Saturday 21 December 2013

MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEMPACHIKA MIMBA MWANAFUNZI WA DARASA LA SABA.



MAHAKAMA ya  Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi  imemuachia  huru  Gelald  Gabriel  (18)  mkazi wa mtaa wa Kawajense  aliyekuwa  mshitakiwa wa kesi ya kubaka na kumpa mimba mwanafunzi  wa  darasa la saba wa shule ya Msingi Msakila  (15)  kwa madai ya kutenda kosa  hilo akiwa na umri mdogo.



Akisoma hukumu hiyo  Hakimu  Chiganga aliieleza mahakama kuwa wakati mshitakiwa anatenda kosa hilo desemba 17 mwaka jana alikuwa na umri wa miaka 17  na kutokana na sheria namba 119  inakataza kumuhukumu kifungo  cha kwenda jela  mtu ambaye hajatimiza umri wa miaka 18.



Hakimu Chiganga alisema kuwa Mshitakiwa  kutenda kosa hilo la kumbaka na kumpa mimba  mwanafunzi huyo  nyakati za saa tatu asubuhi  nyumbani kwa mjomba wake ambapo wazazi wa msichana walikuwa wamepanga kwenye nyumba hiyo.



Mshitakiwa alidaiwa kumbaka msichana huyo baada ya kuona  kuwa  watu wote waliokuwa wanaishi kwenye nyumba hiyo  wameondoka kuelekea  kwenye  shughuli zao za kila siku.



Awali kabla ya kusoma hukumu hakimu hiyo, Hakimu Chiganga alimpa mshitakiwa nafasi ya kujitetea ambapo aliiomba mahakama  imwachie huru kutokana  na umri wake  kuwa mdogo wakati akitenda kosa hilo, pia  alidai kuwa  msichana huyo alikuwa akiishi na mjomba wake  ambaye alikuwa hana mke   hivyo hata huo ujauzito msichana huyo anaweza akawa alipewa na huyo mjomba wake waliokuwa wakiishi naye.



Mwendesha mashitaka mkaguzi wa Polisi,  Ally Mbwijo,  baada ya utetezi huo aliiomba mahakama  itoe adhabu kali kwa mshitakiwa kwani  umri sio kigezo cha kumfanya mshitakiwa atende kosa hilo kwa makusudi.



 Hata hivyo Hakimu huyo akisoma hukumu hiyo kwa kueleza hivyo  mshitakiwa Gelald  amenufaika na sheria hiyo hivyo  mahakama inamwachia huru na asirudie tena kutenda kosa hilo  baada ya kuachiwa huru.

No comments:

Post a Comment