Sunday 24 May 2015

WANASIASA RUKWA WAONYWA

Na Gurian  Adolf
Sumbawanga

SERIKALI ya mkoa wa Rukwa imewaonya baadhi ya wananchi na wanasiasa kutodhubutu kuwaingiza watu nchini kinyume na sheria ili wajiandikishe katika daftari la kudumu la wapigakura kwa lengo wawapigie kura wakati wa uchaguzi mkuu ujao.

Onyo hilo alilitoa jana na mkuu wa mkoa wa Rukwa Stella Manyanya wakati Akizungumza na vyombo vya habari kuhusiana na mchakato wa kuanza uandikishaji katika daftari la kudumu la wapigakura kazi inayoanza leo  Mei  24.

Alisema kuwa wapo baadhi ya wanasiasa ambao wanaweza kushawishika kuwaingiza nchini kinyume na sheria na kujiandikisha katika daftari la wapigakura ili nao wajewashiri katika  uchaguzi mkuu.

‘’mkoa wetu upo mpakani…tunapakana na nchi za Zambia na Congo, hivyo basi ni kosa kisheria kuwaingiza watu nchini kinyume cha sheria pia vivyo hivyo ni kosa kisheria kwa mtu ambaye sio raia kujiandikisha katika daftari la kudumu hivyo nawaasa wananchi wajiepushe kuwaingiza watu nchini kinyume cha sheria’’…….alisema.

Alisema kuwa kutokana na zoezi hilo kuwa linaanza leo hivyo basi nivizuri kwa wakazi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi na kujiandikisha ili wapate fursa ya kuchagua viongozi wao katika uchaguzi mkuu.

Manyanya alisema kuwa wanasiasa wawe makini na mchakato huo kuepusha hisia zao za kisiasa kwani wasipokuwa makini wanaweza kusababisha zoezi hilo likaingia dosari kwani huu ni wakati wa kutazama maslahi mapana ya taifa.

Hata hivyo alitoa wito kwa waandikisha katika zoezi hilo kuwa makini na kufuata sheria na taratibu walizofundishwa ili kutosababisha mkanganyiko wowote ili zoezi hilo lifanyike kwa umakini na kwa muda unaotarajiwa.

Mwisho

No comments:

Post a Comment