Friday 18 August 2017

Ajira afya kuwapa kipaumbele watakaokubairi mazingira magumu kwanza ou

Na walter Mguluchuma
Katavi
Wizara  ya afya Maendeleo  ya  Jamii  Jinsia  Wazee   na   Watoto  inatarajia   kutoa  ajira kwa watumishi wa  kada  mbalimbali za  afya a watakao  pewa  kipaumbele  cha  kwanza  katika   ajira  hizo  ni  wale  wakataoomba  kufanya  kazi katika     Mikoa ya pembezoni ambayo  inaupungufu   mkubwa wa   watumishi wa   Afya.
 Kauli  hiyo  ya  Wizara  ya  Afya  ilitolewa  jana  na  Waziri  wa  Afya  Maendeleo  ya  Jamii Jinsia Wazee  na  Watoto   Ummy Mwalimu  wakati   alipokuwa  akiwahutubia  wakazi wa Manispaa ya  Mpanda  Mkoani   Katavi  katika   uwanja  wa  mpira wa  Polisi   Mpanda  alipokuwa   akifungua  upimaji   na  utoaji   tiba  wa  magonjwa yasiyo  ambukiza.
Waziri   Ummy  Mwalimu    alieleza  kuwa   Serikali  inatarajia  kutangaza  ajira za   watumishi  52,000 wa  kada  mbalimbali  hivi  karibuni   hivyo   kwa   nafasi za  ajira  zitakazo  tolewa  na  Serikali kwa  ajiri ya   Wizara  yake   watatowa  kipaumbele kwa   Mikoa  tisa   ambayo  inaupungufu  mkubwa   wa  watumishi  wa  Afya.
 Alisema  kwa   wale  ambao  watakao  omba  kupangiwa   kufanya   kazi  katika   Mkoa  wa   Dares  salaam  hawata  kuwa   na    nafasi  ya  kuchaguliwa kwanza  kwani    Mkoa  huo  hauna  tatizo  kubwa  kama  ilivyo   Mikoa ya  pembezoni .
Aliitaja  baadhi ya  Mikoa  yenye  upungufu  mkubwa  wa   watumishi wa   kada  ya  Afya  na  ambayo  itapewa  kipaumbele  ili  kupunguza  tatizo  la  watumishi  kwenye  Mikoa  hiyo  kuwa  ni  Mikoa ya  Katavi ,Rukwa ,Kigoma,  Simiyu,   Shinyanga ,  Tabora   Geita  na   Kagera.
Waziri  Mwalimu  pia  alieleza  kuwa   Wizara  ya  yake  imeandaa   mpango wa   kupeleka    Bungeni   mswada  wa  kumtaka  kila  mtu  iwe  ni  lazima kujiunga  na   mfuko wa   Bima ya   afya
  Aliwaonya  watumishi wa   Wizara  hiyo  ambao wanatabia ya  kuchezea  fedha  za  kununulia  dawa  na   aliwataka  waache  mara  moja  na  kwa  wle watakao bainika watachukuliwa   hatua  kali .
Nae   Mkuu wa   Mkoa  wa  Katavi  Meja   Generali Mstaafu   Raphael  Muhuga  alieleza  kuwa  Mkoa wa  Katavi  unajumla ya   Watumishi 692  kati ya watumishi  2,174 wanaohitajika  kati yao  17 ni  watumishi  wa  ngazi  ya Mkoa  na 675 ni wangazi ya  Serikali  za   Mitaa.
Alifafanua  kuwa   Mkoa  wa  Katavi  unajumla  ya  upungufu  wa  watumishi  1,186  sawa   na  asilimia   69 ya  mahitaji ya watumishi.
Kwa  mwaka  wa  fedha  wa  2016 na  2017  Mkoa  na   Halmashauri  zake  tano   umeidhinisha  kuajiri   jumla ya  watumishi wapya  wa  kada   mbalimbali  za  Afya  wapatao  422.
Afisa   Maendeleo   ya   Jamii wa  Mkoa wa   Katavi  Anna  Shumbi   alieleza   kuwa   Mkoa   huo  ni   miongoni  mwa    Mikoa   hapa    nchini    unaoongoza  kwa  mimba za  utotoni .
Alieleza  sababu   zinazochangia  Mkoa  huo  kuwa  na  mimba  nyingi za   utotoni  kuwa   zimekuwa   zikisababishwa   na  wazazi  kuwaacha  watoto wao peke  yao  bila  kuwa  na  uangalizi   hasa   kipindi cha  masika  ambapo  wazazi uhamia  mashambani na kuwaacha  watoto  peke  yao .
Mwisho

No comments:

Post a Comment