa uenyekiti wa CCM wilaya

Na Walter Mguluchuma
Mlele
Chama  cha  Mapinduzi  CCM Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi kimemchagua  Walfugang  Mizengo  Pinda ambae ni mdogo wake na  Waziri  Mkuu Mstaafu  Mizengo  Peter Pinda kuwa mwenyekiti wachama hicho ambaye atakiongoza  kwa miaka mitano ijayo. 
 Uchaguzi huo ulifanyika juzi katika ukumbi wa  Chama  cha  Msingi cha wakulima Ukonongo ulipo Inyonga Wilayani  Mlele huku mgeni rasmi  katika mkutano huo alikuwa ni Waziri  mteule wa  Wzira ya  Maji mhandisi Izack Kamwelwe  ambae pia ni  Mbunge wa Jimbo la Katavi .
Awali Katika hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo wa  uchaguzi msimamizi wa uchaguzi aliwaasa wajumbe wa mkutano huo kujiepusha na kuwachagua viongozi watakao washawishi wawachangue baada ya kuwapatia rushwa.
Akitangaza  matokea  ya uchaguzi huo msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni Katibu  mwenezi wa  CCM  wa  Mkoa wa  Katavi Joseph Makumbule alisema  idadi ya wajumbe waliotakiwa kupiga kura walikuwa  541 ambao walikuwa wametoka  kwenye  Kata 15 za wilaya hiyo  lakini  waliohudhuria ni wajumbe 477.
Makumbule  alifafanua kuwa  wagombea walikuwa watatu  kwenye nafasi ya mwenyekiti  ambapo kura  zilizopigwa zilikuwa 477 ambapo kura moja iliharibika  na  matokeo yalikuwa ni  Gerald  Kasela  alipata kura 146  John  Mbogo  kura  110 na  Walfugang Mizengo Pinda kura 220.
Kwa  mujibu  wa   Kanuni  mshindi wa  nafasi  hiyo lazima  avuke  nusu ya kura  na hapo awali hakuna mgombea aliyefanikiwa kuvuka nusu ya kura zote hivyo ikawalazimu wajumbe wa mkutano huo wapige kura  kwa  mara ya pili kwa wagombea  wawili walipata kura za juu ambao ni  Gerald Kasela  na  Walfugang  Mizengo  Pinda.
 Ambapo katika uchaguzi huo wa marudio  kura  450  zilipigwa  ambapo  Gerald  Kasela alipata kura  156 huku  Walfugang  Mizengo  Pinda  alipata kura  280 na kura   8 ziliharibika  hivyo  msimamizi wa  uchaguzi  Joseph  Makumbule  alimtangaza  Walfugang  Mizengo  Pinda kuwa  ndio  mshindi wa   nafasi  hiyo   na   alimtangaza rasmi kuwa  Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mlele.
 Pia mkutano huo ulimchagua  Renatus Kamaninja kuwa  Katibu   Mwenezi wa  Wilaya baada ya kuwashinda wagombea wenzake watatu  na  Mkuu wa wilaya hiyo Rachael  Kasanda alichaguliwa kuwa   mjumbe wa   mkutano mkuu wa   CCM  Taifa   baada ya kuwashinda wagombea  tisa katika  nafasi hiyo.
Kwapande wa wilaya ya Mpanda , Abal   Hamis  Kimanzi   alichaguliwa  kuwa  Mwenyekiti wa  Wilaya  hiyo  baada ya kuwashinda  Method Mtepa  na  Wense   Kaputa waliogombea  nafasi  hiyo katika mkutano wa uchaguzi uliofanyika   kwenye uwanja wa  Mpira wa  Azimio  Mjini  humo.
Nafasi ya Katibu  Mwenezi wilayaniya  Mpanda  alichaguliwa   Elias   Milwano   ambaye  aliwashinda  wagombea  wawili waliokuwa  wameomba  nafasi  hiyo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment