Na Gurian Adolf
Sumbawanga.
Baadhi ya wazazi katika kata ya Lusaka wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa
wamemuomba kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya hiyo Chrispine
Mrwanda kupeleka ombi lao kwenye baraza la madiwani ili lipitishe kuwa
sheria ambayo itawapa uwezo walimu wa kuwacharaza viboko baadhi ya
wazazi wasiowatimizia mahitaji ya elimu watoto wao.
Ombi hilo walilitoa jana katika viwanja vya serikali ya kijiji hicho
ambapo Idara ya elimu halmashauri hiyo ilikuwa ikifanya ziara yenye
lengo kuboresha ufaulu katika shule za msingi na sekondari ikiwa ni
utekelezaji wa sera ya matokeo makubwa sasa (BRN) katika halmashauri
hiyo.
Mmoja wa wazazi hao Datus Seleman alimuomba kaimu mkurugenzi huyo
kupokea ombi kutoka kwa wazazi wa kata hiyo kuliomba baraza la madiwani
kuanziasha sheria ndogo itakayo waruhusu walimu kuanza kuwachapa viboko
wazazi wote ambao hawawatimizii watoto wao mahitaji ya elimu.
Alisema kuwa wapo baadhi ya wazazi wamekuwa hawajali kuhusu watoto wao
kama wanakwenda hata shuleni ikiwa ni pamoja na kuwanunulia sare za
shule, madaftari na michango mbalimbali kitu ambacho kinapaswa kuwa ni
kosa la kisheria.
Naye bi Maria Maivune alisema kuwa baadhi ya wazazi wamekuwa wakitumia
pesa zao kwa kunywa pombe na kuoa wanawake wengi na hivyo kushindwa
kuwahudumia watoto wao.
"nadhani kama wazazi hao wangekuwa wanacharazwa viboko na walimu labda
wanaweza kubadirika kutokana na aibu ya kuchapwa huenda wakaanza
kuwajali watoto wao".....alisema.
Kwa upande wake kaimu mkurugenzi Mlwanda alisema kuwa halmashauri
itakachopaswa kufanya ni kuwabana wazazi hao ili waweze kutimiza wajibu
wao wakuwapa mahitaji wanafunzui hao ili malengo ya BRN yaweze
kutekelezeka katika Halmashauri hiyo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment