Friday 25 July 2014

Mvuta bangi anusurika kwenda jela miaka miwili

Na Gurian Adolf
Sumbawanga

MUUZA JI wa dawa  za kulevya  aina ya bangi , Ferdinand Makundi (40)
amenusurika  kwenda jela miaka  miwili jela  baada kulipa
faini  ya Sh 100,000- kwa kosa la kukutwa  na  kilo mbili  za bangi.

Hakimu Mfawidhi wa Mahakama  ya Wilaya  ya Nkasi , mkoani Rukwa ,
Ramadhani Rugemalira  alimuhukumu  mshtakiwa huyo  ambaye ni mkazi wa
kijiji cha Mkole  wilayani  humo  kutumikia miaka miwili jela  au
kulipa  faini ya Sh 100,000-  baada ya kukiri kosa lake  mbele ya
mahakama hiyo .

Hata  hivyo mahakama  hiyo ilimwachia  mshtakiwa  huyo  baada ya
kulipa faini  hiyo  mahamani hapo .

Mshtakiwa  huyo  alikiri  kosa lake  hilo  baada ya Mwendesha Mashtaka
, Mkaguzi Msaidizi , Hamimu Gwelo  kumsomea  jana makosa  yake  ya
awali .

Kwa mujibu  wa Gwelo , mshtakiwa huyo  ni mzoefu  kwa  sababu aliwahi
awali  kutiwa  hatiani  na mahakama  hiyo  kwa kosa  la  kukutwa na
dawa  ya kulevya aina ya bangi  pia aliweza  kulipa faini na kuachiwa
hivyo aliiomba  mahakama impatie  adhabu kali  kwa kuwa bado
hajajifunza .

Hati  za mashtaka  mahakamani hapo  zinaonesha kuwa mshtakiwa huyo
alitenda  kosa hilo Mei , 14 mwaka  huu saa saba mchana  akiwa
nyumbani kwake  kijijini Mkole .
Alipotakiwa  kujitetea , mshtakiwa  aliiomba mahakama  hiyo impunguzie
adhabu  kwa kuwa  ana watoto  kumi na  mke  wanaomtegemea .
Mwisho

No comments:

Post a Comment