Tuesday 2 January 2018

Mbunge atekaleza ahadi

Na Walter Mguluchuma
Katavi
Mbunge wa  Jimbo la  Mpanda  Mjini mkoani  Katavi Sebastian  Kapufi  ametoa msaada wa  baiskeli mbili za kutembele watu wenye  ulemavu ambao hawana uwezo wa kutembea kwa miguu.
Msaada  huo ameutoa ili kukamilisha ahadi  aliyoitoa  wakati  wa ziara aliyoifanya  jimboni  kwake  kwenye  katika  Kata za  Kawajense na  Kasokola ambapo walemavu wawili walimuomba  Mbunge huyo awampe  msaada wa  Baiskeli za  kutembele  na  aliwahidi kuwapatia.
 Wakati  wa  ziara  hiyo mbunge  huyo  alifanya  mikutano ya hadhara  kwenye   Kata  hizo  na  ndipo  alipo ombwa baiskeli hizo.
Akizungumza baada ya kubadhiwa  baiskeli hiyo  Justine  Petro (31) mkazi wa mtaa wa  Kwajense  mwenye  ulemavu wa miguu alisema kuwa anamshukuru mbunge  huyo kwa kuteleleza  ahadi yake  aliyoitoa wakati wa  mkutano wa  hadhara uliofanyika   mwezi  agosti  mwaka  jana.
 Alisema baiskeli  hiyo  itamsaidia  kwani  alikuwa   hawezi kwenda   sehemu  yoyote ile  bila  msaada wa kupelekwa na mtu jambo  ambalo  kuna wakati  lilikuwa  kwake linakuwa  nigumu na  hasa  anapokoseka mtu wa  kumbeba na kumpeleka  anako  taka  kwenda.
Petro alisema kuwa  kuna wakati  alikuwa  akishindwa  hata  kwenda  kanisani  kutokana  na wazazi   wake  kutoku na  fedha  za  kumlipia  boda boda hali iliyozidi kumfanya ajione mpwe.
Mbunge wa  Mpanda  Mjini  Sebastiani   Kapufi alisema  Baiskeli  hizo  mbili  alizotoa kwa walemavu hao zimegharimu kiasi cha sgilingi  900,000 na  ametekeleza  ahadi   aliyokuwa  ameitoa  wakati wa ziara yake aliofanya  katika  kata za  Kawajense na  Kasokola .
 Alisema  yeye  kama    Mbunge wa  Jimbo   ataendelea  kutoa misaada  kwenye  jamii na  wala  hata   sita  kutoa  misaada  kwa  watu  wenye mahitaji  maalumu  kama  alivyofanya  kwa watu hao wawili.
Bibi   Anna  John (58) ambaye naye ni mremavu wakutotembea alimshukuru  mbunge  huyo  kwa  kutoa  msaada huo wa  baiskeli kwa   Justine John (18) nambaye ni mjukuu wake kwani atawapunguzia  gharama za kukodi  boda boda  mara kwa  mara.
Mwisho

No comments:

Post a Comment