Friday 21 April 2017

Watakao kaidi kutumia mizani Rukwa,Katavi kutozwa milioni 100!

Gurian  Adolf
Sumbawanga

WAKARA wa vipimo  katika mikoa ya Rukwa na Katavi  umewatahadharisha wafanyabiashara mkoani humo kutumia vipimo vinavyotambulika  kisheria vinginevyo watakijuta wakikabiliwa na hukumu ya faini ya hadi shilingi milioni 100 au kwenda jela miaka mitano ama vyote kwa pamoja.

Akizungumza na rukwakwanza. Blogspot.com  meneja wa vipimo mkoani Rukwa na Katavi Abinery  Nzanga alisema kuwa ni lazima wafanyabiashara wote katika mikoa hiyo kuhakikisha wanatumia mizani na kueleza kuwa baadhi  kuzingatia uzito na si ukubwa wa magunia ambapo alitolea mfano  kwa magunia  Mkaa kg 30, mihogo  kg 60, mchele 100 maharage 100, mahindi kg 100mpunga kg 75  na ngano kg 90.  

Alisema kutokana na wafanyabiashara kutokuwa na utamaduni wa kutumia mizani umekuwa ukisababisha kutokuwa na usawa wakati biashara inapofanyika kwani mara nyingi wakulima wamekuwa wakidhurumika kwani wafanyabiashara wamekuwa wakipima bidhaa kwa wakulima kwa kutumia madebe lakini wao wanakwenda kuuza kwa kutumia mizani.

Nzunga alisema kuwa ili kutenda haki kwa makundi yote ni lazima kipimo cha mizani ambacho ndicho kinatambuliwa kisheria ndicho kinapaswa  kutumika tofauti na hivyo ni ukiukwaji wa sheria na wao hawatakubali kuona kundi moja likidhurumika.

Naye  Juma Chacha afisa vipimo wa wakara hiyo amesema kuwa hivi sasa wataendesha operesheni ili kuwakamata wafanyabiashara wanaokiuka sheria hiyo ili kukomesha biashara ambayo imekuwa ikifanyika bila kufuata sheria.

Kwaupande wao wafanyabiashara wa soko la Mandera mjini Sumbawanga walisema kuwa wao hawana tatizo na matumizi ya mizani kwani wakulima ndiyo wamekuwa wakigoma kutumia mizani kwakuwa hawajui kuisoma.

Walisema kuwa wakotayari kufuata matakwa ya sheria kwakuwa ndivyo inavyoelekeza ili kuepuka mkono wa shelia  kwakuwa nao wanachotaka haki itendeke pindi wanapo fanya biashara zao na kusiwepo wa kupata hasara.
mwisho

No comments:

Post a Comment