Monday 24 April 2017

Msichana adhalilishwa kwa kuchaniwa nguo hadharani,aachwa na nguo ya ndani

Na Gurian  Adolf
Sumbawanga.
 
MSICHANA mmoja mkazi wa mji wa Sumbawanga  amedhalilishwa na wapigadebe wa stendi kuu ya mjini Sumbawanga baada ya kumchania skerti aliyokuwa amevaa kwa madai kuwa wamechoshwa na vitendo vya baadhi ya wakina Dada ambao wamekuwa wakivaa sketi fupi kwa madai  kuwa siyo maadili ya kitanzania.
                   
Msichana huyo ambaye hakuweza kufahamika jina  lake Mara moja jana  alivuliwa nguo na wapiga debe wa stendi kuu baada ya kufika katika stendi hiyo ambayo haikufahamika Mara moja alikuwa amekwenda kufanya nini. 

 
                        Picha ya Msichana akiwa amedharirishwa  baada ya kuchaniwa nguo.
 
Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo Issa Daniel ambaye ni mfanyabiashara ndogondogo ya kuuza urembo katika stendi hiyo alisema kuwa akiwa amekaa katika kibanda chake ghafla alisikia kelele za watu na alipotoka nje aliwaona wapiga debe hao wakiwa na watu wengine wakimfukuza msichana huyo.

Baada ya kufanikiwa kumkamata walimchania sketi aliyokuwa amevaa wakidai kuwa wamechishwa na tabia  ya wanawake ambao wake kuwa wakifika katika stendi hiyo huku wakiwa wamevaa nguo fupi almaarufu kama mini sketi.

Baada ya tukio hilo baadhi ya wanawake walikuwa pembeni wakishuhudia tukio hilo walimchukua msichana huyo na kumwingiza kwenye chumba kimoja ambacho kipo  karibu na kampuni ya simu za mkononi ya Tigo ambapo walimpa kanga ili ajisetiri kufuatia tukio hilo.

Daniel alisema kutokana na kitendo hicho baadhi ya watu walilaani kitendo hicho na kuliomba jeshi la  polisi pamoja na vyombo vingine kuchukua hatua kufuatia tukio hilo.

"Hata  kama alikuwa  amevaa nguo fupi hawakupaswa kumfanyia vile kwani ule ni udhalilishaji wa hali ya juu wangemwambia lakini si  kumchania sketi yake  na kubaki na nguo ya ndani(chupi) kwakweli ni udhalilishaji wa hali ya juu"... Alisema.

Alisema baada ya tukio hilo aliwaona polisi wakiwa wamefika katika eneo la  stendi kuu ambapo walianza kuwasaka wahusika wa tukio hilo na aliomba iwapo watakamatwa wachukuliwe hatua kwani kitendo kile  kamwe hakiwezi kuvumilika katika jamii ya watu wastarabu.

Aidha kufuatia tukio hilo baadhi ya watu walipiga picha kwa kutumia simu zao za mkononi na kuchukua video kisha kuweka katika mitandao ya kijamii ikiwemo facebook na what's up ili watu waweze kuona kile  kilichotokea.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment