Monday 17 July 2017

TRL yawataka waliovamia hifadhi ya reli kuzibomoa nyumba zao

Na Walter Mguluchuma
Katavi
SHIRIKA  la  Reli  Tanzania  TRL  limewataka  limewataka watu waliovamia   hifadhi za  reli na  kujenga   nyumba za  kuishi ndani ya hifadhi  hizo  kuzibomoa wao wenyewe kwa  hiyari kabla shirika hilo halijafanya maamuzi ya kuzibomoa na endapo wakipuuza shirika hilo likibomoa itabidi walilipe shirika hilo kwa kufanya kazi hiyo ya kubomoa. 
Mkurugenzi  mkuu  wa TRL hapa nchini  Masanja Kadogosa  aliyasema hayo jana wakati alipokuwa akizungumza  na  watumishi wa  shirika  hilo katika  stesheni ya  Mpanda  Mkoani  Katavi.
 Alisema kuwa shirika  hilo  halitamvumilia mtu  yoyote   aliyejenga nyumba ndani ya hifadhi  ya  reli  kuendelea  kuishi  kwenye  eneo  hilo kwani ilimetoa muda wa  miezi  sita wawe wamebomoa nyumba  zao na kuondoka Mara moja 
Meneja huyo aliwaonya watu hao  kuwa  endapo  baada  ya   muda  kupita  mtu  yoyote  ambaye  hatakua   hajabomoa  nyumba  yake  shirika litabomoa  na  gharama  husika zitalipwa  na   mtu   aliyejenga  na  kukaidi  agizo la  kubomoa.
Kadogosa  alisema kuwa  kwa  yale  maeneo  ambayo  shirika  litaamua  kujenga  reli na kuwakuta wananchi  wame jenga nyumba watu  hao watalipwa  fidia na  shirika  hilo.
 Hata hivyo  shirika   hilo hivi karibuni  lilitoa   notisi ya  kuwataka  watu  waliojenga  nyumba  katika    maeneo  ya  Msasani na  Tambukaleli  katika   Manispaa  ya  Mpanda   pamoja  na  wakazi wa   Kijiji  cha   Ugala Tarafa  ya   Nsimbo   Wilayani  Mpanda ambao   wamejenga  nyumba  zao ndani ya  hifadhi za  reli  kuhama  na  kubomoa  nyumba  zao  ndani ya   kipiindi cha  siku 30.
Hata  hivyo  Naibu   Waziri wa  Ujenzi   Edwin   Ngoyani  alipokuwa katika ziara hivi  karibu  Mkoani   Katavi  aliwaongezee  muda wa  kuishi  kwenye  maeneo  hayo  hadi  mwezi  januari mwakani.
Naye   Mwenyekiti wa  Bodi ya  Wakurugenzi ya  TRL Prof John  Kondoro   aliwataka  watumishi  wa  TRL wawe  wawazi  kila  wanapofanya  kazi  za  kuwahudumia  wananchi  kama  anavyofanya rais  John   Magufuli  ambavyo   hataki  njia  za  mkato  za  kufanya  kazi kwa  ujanja  ujanja.
  Alisema   shirika  hilo   halitakiwi kuwa   mzigo kwa Serikali   badala  yake  linatakiwa TRL kutoa   ruzuku  kwa  Serikali.
Kwa upande wake Mbunge  wa  Jimbo   la   Nsimno   Richald  Mbogo   alieleza  kuwa   tayari  wananchi  wa  Kijiji  cha  Ugala mameanza  kupimiwa   viwanja  kwa ajiri  ya ujenzi  wa  nyumba zao  ili  waweze  kuhama kwenye  maeneo ya hfadhi ya reli.
Alisema  yeye   kama Mbunge  wa  Jimbo  la  Nsimbo   amesha   andika  barua  ya  kumwomba  Waziri  wa  ujenzi  kuwaongezea  muda   wananchi waliokuwa   wamejenga  nyumba  kwenye   maeneo hayo   iliwaweze  kufanya   maandalizi ya  ujenzi  kwenye  maeneo  waliotengewa.
Mwisho

No comments:

Post a Comment