Sunday 30 July 2017

Waonywa kutofanya ujangiri

Na Gurian Adolf
Katavi
ASKARI wa hifadhi za Taifa (TANAPA)  wameonywa kutojihusisha na vitendo vya ujangili kwani wakibainika kufanya hivyo hatua kari zitachukuliwa dhidi yao kwakua wao ndio wanandhamana kubwa ya kulinda hifadhi hizo. 
Mwenyekiti wa  bodi ya Wadhamini  ya  TANAPA  Mkuu wa  Majeshi  mstaafu   Meja jenerali    George   Waitara  alitoa onyo hilo jana  kwa askari wa   Hifadhi za Taifa  wakati  alipokuwa  akifunga  mafunzo ya   askari hao wapatao 153 wa kutoka   Tanapa  na   Hifadhi ya  Ngorongoro yaliofanyika  katika  kituo  cha   mafunzo   Mlele   Mkoani   Katavi  yenye   lengo la kuwaandaa    ki  utendaji  kazi wa kutoka  mfumo wa  sasa wa kiraia na  kuwa  mfumo wa  Jeshi usu.
Alisema  zipo taarifa  za kuwepo  baadhi ya  askari wa   hifadhi za  Taifa  na wa   mapori ya   akiba  wamekuwa   sio  waaminifu  na  wamekuwa wakifanya   shughuli za  ujangili  kwenye  mapori ya   akiba  na   kwenye  hifadhi za   Taifa kitu ambacho ni makosa makubwa. 
 Aliwataka  wale  wote  wenye  tabia  hiyo  waache  mara  moja  na watakao  bainika  wajue kuwa watachukuliwa  hatua  za  kinidhamu  na  kufikishwa   Mahakamani bila kujali cheo wala wadhifa wa mtu kwani jukumu walilonalo ni kulinda hifadhi hizo. 
Mwenyekiti  huyo wa  bodi ya Tanapa   alifafanua  kuwa   kamwe huwezi kuwa   wewe  ni   askari  unae  linda  maliasili  za   nchi  na  huku  ukiwa  ni   mhalifu  wa   maliasili   za  nchi  yetu na hautavumiliwa. 
 Alisema Tanzania  ilikuwa  imekubwa  na changamoto kubwa  ya  ujangili  wa kutumia  silaha za  moto  na  hasa  za  kivita  ila kutokana  na  mafunzo waliopata   askari  kwenye  kituo cha  Mlele ya mfumo wa  jeshi usu yamesaidia  sana kupunguza ujangili wa kuua   wanyama  kama  Tembo  na   Faru  hata  hivyo  sio  kwamba    ujangili  umeisha   kabisa.
  Pia   alisema   Hifadhi za   Taifa   na  mapori ya  akiba  pia   yanakabiliwa na   changamoto  ya uingizwaji  wa  mifugo ndani ya hifadhi hivyo ni  imani  yake kuwa kupitia  mafunzo   yanayotolewa  kwenye kituo cha  Mlele   askari wa   hifadhi za   Taifa  na   wa  mapori ya   akiba wahakikishe   hifadhi  zinakuwa  salama kabisa .
  Alieleza  kuwa  kazi  kubwa   iliyombele ya  Wizara ya  Maliasili na   Utalii ni kulinda  maliasili za   nchi  ili   vizazi   vijavyo  vikute   wanyama   kama   Tembo na   Faru ambao wako hatarini kutoweka kutokana na ujangili. 
Kaimu   Mkurugenzi  Mkuu  wa hifadhi za   Taifa   Mtango  Mtahiko  alisema   mafunzo  hayo  yatawasaidia  kuwaandaa  wahitimu  kwa kuwajengea   utimamu wa  mwili  na kuwapa mbinu  za kupambana  na  ujangili.
Pia  alisema mafunzo hayo yatawaongezea   ujasiri ,kujiamini  na  hari zaidi  katika  kulinda   rasilimali za   wanyama  pori  na   maliasili kwa   ujumla  na   mpaka   sasa  askari   830 wa   Tanapa  wameisha   patiwa  mafunzo kama    hayo   katika   kituo cha   Mlele  kati ya  askari   837 walipangiwa huhudhuria  mafunzo  hayo ya  mfumo wa  jeshi usu.
Mwakilishi wa   Muhifadhi   Mkuu wa  mamlaka  ya   Ngorongoro  Izraeli   Lamon   alisema  Hifadhi ya   Ngorongoro  inakabiliwa na   changamoto ya   wanyama  kuishi na   watu  ndani ya   hifadhi.
Mkuu wa    Hifadhi wa   kituo cha  Sanane    Abeli  Mtui  alisema   mafunzo  hayo   yatawafanya  wahitimu wafanye  kazi  kwa  uadilifu   mkubwa tofauti na awali. 
Mafunzo  hayo yanafanyika kwa mara ya 14 katika  kituo cha   Mlele   tokea   Wizara ya   Maliasili na   Utalii ilipotangaza  kubadili  mfumo  wake  wa  utendaji  kazi  kwa  watumishi waliochini ya   Wizara hiyo kwa kutoka  mfumo wa sasa   wa  utendaji kazi wa kiraia  na kuwa jeshi usu   PARAMILITARY  TRANSFORMATION
Mwisho

No comments:

Post a Comment