Saturday 21 December 2013

CARITAS NA MAENDELEO SUMBAWANGA YATOA MSAADA



MFUKO wa Calitasi na maendeleo wa jimbo katoliki Sumbawanga  lililopo mkoani Rukwa umetoa msaada wa  mabati  40  yenye thamani ya shilingi 500,000 kwa wahanga  wa mvua kubwa ya mawe iliyonyesha katika  kijiji cha Kasense  kilichopo nje kidogo ya Manispaa ya Sumbawanga mkoani humo.

Akikabidhi msaada huo kwa serikali ya kijiji  mkurugenzi wa mfuko huo Padre  Demetrius  Kazonde alisema kuwa lengo la msaada huo ni kuwasaidia baadhi ya watu ambao nyumba zao ziliezuliwa  kabisa paa ili wazikarabati upesi na warejee katika nyumba zao waondokane na usumbufu wanaoupata.

Alisema kuwa kutokana na kuwa tukio lenye ni dharula mfuko huo ulitafuta fedha hizo kidogo na kuanza kutoa huku akiwaomba watu wenye mapenzi mema wajitolee ili kuwasaidia watanzania wenzao wali katika wakati mgumu kuliko kusubilia serikali ndiyo iwasaidie watu hao.

Katika msaada huo padre huyo alikabidhi pia fedha taslimu kiasi cha shilingi 300,000 ambazo alisema alitumwa na askofu wa Kanisa Katoliki jimbo la Sumbawanga  Damian  Kyaruzi  ambapo alisema askofu huyo alitoa fedha hizo ili ziwasaidie wahanga hao katika wakati huo mgumu walio nao.

Naye Ofisa mtendaji  wa  kijiji hicho Joseph  Nandi  alisema kuwa wameupokea msaada huo kwa mikono miwili hasa katika kipindi hiki ambacho wakazi wa kijiji hicho wapo katika wakati mgumu kutokana na wengine kubomoka kwa nyumba zao na hivyo hawana kwa kuishi.

Alisema kuwa wananchi hao wamekuwa wakisaidiana kwani baadhi waliwachukua watu ambao nyumba zao zimeharibika na kuwapa hifadhi hali iliyosababisha kugawana chakula kidogo walicho nacho na hivyo kuhitaji msaada mkubwa ili waweze kuishi katika mazingira bora zaidi.

Akishukuru wa niaba ya watu ambao nyumba zao zilibomoka kufuatia mvua hiyo  Peter  Mwanisawa alisema kuwa msaada huo umetolewa katika wakati muafaka kwani wengi wa watu ambao nyumba zao ziliboka wanahitaji msaada wa vifaa vya ujenzi kwani ukarabati wa nyumba hizo unahitaji fedha nyingi na bahati mbaya hawana fedha za kuweka kufanya ukarabati huo.

No comments:

Post a Comment