Sunday 24 May 2015

ANASWA NA SILAHA YA KIVITA

Na Gurian  Adolf
Sumbawanga
Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linamshikilia mkazi wa kijiji cha  Mazigo Tarafa ya Inyonga  Wilaya ya Mlele mkoani humo kwa tuhuma za kumkamata na  silaha ya kivita aina ya AK 47  pamoja na Gobore moja.
Mtuhumiwa huyo aliyekamatwa ametajwa kuwa ni  Emanuel  Herman (KAMTUPE) (36) ambae ni mkazi wa Kijiji cha Masigo Tarafa ya Inyonga Wilaya ya Mlele Mkoani  humo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alisema kuwa  tukio la kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo na silaha hizo mbili lilitokea mei 22 majira ya  saa nane usiku  katika  Kijiji hicho cha Masigo.
Kidavashari alisema  mtuhumiwa huyo alikamatwa kufuatia taarifa kutoka kwa raia wema walizozitoa kwa askari wa wanyama pori kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa akimiliki  silaha kinyume cha sheria na amekuwa akizitumia kwa uwindaji haramu.
Baada ya taarifa hizo  kuwafikia askari wa wanyama pori  walianza msako wa kumsaka mtuhumiwa huku wakiwa wanaongozwa na Afisa wa wanyama pori  Cedrick  Mashauri.
 Kidavashari alieleza  katika  msako wa askari  wa wanyama poli  hao walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa  Emanuel  Herman(KAMTUPE) akiwa  na bunduki mbili  moja aina ya   AK 47   na  nyingine  aina ya Gobore.
 Alisema mtuhumiwa alikuwa akimiliki  bunduki hizo  kinyume cha sheria na  alikuwa akizitumia katika ujangiri kwenye uwindaji haramu katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi na kwenye mapori ya akiba.
Mtuhumiwa bado anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi na anatarajiwa kufikiwa mahakamani mara baada ya uchunguzi utakapo kuwa umekamilika.
 Hivi karibuni Askari wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi  waliweza kufanya doria na kufanikiwa kuwakamata watu watatu wakiwa na vipande vitatu vya meno ya Tembo  yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 11 ambayo walikuwa wakitaka kuyasafirisha kutoka kwenye Makazi ya  Katumba Wilaya ya Mlele  kuyapeleka  Mkoa wa Tabora
MWISHO

No comments:

Post a Comment